Karot
JF-Expert Member
- Mar 6, 2017
- 1,159
- 1,309
Jumapili iwe njema nyote wana JF...
Nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye mada husika.
Kisa ni kikubwa lakini nitajaribu kufupisha ili nisiwachoshe kusoma.
Ni kwamba kuna binti mmoja niliwahi kutembea nae mwaka jana. Lakini tulifikia hatua baada ya wiki mbili akanambia anajihisi ya kwamba ni mjamzito.
Sikuwa na shaka kwakweli maana niliamini kwakua nilikua kila wikiend nikiwa free kazini nakutana nae. Sikubahatika kwenda kumpima kutokana na majukumu kuwa mengi. Nilisafiri kikazi mwaka mmoja na miezi miwili.
Lakini wakati nipo safarini alikua akinipa taarifa mbali mbali za maendeleo yake ya kiafya na mimi nikawa namsaidia. Ikafikia hatua akanambia ameshajifungua salama na hakuna tatizo lolote lililojitokeza kikubwa nimuhudumie mtoto.
Sikuona shida nikawa nafanya hivo lakini kwa shida sana maana nilishawahi kubambikiziwa mimba hewa nikaliwa vyangu mpaka nikachakaa.
Na huyo wa kwanza nae nilikua safarini.
Lakini pamoja na yote, niliku nashindwa kumwelewa kwanini nikimuomba anitumie picha za mtoto inakua mbinde mpaka naanza kumtilia mashaka???
Nilimuomba anitumie picha hizo hadi ikakata miezi kama minne ndo akanitumia... Sasa nikabahatika kutimba nyumbani lakini kwa bahati mbaya yeye alikua Iringa mimi nikawa Zenji.
Mungu si Athumani wiki jana akanambia yupo Dar na mimi kwa bahati nzuri nikawa nina mpango wa kutimba Dar. Nikasema poa itajulikana mbivu na mbichi. Kwa bahati tu jana nimetua Dar na nikajaribu kumtafuta nimuone mtoto wangu.
Nilienda mpaka ghetoni kwake alipopanga, kweli mtoto anae lakini kimbembe kikawa hapa.....
Na hapo ndo nikajua ukweli kwamba kuna kitu nadanganywa.
ITAENDELEA......
Nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye mada husika.
Kisa ni kikubwa lakini nitajaribu kufupisha ili nisiwachoshe kusoma.
Ni kwamba kuna binti mmoja niliwahi kutembea nae mwaka jana. Lakini tulifikia hatua baada ya wiki mbili akanambia anajihisi ya kwamba ni mjamzito.
Sikuwa na shaka kwakweli maana niliamini kwakua nilikua kila wikiend nikiwa free kazini nakutana nae. Sikubahatika kwenda kumpima kutokana na majukumu kuwa mengi. Nilisafiri kikazi mwaka mmoja na miezi miwili.
Lakini wakati nipo safarini alikua akinipa taarifa mbali mbali za maendeleo yake ya kiafya na mimi nikawa namsaidia. Ikafikia hatua akanambia ameshajifungua salama na hakuna tatizo lolote lililojitokeza kikubwa nimuhudumie mtoto.
Sikuona shida nikawa nafanya hivo lakini kwa shida sana maana nilishawahi kubambikiziwa mimba hewa nikaliwa vyangu mpaka nikachakaa.
Na huyo wa kwanza nae nilikua safarini.
Lakini pamoja na yote, niliku nashindwa kumwelewa kwanini nikimuomba anitumie picha za mtoto inakua mbinde mpaka naanza kumtilia mashaka???
Nilimuomba anitumie picha hizo hadi ikakata miezi kama minne ndo akanitumia... Sasa nikabahatika kutimba nyumbani lakini kwa bahati mbaya yeye alikua Iringa mimi nikawa Zenji.
Mungu si Athumani wiki jana akanambia yupo Dar na mimi kwa bahati nzuri nikawa nina mpango wa kutimba Dar. Nikasema poa itajulikana mbivu na mbichi. Kwa bahati tu jana nimetua Dar na nikajaribu kumtafuta nimuone mtoto wangu.
Nilienda mpaka ghetoni kwake alipopanga, kweli mtoto anae lakini kimbembe kikawa hapa.....
Na hapo ndo nikajua ukweli kwamba kuna kitu nadanganywa.
ITAENDELEA......