kwaku the traveler
JF-Expert Member
- Feb 12, 2023
- 308
- 848
Ilikuwa Saa 8 inaenda saa 9 usiku, weekend, nimekaa zangu Getto usingizi sipati nikasema ngoja nitoke niende town.
Basi bhana nikaenda club moja hivi inaitwa The Boss ipo Mianzini Mataa (Arusha), wenyeji itakuwa wanafahamu hicho kiwanja.
Bhasi nimezuga zuga hapo saa 8 inaenda 9 nikaondoka. Basi bhana nimefika maeneo fulani wanaita Sakina Triple A kwa juu kidogo wanaita Manguruweni karibu na White Rose bar, kuangalia mbele naona machalii wanne wapo wamepaki bike (toyo) pembeni wanasubiria mwenzao atoke waingie wengine.
Nilipofika yale maeneo nimeshangaa usiku hivi mbona bike ipo imepaki bila mtu halafu gafla nasikia kama kelele kwa mbali, aisee naangalia vizuri kwa mbali kidogo wale jamaa mmoja aliniona wakashituana chapu wakawasha bike wakakimbilia roughroad inapanda kwa juu huko.
Kumbe ile sauti ni mwanamke aisee, chapu akanikimbilia kunishika kabisa analia, aisee ilikuwa so. Basi nikamchukua, nikamuuliza ilikuwaje hadi usiku huu unatembea?
Akaniambiya alikuwa anatoka kazini alikuwa kaingia night, kwahiyo boda aliyopanda hela ilipelea wakamtua hapo, kwao kutoka lilipotokea tukio ni kama dakika 10 hivi, kuna kanisa kubwa jipya huko mbele ndiyo mitaa yao.
Nikamwambiya nakupeleka kwenu, akawa hataki. Yaani anaogopa bado, lakini nilifanikisha. Hadi leo huwa ananishukuru sana.
Tukio lilitokea mwaka 2021.
Basi bhana nikaenda club moja hivi inaitwa The Boss ipo Mianzini Mataa (Arusha), wenyeji itakuwa wanafahamu hicho kiwanja.
Bhasi nimezuga zuga hapo saa 8 inaenda 9 nikaondoka. Basi bhana nimefika maeneo fulani wanaita Sakina Triple A kwa juu kidogo wanaita Manguruweni karibu na White Rose bar, kuangalia mbele naona machalii wanne wapo wamepaki bike (toyo) pembeni wanasubiria mwenzao atoke waingie wengine.
Nilipofika yale maeneo nimeshangaa usiku hivi mbona bike ipo imepaki bila mtu halafu gafla nasikia kama kelele kwa mbali, aisee naangalia vizuri kwa mbali kidogo wale jamaa mmoja aliniona wakashituana chapu wakawasha bike wakakimbilia roughroad inapanda kwa juu huko.
Kumbe ile sauti ni mwanamke aisee, chapu akanikimbilia kunishika kabisa analia, aisee ilikuwa so. Basi nikamchukua, nikamuuliza ilikuwaje hadi usiku huu unatembea?
Akaniambiya alikuwa anatoka kazini alikuwa kaingia night, kwahiyo boda aliyopanda hela ilipelea wakamtua hapo, kwao kutoka lilipotokea tukio ni kama dakika 10 hivi, kuna kanisa kubwa jipya huko mbele ndiyo mitaa yao.
Nikamwambiya nakupeleka kwenu, akawa hataki. Yaani anaogopa bado, lakini nilifanikisha. Hadi leo huwa ananishukuru sana.
Tukio lilitokea mwaka 2021.