bendaki
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 952
- 346
Vita huletwa na watawala. Vita huja wakati wachache wawaonapo wengi kuwa ni majuha na watakavyo ndivyo na sivinginevyo. Hutokea pale vyombo vya dola hudanganyika kwa matakwa ya wachache na kutii hata kuua ili wachache watawale watakavyo. Hutokea pale wengi huanza kuwa na uelewa wa kuwa wamekuwa wanadanganywa na vitu visivyo na thamani.
Hutokea pale ardhi inapokuwa haikidhi haja tena aidha kwa kukosekana au mazao ya kilimo kutokithi matakwa. Hutokea pale ajira hazipo na zilizopo wanapeana wachache. Hutokea pale viongozi kuwa na mikakati ya wao na wanaowataka kuendelea kuongoza wakati walio wengi kuwa wamewachoka. Hutokea wakati rasilimali za nchi zinapomilikiwa na wachache kiujanjaujanja.
Hutokea pindi wanafanikiwa kiujanjaujanja kuanza kuwakejeli watawaliwa kwa kutumia matusi, mipasho, nk. Hutokea pindi ahadi zinapokuwa hazitimizwi. Hutokea pindi rushwa, ufisadi, ubadhirifu na serikali kutokuwa na bajeti inayotekelezeka. Hutokea pindi serikali inapo wabebesha watu wake deni kubwa na viongozi kuishi kwa anasa.
Hutokea pale ardhi inapokuwa haikidhi haja tena aidha kwa kukosekana au mazao ya kilimo kutokithi matakwa. Hutokea pale ajira hazipo na zilizopo wanapeana wachache. Hutokea pale viongozi kuwa na mikakati ya wao na wanaowataka kuendelea kuongoza wakati walio wengi kuwa wamewachoka. Hutokea wakati rasilimali za nchi zinapomilikiwa na wachache kiujanjaujanja.
Hutokea pindi wanafanikiwa kiujanjaujanja kuanza kuwakejeli watawaliwa kwa kutumia matusi, mipasho, nk. Hutokea pindi ahadi zinapokuwa hazitimizwi. Hutokea pindi rushwa, ufisadi, ubadhirifu na serikali kutokuwa na bajeti inayotekelezeka. Hutokea pindi serikali inapo wabebesha watu wake deni kubwa na viongozi kuishi kwa anasa.