Niliyoyashuhudia Jeshini

Yani natamani kuingia kwenye Uzi nilipige mbata..Matoto ya Mama kila kitu linalia tu kama mwanamke..Watoto wa Mama ndio hawa wakikutana na Mitiani ya maisha kidogo tu wanajinyonga,Au kutoa ndogo...Sasa apo poti angesema amuombe TIGO dogo ili apunguziw mazoezi unafkiri huyu Mtoto wa Mama asingetoa??
Watoto wa Mama inabidi mjue Dunia ni katili sana hii lazima uwe MGUMU sio Kuonesha huruma na kulia ovyo Haisaidii.Kuna siku utaishi bila mama ndo utajua dunia ni Katili
Huyu ni binti kwa mujibu wa maelezo yake
 
Yani natamani kuingia kwenye Uzi nilipige mbata..Matoto ya Mama kila kitu linalia tu kama mwanamke..Watoto wa Mama ndio hawa wakikutana na Mitiani ya maisha kidogo tu wanajinyonga,Au kutoa ndogo...Sasa apo poti angesema amuombe TIGO dogo ili apunguziw mazoezi unafkiri huyu Mtoto wa Mama asingetoa??
Watoto wa Mama inabidi mjue Dunia ni katili sana hii lazima uwe MGUMU sio Kuonesha huruma na kulia ovyo Haisaidii.Kuna siku utaishi bila mama ndo utajua dunia ni Katili
Kunywa maji punguza hasira mkuu!
 
Course ya kujitolea nisingetoboa
haina utofauti na yenu...wao pia ni short course tu... syllabus yenu na yao haijatofautiana...hivyo unge toboa...

ndio maana Mujibu, na Wazalendo huwa kufa kwenye mazoezi ni nadra sana labda mtu awe alikuwa tu na maradhi yake mwenyezi Mungu akampenda.

full course ndio Balaa ili wakufunzi waonekane wamefanya kazi lazima askari wakate moto...!😭😭😭

 
MITAPENDEZA kama utanalizia episode ya 14.
Tueleze usiku wa kuamkia sherehe ilikuaje,siku yenyewe ya sherehe uli perform vipi karate, usiku wake furaha ulikuaje, safari ya kurudi home.
Mama alikupokeaje stendi, wadogo zako walifurahí vipi kukuona tena stori zilikuaje mpaka muda wa kwenda kulala.
Usiku wa kuamkia sherehe ulikua mzuri, nilipata kombati na buti kama nilivyotamani
Siku ya sherehe niliperform vizuri karate

Nilifurahi nimemaliza course, kesho nikapanda kwenye gari kurudi home hapo nikapata hisia a huzuni nikahisi kumiss jeshi kabla hata ya kufika nyumbani.

Nilivyoshuka ubungo sista angu alikuja kunipokea, naongea nae kwenye simu kumuelekeza nilipo aje kunifata

Nikashangaa mtu amefika nilipo halafu ananipita, nikamuita "dada" alivyogeuka akaanza kucheka "Aisee ndo umekua hivyo! Unajua sikukujua kabisa umebadilika"
Nilivyotoka jeshi nilikua mweusi sana

Mama alifurahi kuniona
Mwanzoni walikua wananishangaa jinsi nilivyochangamka nimekua mchapakazi.

Wadogo wa kupiga nao story kama
ulivyouliza sikua nao, mimi kwetu ndo lastborn.
 
SEHEMU YA 6

NIKAFUNGUA MOYO

Nilifungua moyo niliona sina jinsi pale siwezi kutoka, mateso upande wangu yalipungua kuna ratiba za jeshi nikaanza kuzipenda hivyo sikuons mambo tena kama mateso ila njia ya kujifunza.

Kwanza, saa 10 alfajiri filimbi ikilia nawahi kombania inapigwa rokoo.
Baada ya pale wanaita wagonjwa njoeni upande wa huku, wazima pangeni mistari mabio yanaanza uelekeo road kuu. (Mabio- Jogging)

Nilikua nakimbilia mabio bila kulazimishwa nilikua naenjoy zile chenja sababu zinaongeza morale na My favourite ni hii; (Nimesahau maneno ila anayekumbuka naomba aniandikie)
🎶Kimbwekombweko cheza!
Kimbekele cheza....🎶


WEEK 6
Nakumbuka tulikua kombania usiku tumekaa chini kwenye vumbi bakabaka ana dumu na fimbo akipiga 1 tunasimama akipiga 2 tunachuchumaa akipiga 3 tunalala chini zoezi, push up za kutosha ila hapa girls tulikua tunachekesha sana hizo pushup zetu! Tulikaa mpaka saa 5 tukaenda kulala

Mimi nilikua nikirudi Angani naenda kuoga, kupiga mswaki na marafiki zangu tukirudi tunavaa nguo kabisa ndo tunalala ili filimbi ikipigwa hiyo saa 10 alfajiri ngoma uelekeo kombania.
Basi alfajiri ikafika kila mtu kafunga kikombe chake kwenye pitshort sababu tuliambiwa kuna dharula hivyo kila mtu aende na kikombe kakifunga kwenye pitshort angani kutafungwa hivyo hakuna atakayeweza kuingia.

Kama kawaida mabio umbali kutoka Gongo la Mboto hadi Airport nilikua naenjoy mabio.

Tumerudi kushakucha! tukaambiwa tupange foleni kazi imeanza.

Nilijuta upya kwenda jeshi, Bakabaka wakaanza kurutaaaa fungua moyo kazi imeanza! wote kichurachura uelekeo huu hapa basi tunawafata kwa kichurachura huku wanatuonyesha maeneo ya jeshi kama nyumba zao, jikoni, utawala, mazingira yote. Vuta picha kambi za jeshi zilivyo kubwa sasa tunazunguka kwa kichurachura, mkichoka mnaroll.

Tukachukuliwa hadi kwenye bonde tukaambiwa aya lala chini roll mpaka darajani! Huwa nahisi kambi nyingi zina madaraja chini mteremko wa maji.

Tulikua kimafungu hivyo ni rahisi kusimamiwa na kila mtu anafanya kwa uangalizi mkubwa.
Wazee nikaanza kuroll mpaka darajani nilihisi dunia chungu, kilio sio cha nchi hii njia yenyewe ina kokoto, vumbi.

Tumefika darajani kuna mteremko wa maji yanapita njia bakabaka akasema aya tumbukieni humo ndani ya daraja, muoge sababu tokea mnekuja hamjaoga Sawa kuruti?? Tunaitikia "Ndio sawa afande"

Aisee tukatumbukia fasta sababu ukiremba cha moto utakiona
Wakatuambia hakikisha umejipakaza poda ya kutosha mwili mzima umekua mrembo ndo utoke (poda- vumbi, matope).

Sasa katika harakati za kujipaka matope kuna kitu kikanichimba gotini sijui mpaka leo ni nini damu zikaanza kumwagika kama zote goti linauma
Ikabidi wanitoe nikapelekwa zahanati kufungwa bandage hiyo siku ikawa ponea yangu
Ila wenzangu walisota sana.

Mchana sasa muda wa kula tukaambiwa kila mtu akachukue tofali kituoni dakika 5 uwe usharudi kuchukua msosi.
Mimi nina kidonda nikajua nitaonewa huruma kumbe holaa nikaenda kubeba tofali tunabeba kwenye kipara, wengine wakaeka ngata ya box!

Tulivyofika jikoni wakaanza kukagua walioeka ngata wakakusanywa wakapewa trip zingine wabebe matofali ndo wachukua msosi.
kuruta wengi tulikua tushafungua moyo, vilio malalamishi yalipungua sana.
Baada ya msosi kuruta wote uelekeo shambani hamna kupumzika.

Mjeda namesake akamfata bakabaka "Naomba mabinti wachache wakasafishe maeneo ya mkuu wa kambi
Basi na mimi nikachukuliwa ikawa ponea yangu, mkuu wa kambi alikua anaishi pale.

Jioni tukaenda kula after filimbi uelekeo kombania uwe umemaliza kula ama lah, nikaenda
Tukaanza kufundishwa kwata hapo usiku tunafundishwa zile nyepesi za mwanzo
Hapa nilipata mtihani mpya!😂 nilikua Nanga hatarii mkono siwezi kutupa ipasavyo usiku ule nilichezea mapanzi ya kutosha.

Kwanini wanaojitolea ni wakatili vileee?

Itaendelea.....

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Kila baada ya page ngapi huwa unaendelea
 
Story nishaandika nimemaliza
Safi hongera sana nitakutafuta unisimulie na unioneshe makovu. Wale askari wabaya sana wana roho mbaya wanakutesa binti hujazoea shida? Toka juzi sijalala nawafikiria. Naweza pata majina yao? Pole sana ephen_ ni mijitu tu yenye roho mbaya inafanyia hivyo wenzao.

Pole pia kwa kuandika. Vidole vitakuwa vinauma. Nikupeleke Hosp? Wakaangalie visije kuvimba au kukakamaa. Pole. Next time utaniambia nikutafutie mtu wa kukusaidia kuandika.
 
Safi hongera sana nitakutafuta unisimulie na unioneshe makovu. Wale askari wabaya sana wana roho mbaya wanakutesa binti hujazoea shida? Toka juzi sijalala nawafikiria. Naweza pata majina yao? Pole sana ephen_ ni mijitu tu yenye roho mbaya inafanyia hivyo wenzao.

Pole pia kwa kuandika. Vidole vitakuwa vinauma. Nikupeleke Hosp? Wakaangalie visije kuvimba au kukakamaa. Pole. Next time utaniambia nikutafutie mtu wa kukusaidia kuandika.
Aisee! Unajua kuapologize
Asante kwa hizo offers...
 
Ooooh... Kweli? Nisamehe kama nilikukwaza. Ni mabhangi tu haya napovuta sometimes yes sometimes no. Dr. Kanishauri nikivuta bhangi nisiwe nawasiliana na mtu.

Karibu sana. Je unakunywa wine? Nimtume mtu akuletee. Pole pia kwa uchovu maana kusoma hizi text kunachosha pia.
Yale yaishapita sina kinyongo na wewe,
Nilichukulia unachangamsha genge.

Bhangi sio nzuri kwa afya punguza ukorofi, kwani wewe hauogopi kupigwa na watu wenye hasira kali?

Mimi wine situmii, Asante hata hivyo!
 
Yale yaishapita sina kinyongo na wewe,
Nilichukulia unachangamsha genge.

Bhangi sio nzuri kwa afya punguza ukorofi, kwani wewe hauogopi kupigwa na watu wenye hasira kali?

Mimi wine situmii, Asante hata hivyo!
Kupigwa siogopi. Mi huwa naogopa kupiga tu. Vijana wa siku hizi hawana kitu nale nale sana. Mi huwa nawatandika tu vibao. Ila nitapunguza ukorofi kama ulivyonishauri. Mi wala si mbishi. Ila wakinichokoza nitawatandika makofi na nimeshawapa warning pia wasikusumbue. Wananielewa huwa sipendi upuuzi. Ukiwa na tatizo lolote lile nijulishe.
 
Kupigwa siogopi. Mi huwa naogopa kupiga tu. Vijana wa siku hizi hawana kitu nale nale sana. Mi huwa nawatandika tu vibao. Ila nitapunguza ukorofi kama ulivyonishauri. Mi wala si mbishi. Ila wakinichokoza nitawatandika makofi na nimeshawapa warning pia wasikusumbue. Wananielewa huwa sipendi upuuzi. Ukiwa na tatizo lolote lile nijulishe.
Noted
 
SEHEMU YA 3
Watu tunang'oa visiki huku tunasinzia, yule mjeda namesake akanifata "njoo huku" nikaenda sasa kuna vichaka vingi akanipeleka kichaka flani hivi majani yamekaa kimduara katikati uwazi upepo unapita. Akaniambia "lala hapo muda wa kuondoka ukifika nitakufata" nikapiga zangu mbonji.

Nakuja kushtuliwa na mateke, nimekurupuka namuona bakabaka ananitizama tena ana nyota mbili (bakabaka - mwanajeshi aliyeajiriwa) "toka huko chuchumaa hapa haraka" nikatii amri mzee.
Umefikaje huku? Swali nimepigwa...

Nikafikiria nikaona siwezi kumchoma mjeda namesake ni vyema nipambane na hali yangu.
Nikaanza kujitetea pale, "Mimi naumwa vidonda vya tumbo nimezidiwa nikaona nipumzike hapa" akamwita mjeda hana cheo akamwambia naomba umshughulikie huyu.
Yule mjeda akaniambia "adhabu yako utabeba kisiki kikubwa peke yako kupeleka kambini". Nikaona nishaanza kupata msala mapema muhimu nikurudi nyumbani.

Nimekaa kihuzuni mjeda namesake akaja "nimekutafuta kule sijakuona" nikamwambia nilifumwa nikampa mkasa wote akaniambia nisijali atanisaidia. Kweli saa 4 ikafika filimbi ikalia kisiki kimoja mnabeba watu wawili kwenda kambini. Yule bakabaka akasema yule mwenye adhabu yangu yuko wapi? Nikaenda akanipa kisiki kikubwa machozi yakaanza kunilenga.

Akaniambia unatoka mkoa gani nikamwambia Dar! Akacheka sana "mbona watu wa dar wajanja? Wewe kitu kidogo unalia ebu acha usen....."

Nikapewa kisiki kikubwa peke yangu yeye akaondoka, namesake akawapasia kile kisiki kuruta wengine, akawaita wakaka wawili akawaambia kisiki chao wanipe mimi changu wabebe. Hawakupinga fasta wakabeba.
Kama kawaida uelekeo kambini, umbali kutoka pale shamba hadi huko ni kama 2km, kutembea ni mchakamchaka.

Tumefika tukaenda dining, tukakuta bakabaka kama wote
"Aya kila mtu ana kikombe chake! chukua ndoo nenda kituoni kajaze mchanga ulete hapa ndo uchukue chai"
Kituoni ni kule siku ya kwanza tuliposhuka na gari
Njaa inauma, muda huo nikawa sisikii tena kulia ila hasira kama zote nikajuta kwenda jeshi.

Kufika huko kituoni michanga yenyewe ina maji, nikatiliwa mchanga nikamuomba yule mjeda aniwekee ndoo nusu sababu kipara plus ndoo ya mchanga nzito, akaniwekea.
Niliporudi jikoni kumbe bakabaka wanakagua kama ndoo imejaa au ipo nusu........

Tupo kwenye foleni ya kukaguliwa machozi yananilenga najua kabisa narudishwa nikajaze ndoo, akaja mjeda namesake akaniuliza "ndoo yako imejaa? Nikamwambia hapana
Basi kuna kuruta alikua anapita amerudishwa akajaze ndoo mjeda namesake akamwambia chukua mchanga wako muongezee huyu wewe ukajaze tena!

Yule akupinga akanijaziwa ndoo nikakaguliwa imejaa nikachukua chai na mkate.

Uzuri chai imekolea sukari na mkate mzuri mkubwa nikala nikashiba ila majonzi yakawa palepale ninayo moyoni.

Yaani siwezi kupewa msosi mpaka jasho linitoke?

Nikipata upenyo lazima nimpigie mama aje kunifata.

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
umekuja kula hapa
 
SEHEMU YA 11

2. NGOMA COY

Nilimwambia Anna mimi kwata nishafukuzwa, akanishauri nihamie ngoma coy.
Ngoma coy wanajihusisha na sanaa kuimba, kucheza, kuigiza hivyo.

Nikapiga picha mimi kuigiza, kucheza, kuimba siwezi nitafanyaje sasa? Nikajipa moyo kesho nikaongozana na Anna kitengo.

Nimefika pale bakabaka akaniambia bora umekuja ngoma coy huku utawala kama wote! hamna jua wala kutumia nguvu. Sasa kuna mchujo humu huingii bure, wote unaowaona hapa wamefanya vizuri kipindi cha mchujo.

"Aya imba tukusikie sasa ndo mchujo huu usifanye masihara"
Mimi kuimba sijui
"Sasa hujui kuimba, hapa umefata nini? Aya cheza tuone"
Kuna mziki kabisa kwenye lile hall! Navyokwambia ngoma coy utawala ujue utawala kweli!!
Mziki unapiga nicheze! Anna ananiangalia anacheka tu, nikajikaza kucheza

Naona kuruta wananicheka na mimi najua hapa naharibu tu.
"Weeee! Kuruta kucheza unajua lakini sasa hapa tumeshajaa tupo wengi, jaribu vitengo vingine" akaniambia bakabaka

Majibu hayo tu nikajua nimeboronga kucheza hivyo kanikataa kiaina kama walijua wamejaa kwanini hakuniambia tokea mwanzo?......

Sasa niende wapi! Ngoma coy sijafit ila ningekubaliwa hapa ingekua utawala kama wote.
Nikarudi hangani mapema, sababu muda ulikua umebaki mwingi kuruta wapo vitengoni.
Hairuhusiwi kwenda hangani muda wa kazi hivyo nililala chini ya deka ili bakabaka wakipita wasinione.

Usiku kama kawaida kombania! Ukifika unakaa chini vumbi kama lote. Kipindi hiki tushamaliza zile first weeks za mateso hivyo tukawa hatupewi mazoezi magumu hivyoo!

Tunanyanyua viroba (squats) tukichoka tunaimba chenja mambo yakizidi tunaekewa mziki tucheze bakabaka wetu alikua na speaker ndogo.


3. KITENGO CHA KAZI MCHANGANYIKO
Nilivyotoka ngoma coy nikaja huku sasa.
Kazi mchanganyiko wanadeal na kufyatua tofali na kubeba, kuchimba visiki, kuvuna machungwa na kupukuchua mahindi, kumwagilia bustani ya mbogamboga bondeni, kusafisha vyoo, kufyeka nyasi.

Mwanzo nilijitahidi nikaekwa kundi la kuvuna machungwa! Bakabaka walituambia kula machungwa hadi usaze kubeba hairuhusiwi hivyo nilikula utawala sana shambani.

Mpaka shamba likawa jeupe tumevuna kila kitu
Hivyo kazi ya machungwa baada ya kama wiki ikafa tukawa hatuendi tena.

Nikawa najila ili niende kundi la bustani nikafanikiwa, kule pia utawala sana tunamwagilizia michicha spinach ila tatizo likaja bustani kwenda ni asubuhi na jioni tu. Mchana tunaambiwa twende shambani kung'oa visiki.

Huko shambani mbali kama 2km nikaona hiki kipengele kila siku kubeba visiki nikawa nalalamika sana.
Anna akaniambia kwanini usiende kitengo cha karate?

Nikafunga ukurasa na kazi mchanganyiko nikahamia karate rasmi!

Itaendelea.

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Ngoma coy aka nengu nengu,wanakuwaga walaini sana watoto wa michezo coy.

Kuna jamaa angu alikimbilia nengu nengu baada ya mziki wa kombania kuwa mgumu.

Jeshini kitengo mura,ukiwa na kitengo shuruba zinakuwa chache,kama ukipata nafasi ya kujichanganya kwenye kitengo nenda,iwe ujenzi ,iwe ngoma,iwe mpira au sanaa yoyote

Kukaa bila kitengo ina maana utakuwa kombania mda wote,na kombania haipumziki ,kila kazi zinatazama kombania,kwa hiyo ukiwa kombania kila kazi utafanya,iwe kubeba magogo,kupasua kuni,kubeba tofari,kung'oa visiki,kulima ,kuvuna nk.

Na vibangala vya watu wetu vinakuga na usimamizi sana ,unakuta maafande wapo zaidi ya mmoja mana mnakuwa kuruta wengi hivyo usimamizi unakuwa sio wa mtu mmoja,hali kwenye vitengo usimamizi unakuwa wa viongozi wa kawaida au hakuna kabisa ni kujisimamie wenyewe tu,

Watoto wa kota huwa wanaenda jeshini wana abc za kutosha ,hiyo husaidia kukabiliana na upepo wa kule.
Jeshini ubishi hakuna ,kila kitu ndio afandee hata kama kinakukera moyoni, utafanyaje ,ndo mana unaambiwa fungua moyo

Kumaliza ukuruta ni kazi ngumu sana ,hadi ndege wa angani wakipita wana wahurumia .
Utapauka,utakonda,ngozi itabadilika,wana kutoa umaarufu,hata kwenu ni mambo fresh lakini utakuwa sare tu na mtoto wa mkulimaYAANI NDO MAANA HALISI YA KUKUTOA URAIA NA KUWA ASKARI.
 
Back
Top Bottom