Nilinusurika kuuvaa mkenge wa mume wa mtu

bongo-live

JF-Expert Member
Jul 3, 2013
1,140
1,292
Katika harakati za kutafuta mume ilikuwa hivi:

Nilipendana na kaka mmoja wa Singida. Huyu kaka aliniambia anataka nimpeleke kwa wazazi ili akajitambulishe na tufunge ndoa kwakuwa mwanzo nilimweleza nataka tufunge ndoa kwanza ndipo nitampa penzi na kwakuwa nilikuwa bado bikra akakubali.

Akaniambia nijiandae nimpeleke kwa wazazi, nikawaza ni wanaume wachache sana watakubali ndoa bila kutest dyudyu. Siku moja nikamwomba niende kwake kumtembelea, akasita kidogo halafu akaniambia usijali kwa leo sitaweza ila nitakualika siku rasmi.

Siku ikafika nikaenda kwake jioni kwenye saa moja hivi nikakaa kwa kiti, macho yngu yanazunguka kuangalia mazingira ya hapo ndani. Nikaona sehemu ukutani pameandikwa 1,3,2,7. Jamani nyumba iliyoishi mtoto haijifichi, nikawazaa nikaona nimtume dukani anifuatie chipsi na soda nina njaa, akakubali.

Kitendo cha kwenda dukani, nikasuburi dakika 5 nikafunga mlango kwa hofu. Nikakagua kabatini, nikakagua uvunguni, ile nimenyanyua godoro nikakutana na chupi za kike tena chafu na kanga. Ile kanga nikaitoa nikaiweka kitandani, aliporudi toka dukani akaikuta akahamaki eti "nilinunua kanga kwa ajili ya kuogea". Nikamwambia poa, hata mimi nataka niwahi nyumbani kaka ni mkali.

Hata kula sikuweza nikaondoka. Jamaa alikuwa kafukuza mke, ningeuvaa mkenge.

Akili ni nywele.
 
Katika harakati za kutafuta mume***ilikuwa hv;;; nilipendana n kaka mmoja wa singida; huyu kaka aliniambia anataka nimpeleke kw wazazi ili akajitambulishe; na tufunge ndoa; kwa kuwa mwanzo nilimweleza nataka tufunge ndoa kwanza ndipo nitampa penzi,kw kuwa nilikuwa bado bikra akakubali; akaniambia nijiandae nimpeleke kw wazazi; duu; :nikawazaaaaa n wanaume wachache sn watakubali ndoa bila kutest dyudyu; cku moja nikamwomba niende kwake kumtembelea; akasita kdg; akaniambia usijali kw leo sitaweza ntakulika ck rasmi;;;;;;cku ikafika nikaenda kwake jion kwenye saa moja hv;;;; nikakaa kw kiti; macho yngu anazunguka kuangalia mazingira y hapo ndani; nikaona sehemu ukutani pameandikwa 1,3,2,7,jmn nyumba iliyoishi mtot haijifichi; nikawazaa nikaona nimtume dukani anifuatie chipsi n soda nna njaa; akabali waooo; kitendo cha kwenda dukan; nikasuburi dkk 5 nikafunga mlango kw hofu; nikakagua kabatini; nikakagua uvunguni; ile nimenyanyua godoro nikakutana na chupi za kike tena chafu;;;; n kanga;ile kanga nikaitoa nikaiweka kitandani aliporudi toka dukani akaikuta akahamaki; et nilinunua kanga kw ajili y kuogea ;;;,nikamwambia poa; ht mimi nataka niwahi nyumbn kaka ni mkali;; ht kula ckuweza nikaondoka,,jamaa alikuwa kafukuza mke ningeuvaa mkenge akili n nywele;;;;;;;
ni mwanaume gani ambaye anajua ananguo za MKE/MWANAMKE ndani alafu akuruhusu tu uje chumbani kwake bila kuzitoa????
 
si mnapendaga uongo...kaona apige fiksi itakuwa rahisikuingia kingi...una bahati umegundua good for you.....maana aliona akikuambi aukweli uatakosanaiko hivo...sokuwa makini ni fundisho before haijatokea effect....umejifunza...wengine wanajifunza yakishatokea
 
akili ni nywele ila zenu mnaweka dawa ndio maana mnazingua

swali ushaolewa au bado bikira
 
Katika harakati za kutafuta mume ilikuwa hivi:

Nilipendana na kaka mmoja wa Singida. Huyu kaka aliniambia anataka nimpeleke kwa wazazi ili akajitambulishe na tufunge ndoa kwakuwa mwanzo nilimweleza nataka tufunge ndoa kwanza ndipo nitampa penzi na kwakuwa nilikuwa bado bikra akakubali.

Akaniambia nijiandae nimpeleke kwa wazazi, nikawaza ni wanaume wachache sana watakubali ndoa bila kutest dyudyu. Siku moja nikamwomba niende kwake kumtembelea, akasita kidogo halafu akaniambia usijali kwa leo sitaweza ila nitakualika siku rasmi.

Siku ikafika nikaenda kwake jioni kwenye saa moja hivi nikakaa kwa kiti, macho yngu yanazunguka kuangalia mazingira ya hapo ndani. Nikaona sehemu ukutani pameandikwa 1,3,2,7. Jamani nyumba iliyoishi mtoto haijifichi, nikawazaa nikaona nimtume dukani anifuatie chipsi na soda nina njaa, akakubali.

Kitendo cha kwenda dukani, nikasuburi dakika 5 nikafunga mlango kwa hofu. Nikakagua kabatini, nikakagua uvunguni, ile nimenyanyua godoro nikakutana na chupi za kike tena chafu na kanga. Ile kanga nikaitoa nikaiweka kitandani, aliporudi toka dukani akaikuta akahamaki eti "nilinunua kanga kwa ajili ya kuogea". Nikamwambia poa, hata mimi nataka niwahi nyumbani kaka ni mkali.

Hata kula sikuweza nikaondoka. Jamaa alikuwa kafukuza mke, ningeuvaa mkenge.

Akili ni nywele.
Ssa hiyo 1,3,2,7 hujatuambia ina maana gani?
 
Hongera kwa kutegua tego. Sasa kama hiyo bikra bado ipo, njoo mimi nikuoe, sina mke na wala sijafukuza mke. Am purely a single boy...
 
Back
Top Bottom