Habari za muda wakuu,
Natumaini nyote mnaanza mapumziko ya mwisho wa wiki salama,
Turejee kwenye mada tajwa.
Ni kwa muda mrefu sana tumekuwa tukisikia maswala ya kiunyanyasaji yakifanywa na wakufunzi wa vyuo dhidi ya wanafunzi kwa masilahi yao binafsi.
Mfano maswala ya kuwaomba wanafunzi rushwa (fedha au ngono ) ili kuwafaulisha katika kozi zao.
Matukio hayo yamekuwa yakiwaathiri wanafunzi wa jinsia zote lakini athari kubwa zimekuwa zikiwapata watoto wa kike na hii ni kutokana na sababu ya udhaifu walionao kimaumbile n.k, matatizo yanayowakumba kutokana na tabia hizo chafu ni pamoja na matatizo ya kisaikolojia, mimba na hata magonjwa ya zinaa (kama nchi tunapaswa kuchukua hatua)
Binafsi nimewahi kuathirika na mchezo huo mchafu enzi za uanafunzi. Nimekaa kwa muda mrefu sana nikisoma mazingira ya mchezo huu sasa nimeamua kuja na kampeni hii ya kuwafichua wale wote wanaojihusisha na mchezo huu mchafu (ndugu zangu hali ni mbaya sana vyuoni)
Watoto wa kike kama nilivyosema hapo juu, wanaathirika sana na huu upuuzi wa wa kufunzi wasio na maadili katika taaluma zao, wamekuwa wakibaki na maumivu yao mioyoni ikiwauwa ndani kwa ndani.
Sasa nawapa nafasi ya kusema na nitawasaidia kwa namna moja ama nyingine kurejesha furaha na matumaini yao kwa kuwachukulia hatua stahiki wakufunzi walio wavunjia heshima na kuzitesa hisia zao.
Kiukweli ninachukia sana pale ninapoona mwanaume akimliza mwanamke kwa sababu tu ya udhaifu wake, jaribu kuvuta picha mzazi unampeleka mwanao chuo halafu anafelishwa, anapewa mimba au anapewa magojwa na mwalimu aliye aminika umma ili kuielimisha Jamii (inauma usiombe ikukute ndugu)
Jinsi kampeni itakavyofanya kazi, nimeshapandikiza agents katika baadhi ya vyuo (bado nahitaji agents wengi zaidi) hawa watakuwa wakipewa mfunzo endelevu na kazi yao ni kuniletea majina pamoja na details za kutosha za hao wakufunzi wapuuzi wasio na huruma na kizazi chao then mimi nitaendelea na taratibu zingine, ninahitaji wanasheria pia katika jopo langu ili pale kwenye ushahidi wa kutosha tuwaburuze mahakamani hawa wakufunzi wakapambane na majaji kortini.
Ewe mwanafunzi uliyeombwa rushwa ya aina yoyote au uliyenyanyaswa kwa namna yoyote na mwalimu huko chuoni kwako ni PM tuangalie jinsi ya kudeal na hao watu. Nimeamua kufanya hivyo ili kuwapa watu nafasi ya kusema lakini pia hii ni baada ya kuona kuwa nchi inataasisi butu sana kila kona ubabaishaji tupu. Mimi ni private investigator niliyejitolea kuiokoa jamii na ndoto yangu ni kuona vitendo vya namna hiyo vinakoma.
Baadhi yao nitawataja humu live.
Naombeni maoni yenu jinsi ya kuboresha movement hii, ahsanteni.
Natumaini nyote mnaanza mapumziko ya mwisho wa wiki salama,
Turejee kwenye mada tajwa.
Ni kwa muda mrefu sana tumekuwa tukisikia maswala ya kiunyanyasaji yakifanywa na wakufunzi wa vyuo dhidi ya wanafunzi kwa masilahi yao binafsi.
Mfano maswala ya kuwaomba wanafunzi rushwa (fedha au ngono ) ili kuwafaulisha katika kozi zao.
Matukio hayo yamekuwa yakiwaathiri wanafunzi wa jinsia zote lakini athari kubwa zimekuwa zikiwapata watoto wa kike na hii ni kutokana na sababu ya udhaifu walionao kimaumbile n.k, matatizo yanayowakumba kutokana na tabia hizo chafu ni pamoja na matatizo ya kisaikolojia, mimba na hata magonjwa ya zinaa (kama nchi tunapaswa kuchukua hatua)
Binafsi nimewahi kuathirika na mchezo huo mchafu enzi za uanafunzi. Nimekaa kwa muda mrefu sana nikisoma mazingira ya mchezo huu sasa nimeamua kuja na kampeni hii ya kuwafichua wale wote wanaojihusisha na mchezo huu mchafu (ndugu zangu hali ni mbaya sana vyuoni)
Watoto wa kike kama nilivyosema hapo juu, wanaathirika sana na huu upuuzi wa wa kufunzi wasio na maadili katika taaluma zao, wamekuwa wakibaki na maumivu yao mioyoni ikiwauwa ndani kwa ndani.
Sasa nawapa nafasi ya kusema na nitawasaidia kwa namna moja ama nyingine kurejesha furaha na matumaini yao kwa kuwachukulia hatua stahiki wakufunzi walio wavunjia heshima na kuzitesa hisia zao.
Kiukweli ninachukia sana pale ninapoona mwanaume akimliza mwanamke kwa sababu tu ya udhaifu wake, jaribu kuvuta picha mzazi unampeleka mwanao chuo halafu anafelishwa, anapewa mimba au anapewa magojwa na mwalimu aliye aminika umma ili kuielimisha Jamii (inauma usiombe ikukute ndugu)
Jinsi kampeni itakavyofanya kazi, nimeshapandikiza agents katika baadhi ya vyuo (bado nahitaji agents wengi zaidi) hawa watakuwa wakipewa mfunzo endelevu na kazi yao ni kuniletea majina pamoja na details za kutosha za hao wakufunzi wapuuzi wasio na huruma na kizazi chao then mimi nitaendelea na taratibu zingine, ninahitaji wanasheria pia katika jopo langu ili pale kwenye ushahidi wa kutosha tuwaburuze mahakamani hawa wakufunzi wakapambane na majaji kortini.
Ewe mwanafunzi uliyeombwa rushwa ya aina yoyote au uliyenyanyaswa kwa namna yoyote na mwalimu huko chuoni kwako ni PM tuangalie jinsi ya kudeal na hao watu. Nimeamua kufanya hivyo ili kuwapa watu nafasi ya kusema lakini pia hii ni baada ya kuona kuwa nchi inataasisi butu sana kila kona ubabaishaji tupu. Mimi ni private investigator niliyejitolea kuiokoa jamii na ndoto yangu ni kuona vitendo vya namna hiyo vinakoma.
Baadhi yao nitawataja humu live.
Naombeni maoni yenu jinsi ya kuboresha movement hii, ahsanteni.