Nimeamua kuwajibika na kuachia ngazi!

Zinduna

JF-Expert Member
Nov 6, 2011
2,378
3,379
Mwaka mmoja uliopita nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya kutunza mazingira hapa chuoni kwetu na nilipitishwa kwa kura nyingi sana na wanachuo wenzangu na kupata ushindi wa kishindo.

Lakini jana katika mkutano wa mwaka wa kamati ya kutunza mazingira, taarifa yangu ya mafanikio yaliyofikiwa na kamati yangu yameonekana kuwa kinyume na matarajio ya wanachuo wenzangu, kwani kulikuwa na malalamiko mengi sana ya uchafu katika mazingira ya chuo, mitaro kuziba kutokana na uchafu, mazalia ya mbu kutothibitiwa na hivyo kusababisha wanafunzi kuugua malaria kwa kiwango cha kutisha.

Nilikubali udhaifu wa kamati yangu katika kutekeleza majukumu yake kama yalivyoainishwa katika muongozo wa kamati yetu, hivyo niliamua kujiuzulu ili kupisha mtu mwingine mwenye uwezo wa kuongoza.

Nawausia wana JF wenzangu na wananchi wote kwa ujumla, muige mfano wangu, pale inapoonekana mmeshindwa kutekeleza majukumu yenu mliopangiwa hata kama ni majumbani kwenu, basi mkubali kuwajibika na kuachia ngazi.

Nawasilisha!
 
Sijui hata nisemeje
Angel Msoffe inabidi unipongeze kwa kuonesha mfano wa kukubali kuwajibika na kuwapisha wenye uwezo wa kuongoza, mbona simple tu, tena nimepongezwa sana na wanachuo wenzangu kwa kuthibitisha kwamba cheo ni dhamana.
 
Last edited by a moderator:
Lazima utakuwa kiongozi kilaza kuliko wote katika kabineti yenu na ndio maana ukashindwa kutimiza matakwa ya waliokuweka hapo.
 
Mwaka mmoja uliopita nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya kutunza mazingira hapa chuoni kwetu na nilipitishwa kwa kura nyingi sana na wanachuo wenzangu na kupata ushindi wa kishindo.

Lakini jana katika mkutano wa mwaka wa kamati ya kutunza mazingira, taarifa yangu ya mafanikio yaliyofikiwa na kamati yangu yameonekana kuwa kinyume na matarajio ya wanachuo wenzangu, kwani kulikuwa na malalamiko mengi sana ya uchafu katika mazingira ya chuo, mitaro kuziba kutokana na uchafu, mazalia ya mbu kutothibitiwa na hivyo kusababisha wanafunzi kuugua malaria kwa kiwango cha kutisha.

Nilikubali udhaifu wa kamati yangu katika kutekeleza majukumu yake kama yalivyoainishwa katika muongozo wa kamati yetu, hivyo niliamua kujiuzulu ili kupisha mtu mwingine mwenye uwezo wa kuongoza.

Nawausia wana JF wenzangu na wananchi wote kwa ujumla, muige mfano wangu, pale inapoonekana mmeshindwa kutekeleza majukumu yenu mliopangiwa hata kama ni majumbani kwenu, basi mkubali kuwajibika na kuachia ngazi.

Nawasilisha!

chuo gani hicho? chuo madrasa,chuo cha kata au chuo kikuu?
 

.....hata kama ni majumbani kwenu, basi mkubali kuwajibika na kuachia ngazi.


Sasa weee Zinduna, nikiwa kama Baba Mwenye Nyumba na nikashindwa kutekeleza majumu yangu, naachia vipi hiyo ngazi??

Naomba talaka au inakuaje? Natelekeza familia au ni vipi??

Mbona mfano wa kufuata nyayo zako ulioutoa haufananiii????

Na kwanini hukurekebisha mapema hadi ukasubiri mwaka mzima upite hadi kwenye uchaguzi tena ndio ukubali makosa?? Haukuwa na macho Bint???

Kwa style yako binafsi Im sorrrryyyyy.....sifuati mfano wako wa kusubiria mpaka mambo yaharibike kiasi hicho.
 
Lazima utakuwa kiongozi kilaza kuliko wote katika kabineti yenu na ndio maana ukashindwa kutimiza matakwa ya waliokuweka hapo.
Kwa hiyo unamaanisha kwamba hata wale mawaziri waliotemwa na mkuu wa nchi hivi karibuni ni vilaza? Unataka nikuelewe hivyo?
 
Sasa weee Zinduna, nikiwa kama Baba Mwenye Nyumba na nikashindwa kutekeleza majumu yangu, naachia vipi hiyo ngazi??

Naomba talaka au inakuaje? Natelekeza familia au ni vipi??

Mbona mfano wa kufuata nyayo zako ulioutoa haufananiii????

Na kwanini hukurekebisha mapema hadi ukasubiri mwaka mzima upite hadi kwenye uchaguzi tena ndio ukubali makosa?? Haukuwa na macho Bint???

Kwa style yako binafsi Im sorrrryyyyy.....sifuati mfano wako wa kusubiria mpaka mambo yaharibike kiasi hicho.
Uchaguzi wa viongozi hufanyika kila baada ya miaka mitatu, mie nimeachia ngazi baada ya mwaka mmoja tu, si ujasiri huo?
 
Uchaguzi wa viongozi hufanyika kila baada ya miaka mitatu, mie nimeachia ngazi baada ya mwaka mmoja tu, si ujasiri huo?

Okay...umejitahidi!

Haya eleza huo uwajibikaji katika ngazi ya familia, naachia vipi kulingana na mfano wako??
 
Okay...umejitahidi!

Haya eleza huo uwajibikaji katika ngazi ya familia, naachia vipi kulingana na mfano wako??
Unamuachia mkeo madaraka kimya kimya, kwa mfano kusimamia biashara, au kukusanya kodi za nyumba na majukumu yote yaliyokushinda. umeelewa eh!
 
utakuwa zaidi ya kilaza! ulitakiwa ushitakiwe na ufungwe kwa kushindwa kutekeleza majukumu yako, tena ulitakiwa kunyongwa, umesababisha watu wamekufa na malaria, kuharisha na magonjwa ya tumbo. tena ulitakiwa upigwe mawe, na urahaniwe kwa kushndwa kutekeleza majukumu yako, unajisifia upuuzi! nawe ni wale wale!
 
utakuwa zaidi ya kilaza! ulitakiwa ushitakiwe na ufungwe kwa kushindwa kutekeleza majukumu yako, tena ulitakiwa kunyongwa, umesababisha watu wamekufa na malaria, kuharisha na magonjwa ya tumbo. tena ulitakiwa upigwe mawe, na urahaniwe kwa kushndwa kutekeleza majukumu yako, unajisifia upuuzi! nawe ni wale wale!

Hahahaha.....Dah!

Kama hukumu ya viongozi ndio hiyo, basi 2015 sigombei hata kama mabadiriko yanahitajika kwa vijana, Dahhhhh!
 
utakuwa zaidi ya kilaza! ulitakiwa ushitakiwe na ufungwe kwa kushindwa kutekeleza majukumu yako, tena ulitakiwa kunyongwa, umesababisha watu wamekufa na malaria, kuharisha na magonjwa ya tumbo. tena ulitakiwa upigwe mawe, na urahaniwe kwa kushndwa kutekeleza majukumu yako, unajisifia upuuzi! nawe ni wale wale!
Bahati mbaya hatuna sheria hiyo, maana tungekuwa nayo, sidhani kama baraza letu la mawaziri la awamu ya tatu na nne lingesalimika, tungekuwa tumewasahau zamaaani!
 
Hahahaha.....Dah!

Kama hukumu ya viongozi ndio hiyo, basi 2015 sigombei hata kama mabadiriko yanahitajika kwa vijana, Dahhhhh!
Na ndio maana viongozi vijana tunatakiwa kuonesha mfano kama mimi!
 
Back
Top Bottom