Nilimwambia usimkubalie kama tahadhari

Nilimwambia usimkubalie kama tahadhari

msani

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2011
Posts
1,800
Reaction score
1,194
Sijui ni tamaa au ujinga au ndio style yake.

Ninafanya kazi Wizara fulani mkoani Arusha alikuja dada mmoja ofisini kuja kunisalimia maana tulisoma naye na ni rafiki yangu wa karibu sana.

Kwenye hiyo ofisi bosi ni kiwembe balaa na tulikuwa tunajua kuwa ameathirika na ukimwi. Kila binti mrembo akiingia pale alikuwa anatongozwa na wengi waliingia mkenge. Siku hiyo akaingia huyo binti mrembo rafiki yangu na alipotoka tu nikaitwa ofisini na kukawa na maongezi ya kikazi lkn moyoni nilijua kuna la ziada maana namfahamu.

Kweli mwisho wa mazungumzo akiniulizia yule binti nikamwambia ni rafiki yangu na kuhusu uhusiano nikajibu ni rafiki yangu pia. Akaniomba namba yake nikamwambia nitampa baada ya kuomba ruhusa.

Nikamwambia binti na kumweleza nilivyobanwa huku na bosi,binti akasema we mpe,nikatekeleza! Ila jioni ila baada ya siku 2 tukaonana na yule binti nikamwambia kuwa pale sio salama na kwamba kumwambia vile sio kwamba namuona ni mwepesi la hasha bali kumtahadhalisha na binti akasema anajua jinsi ya kumuhendo na kwamba atakwama mwenyewe.

Siku moja baada ya wiki 3 nipo kwenye hoteli moja ghafla macho yangu yakawa yanakataa kuamini kilicho mbele yangu na mara bosi naye anakutana na macho yangu na kunisalimu na kuniambia wapo hapo wanapumzika kidogo na binti yule yule rafiki yangu.

Sasa sijui kamwambia bosi niliyomueleza au kaamua kunyamaza?

Sijui ni tama au nini?

Huyu binti kaingia cha kike maana wamekuja wengi wanalia hapa ofisini na nimefuta na namba yake.

Sijui nilifanya kosa anyway ngoja nisubiri wiki ianze nitaona mwelekeo utanipa majibu kama kaambiwa au la.
 
kumuita mtu mgonjwa while hauko sure ni kuhisi tu na ku guess guess sio vizuri.....inawezekana huyo binti anaijua vizuri status yake ndo maana kaamua kujilipua.......yawezekana mgonjwa ni binti aliepaswa kuwa warned ni huyo Boss...all in all ujifunze kuto ongea yale ambayo ukiulizwa 'evidence' huwezi kutoa.....
 
Sa we kinakuuma nini..kama mie hata nisingesumbuka kuandika uzi JF..
 
mmmmmmmmmmmmmmh...........!
 
Umeamua kuja kunitangaza hapa JF? Sasa tutaona nani mbabe kati yangu na wewe!
 
kumuita mtu mgonjwa while hauko sure ni kuhisi tu na ku guess guess sio vizuri.....inawezekana huyo binti anaijua vizuri status yake ndo maana kaamua kujilipua.......yawezekana mgonjwa ni binti aliepaswa kuwa warned ni huyo Boss...all in all ujifunze kuto ongea yale ambayo ukiulizwa 'evidence' huwezi kutoa.....

shikamoo braza
 
Mkuu umeongea vizuri sana..tuache kugeneralize mambo kwa hearsay..
Huku uswahilini yaani kila mtu ni daktari...yaani full kupima kina cha maji kwa miguu..
Wakati mwingine huwa napata shida pale mtu 'anapojifanya ananionea huruma mimi wakati na yeye yakwake yanamshinda'..Afu huyo binti ni mtu mzima aachwe afanye maamuzi yake..utamzuia kwa huyu kwa sababu 'unamjua' ..je? akiwa mbali na wewe?

kumuita mtu mgonjwa while hauko sure ni kuhisi tu na ku guess guess sio vizuri.....inawezekana huyo binti anaijua vizuri status yake ndo maana kaamua kujilipua.......yawezekana mgonjwa ni binti aliepaswa kuwa warned ni huyo Boss...all in all ujifunze kuto ongea yale ambayo ukiulizwa 'evidence' huwezi kutoa.....
 
Wadada hatuna maana. Na hasa mbele ya hela. So usishangae kama kasema.
 
Sijui ni tama au ujinga au ndio style yake!!!Ninafanya kazi wizara Fulani mkoani arusha alikuja dada mmoja ofisini kuja kunisalimia maana tulisoma naye na ni rafiki yangu wa karibu sana. Kwenye hiyo ofisi bosi ni kiwembe balaa na tulikuwa tunajua kuwa ameathirika na ukimwi. Kila binti mrembo akiingia pale alikuwa anatongozwa na wengi waliingia mkenge. Siku hiyo akaingia huyo binti mrembo rafiki yangu na alipotoka tu nikaitwa ofisini na kukawa na maongezi ya kikazi lkn moyoni nilijua kuna la ziada maana namfahamu. Kweli mwisho wa mazungumzo akiniulizia yule binti nikamwambia ni rafiki yangu na kuhusu uhusiano nikajibu ni rafiki yangu pia. Akaniomba namba yake nikamwambia nitampa baada ya kuomba ruhusa. Nikamwambia binti na kumweleza nilivyobanwa huku na bosi,binti akasema we mpe,nikatekeleza! Ila jioni ila baada ya siku 2 tukaonana na yule binti nikamwambia kuwa pale sio salama na kwamba kumwambia vile sio kwamba namuona ni mwepesi la hasha bali kumtahadhalisha na binti akasema anajua jinsi ya kumuhendo na kwamba atakwama mwenyewe. Siku moja baada ya wiki 3 nipo kwenye hoteli moja ghafla macho yangu yakawa yanakataa kuamini kilicho mbele yangu na mara bosi naye anakutana na macho yangu na kunisalimu na kuniambia wapo hapo wanapumzika kidogo na binti yule yule rafiki yangu. Sasa sijui kamwambia bosi niliyomueleza au kaamua kunyamaza? Sijui ni tama au nini? Huyu binti kaingia cha kike maana wamekuja wengi wanalia hapa ofisini na nimefuta na namba yake!Sijui nilifanya kosa....anyway ngoja nisubiri wiki ianze nitaona mwelekeo utanipa majibu kama kaambiwa au la!!!!

Hukufanya vyema kuzungumzia afya ya mtu ambaye hata uhakika hauna.

Uwezekano wa huyo binti kumtonya bosi wako juu ya vile ulivyosema ni mkubwa mno.

Especially kama jamaa litakuwa lihongaji ama ligegedaji lizuri.
 
wivu ni kidonda umeshiriki ugua pole


naimba tu
kataa tuone
 
Huyo binti alidhani pengine unamuonea wivu na unamtaka.
Nimewahi kuona case kama hiyo....my sista alikuwa na mpenzi wakaachana, baada ya kuachana akasikia yule mwanaume anamfukuzia mtu mwingine aliyekuwa mke wa mtu anayeaminika alikufa kwa ngoma. Kwa sababu walikuwa na mawasiliano bado my sista akajaribu kumshauri kwamba unapoenda pale sipo si ulimuona mumewe alivyokuwa anafungwa nepi? (kipindi hicho dawa za kupunguza makali hazikuwa za bwelele kama ilivyo sasa). Yule mwanaume hakuelewa akadai wivu unamsumbua na kashfa nyingi juu. Akaendelea akaweka ndani.....hivi ninavyoandika wote wawili ni marehemu.
 
Ishu Hapo ni kupunguziana virusi,huku kwetu tunakawaida ya kusema "Ngoma Droo"
 
Back
Top Bottom