Japokuwa umeichagiza hii habari kama kianzio ili watu washawishike kusoma tangazo lako la biashara,ni vizuri binadamu kusaidiana.
Inasemwa unapomsaidia mtu kama huyo wala hela utakayompa hataijengea nyumba au kununulia gari ila utakuwa umempunguzia maumivu na kumfariji wakati akisubiri mafanikio yake kesho na hii ni sadaka ambayo Mungu anaiona moja kwa moja,hata humu JF wapo watu wanafungua mada wakiwa ktk shida kama mtu una uwezo saidia tu 5K yako utakayompa haimsaidii zaidi ya kushibisha tumbo lake tu.
Wakati mwengine unakuta mlemavu wa macho anatembeza viberiti (nilimkuta K/koo) au mama mtu mzima anauza vitu kama limao au tangawizi (nilimkuta mmoja makutano ya Msimbazi &Twiga anakuwepo asubuhi) msaidie wala bidhaa yake usiichukue maana amejaribu kutokuomba akaona afanye kitu ili kuishi ukimsaidia umemfariji sana.