Nimebadili msimamo kuhusu September 1

britanicca

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
17,216
Reaction score
41,823
Wanajamii wenzangu habari za mda huu,

Kufuatia tangazo ambalo tulitangaziwa na mwenyekiti wetu bwana alikaeli mbowe kuwa September moja ni siku ya maandamano nchi nzima nilikuwa kwenye maandalizi ya kuandamana lakin ntaomba mnisamehe SITAFANYA MAANDAMANO HAYO.

Sababu kuu za kunifanya nisiandamane ni hizi;

1. Amani ya nchi yetu, nimefuatilia nchi kadhaa zilizoitisha maandamano yasiyo na kikomo, zimejikuta hazipati kile zilichotegemea matokeo yake imekuwa ni machafuko ya kupinduana kila Mara na watu wamekuwa wakimbizi wa nchi zao,

2. Pili maandalizi ya September 1 yameingiliwa na JWTZ jambo ambalo ni hatari zaidi, chezea kwa kamanda Sirro lakini si kwa Mwamunyange, yani hujui kusoma hata picha huoni kuwa huyu ni mbuzi huyo ni kondoo? Kujitolea kwa wanajeshi kufanya usafi we upite na mabango yako unaleta FYOKOFYOKO zako na unachafua tena aisee, patella will be dislocated in your body system, ni bora ni kakaa nyumbani kwangu tu.

3. Majukumu yanayonikabili
Majukumu niliyonayo kikazi ni mengi sana, kuna familia na kusomesha watoto, nina wategemezi kibao, nina mipango mingi sana mbeleni sioni sababu ya kufupisha maisha yangu kisa namsaidia LOWASSA na MBOWE kutimiza azima zao.
NOTE THAT ikitokea nikafa kama Mwangosi, au Alphonce Mawazo, nitaishia kutumika kwenye kumbukumbu za kuleta umaarufu wa chama lakini ipo siku wana CHADEMA watanisahau na kutelekeza familia yangu.

4. Tuheshimu katiba ya nchi yetu, ambayo kuna majukumu na wajibu wa raia, ikiwemo kutii sheria na amri za wakubwa akiwemo mkuu wa nchi ambaye kimaandishi hayuko juu ya sheria lakin kiuhalisia neno lake lolote ni sheria, sipaswi kupingana naye, ni wengi kama 30% ya watanzania wanaonekana kumpinga lakini ndiyo rais, hata angepingwa na 90% lakini ameshakuwa rais wetu.

5. Tukio la Jana kati ya lowassa na mheshimiwa Rais limenionesha kuwa wenda hawa wakubwa wanaelewana vizuri tu ila sisi ndiyo madaraja ya kufikia malengo yao, hivyo naamini ipo siku moja nitakuwa katika ngazi fulani kuwatetea wananchi kwa moyo wa dhati hivyo sipaswi kufupisha maisha yangu kwa kuwa daraja la wengine.

NB: Ukizingatia mzee Mkapa ndo alimkata Lowassa baada ya wengine kuwa na kigugumizi July 11, 2015, lakini Lowassa hakujali hayo kaenda kwenye Jubilee yake, siasa si uadui.

6. Muda wa Rais Magufuli madarakani ni mfupi mno kulipo uwepo wa Tanzania, mh Magufuli hawezi kuongoza nchi zaidi ya mwaka 2026, hivyo ngoja tumvumilie tu kama tulivyo wavumilia wengine na madhaifu yao, na huyu mheshimiwa tumvumilue tu muda wake utapita na watanzania watakuwa wameshapata mwamko zaidi juu ya nini wanakitaka toka kwa kiongozi anayechaguliwa na watakuwa na uwezo wa kupima.

7. Matamko ya viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali, matamko ya viongozi wa dini, wawakilishi wa Mungu hapa duniani wametuasa tusifanye maandamano na si vema kuandamana wakati viongozi wenye maono ya Mungu wametuhasa na wanayajua madhara yake.

8. Mimi kama mtanzania niwe mkweli sitaki demokrasia ila nataka wanangu wale washibe, wasome bure, nikitaka kusafiri ndani na nje ya nchi usafiri uwepo, nataka ulinzi, matibabu, maji safi, barabara, umeme, uhuru wa kutembea bila kukabwa na majambazi, kuongezeka kwa kipato changu, kupata huduma kwa haraka bila urasimu, sipendi mazingira ya rushwa yaendelee kuweko, nataka huduma bora, bei ya vitu ishuke, ila sitaki demokrasia alafu nkayakosa hayo. Hivyo ikitokea Rais Magufuli akaninyima nilivyotaja hapo juu naomba nishirikishwe maandamano yasiyo na kikomo, hapa sitamsikiliza yeyote.

9. Familia yangu na ukoo tupo watu 67 kuanzia baba, baba mdogo, mama na mama wadogo na watoto wao, kwa tafiti ndogo niliyofanya wapo wafuasi wa CCM 21 CHADEMA 23, TLP 2 na wengine hawana vyama, nikajiuliza tukiingia barabarani kupingana na kurushiana mawe kumbe kuna uwezekano ukakuta namtupia mzee jiwe la kisogo, naomba Mungu aepushe hiki kukombe,

Hizo ndizo sababu zangu za msingi zilizonifanya kubadili maamuzi ya kuandamana.
 
WAla wewe si WA upande huo, duniani pote mabadiriko huletwa Na wachache tena wanaotukanwa! Msalaba hukuwa Kwa ajili ya wote ila mmoja lakini Leo ni heshima Kwa wakristo
 
WAla wewe si WA upande huo, duniani pote mabadiriko huletwa Na wachache tena wanaotukanwa! Msalaba hukuwa Kwa ajili ya wote ila mmoja lakini Leo ni heshima Kwa wakristo

Unaposema duniani, kwa dunia ya leo unamaanisha kama wapi na wapi?
 
tarehe 16 aug ulikuja na mada yenye kichwa ni ngumu kuipigia kura chadema 2020


ushauri wangu uza viungo vyako ulivyopanga kuviuza
 
mi nakujua vizuri tu wewe we siunauza flani za kijani pale lumumba sasa iweje leo utuambie ulitaka kuandamana kama sikutudanganya pia naskia posho mmeongezewa kwa kazi nzuri mnazofanya mitandaoni
Unaposema duniani, kwa dunia ya leo unamaanisha kama wapi na wapi?
 
mi nakujua vizuri tu wewe we siunauza flani za kijani pale lumumba sasa iweje leo utuambie ulitaka kuandamana kama sikutudanganya pia naskia posho mmeongezewa kwa kazi nzuri mnazofanya mitandaoni

Unasema "duniani kote mabadiliko huletwa na wachache" lete majibu dunia ya leo sehemu gani wameleta mabadiliko kwa maandamano???
swali dogo, mara Lumumba mara tshirt.
 
tarehe 16 aug ulikuja na mada yenye kichwa ni ngumu kuipigia kura chadema 2020



ushauri wangu uza viungo vyako ulivyopanga kuviuza
Kwani kila aliyetakiwa kuandamana ni chadema? Mi ni CUF Mwana UKAWA
 


threads zako zenyewe ni ushahidi tosha kuwa hujawahi na haitatokea wewe kujiunga na mapambano ya ukawa au chadema. ona hii thread yako hapa chini

Ni ngumu na ni aibu kujipanga foleni mwaka 2020 kuwapigia CHADEMA kura
 
Mkuu hiyo no2 kiboko niko kwenye daladala nimetoa kicheko Abiria wote wamenigeukia,ikabidi nimsomee wa pembeni yangu naye anavunja mbavu daladala lote wanacheka
 
kwa nini usiwe mvumilivu kwa kusimamia mile ulichokiamini na kukiandika hapa chini

Pamoja na mapungufu ya Magufuli ilibidi nimchague maana ndo alikuwa na angalau kati ya waliogombea
Ningeandamana kwa kushinikiza afanye mengineyo

Kaa ukijua kwamba
1. Si wote walompigia kura magufuli ni ccm, wengine tuko wapinzani
2. Haimaanishi ukimchagua MTU awe kiongozi kuwa huwez kumkosoa , yapo mengi ya kumkosoa
3. Pia hayo mapungufu nlosema ndo nilikuwa naenda kuandamana ayarekebishe,
4. Ndo alikuwa na uafadhali, angepita lowassa ningeandamana siku hiyo hiyo
 
Mkuu hiyo no2 kiboko niko kwenye daladala nimetoa kicheko Abiria wote wamenigeukia,ikabidi nimsomee wa pembeni yangu naye anavunja mbavu daladala lote wanacheka
Hehehehe ipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…