Nilikuwa teja sasa ni mchungaji

Nilikuwa teja sasa ni mchungaji

Sasa ndugu Mchungaji usisahau ukifanikiwa kutoa charity najua mateja wengi watakaotaka kupata motivation hizo buku saba watazitumia kwa jambo lingine..., hence kwa kusaidia jamii, ukishapata za kutosha tengeneza pdf (haina gharama) wape wadau vijiweni bure (ingawa watakupiga mawe) ila ndio utumishi wenyewe huo

Addiction ni mbaya sana bora wawe addicted kwenye Imani (no matter hata kama imani hio ni ya ukweli au hapana, so long as haidhuru wengine)
Asante kwa ushauri mzuri ukweli nimeishi maisha hayo najua ubaya wake.

Napambana naomba Mungu anisaidie nipate hela ambayo itanisaidia mbali kutoa PDF nitoe vitabu kwenye sober house mbalimbali.

Ili wale wote wanao pata huduma kwenye hivyo vituo wawe na muda wa kusoma hizi shuhuda za kuwajenga
 
Mara nyingi ninapo kaa chini, na kutafakari safari nzima ya maisha yangu,

kule Mungu alikonitoa, mpaka hapa aliponifikisha, naishiwa maneno ya kumshukuru.

Ndio maana hata sasa ninasema ya kwamba Yeye ni Eben-Ezer, nikimaanisha ya kuwa Mungu ndiye amenisaidia, kufika hatua hii niliyofikia.

Maneno ya kitabu cha Zaburi 119:17 yanayosema; "Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, ili nipate kujifunza amri za Mungu” yanaelezea sana ushuhuda mzima wa maisha yangu.

Magumu, shida na mahangaiko yote niliyopitia vimetumika kama daraja la kunivuta karibu sana na Mungu.

Zaidi ya mimi binafsi kuokolewa, ninaamini ushuhuda wa maisha yangu unaniweka kwenye nafasi ya kuwa msaada kwa wengi walio katika changamoto kama nilizopitia mimi.

Karibu ujipatie nakala ya kitabu changu kinachokwenda kwa Jina la #NILIKUWA_TEJA_SASA_NI_MCHUNGAJI

Kitabu hiki kinapatikana kwa bei nafuu kabisa ya shilingi 7,000/= za kitanzania.

Unaweza kununua nakala yako kwa

Tigo Pesa
0659-409447

M-PESA 0767 879406

Airtel Money 0789 795435

Hakikisha unanitumia na majina yako kamili.

Kwa huduma ya (delivery) utachingia nauli kidogo.
Barikiwa
@pastorwinner80
Ukonga
February 12,2021View attachment 1701077View attachment 1701078
We sema unauza vitabu achana na mbwembwe za uchungaji,
 
Wengi tunafahamu, kwa maisha ya mjini inapofika kipindi cha sikukuu, kama vile ‘Christmass’ na Mwaka mpya watoto hufanyiwa mambo mengi mazuri na wazazi wao. Nikiwa mjini naishi kwa ndugu zangu, kipindi cha sikukuu kilikuwa ni kipindi ambacho nilikuwa naongezewa uchungu na chuki.

Watoto wenzangu wote walikuwa wananunuliwa nguo za sikukuu kasoro mimi. Zaidi ya yote, siku za sikukuu wao wanapelekwa matembezini wakiwa wamependeza, lakini mimi ninaachwa nyumbani kama mlinzi.

Mambo ya namna hii ni mazito sana kwa
mtoto kuyabeba.

Ni mambo ambayo kwa mzazi/mlezi anayeyafanya anaweza asione madhara yake, lakini ukweli ni kwamba yanasababisha majeraha makubwa sana ndani ya nafsi za watoto na yanaacha kumbukumbu hasi ambazo zitadumu maisha yake yote.

Hali ilikuwa vivyo hivyo inapofika wakati wa shule kufungua, baada ya likizo kuisha. Watoto wenzangu wote walikuwa wakifurahi kwenda shule, wakiwa na sare mpya zenye kupendeza.

Lakini kwangu mimi hali ilikuwa ni kinyume chake. Hakukuwa na dalili hata kidogo ya kwamba nitapelekwa shule.

Roho yangu ilikuwa inaniuma sana, ila sikuwa na la kufanya. Sababu kurudi kwetu nilikuwa siwezi mana baba ni kama alidhamiria kuniua,

Kosa kidogo tu alikuwa ananishika ananifunga kamba miguu na mikono ananipiga kwa mjeredi wa kuchapia ng'ombe hadi nikawa napoteza fahamu na masikio kuziba.

Siwezi sahau siku ambayo mama yangu mzazi aliamua kutoka kijijini kuja mjini. Lengo lake lilikuwa ni kuwashawishi baadhi ya ndugu wenye uwezo wanisomeshe, japo elimu ya msingi.

Mbele ya macho yangu, mama alijibiwa kwamba, “Ndugu, kama ni dhambi, basi leo hii Mungu na atuhesabie kuwa tumekataa kuishi na kumsomesha mtoto wa ndugu yetu.”

Tokea wakati huo, niliapa moyoni na kujisemea, ni heri kuishi maisha ya mtaani kama chokoraa lakini niwe na uhuru. kuliko kukaa nyumba moja na
ndugu au jamaa kama mtumwa nisiye na thamani yoyote Itaendelea...........
 
Pole na hongera kwa kuitikia mwito wa kuwa pastor, ila kwa ushauri ungeendeleza kisa chako kwa urefu kidogo hapa JF kabla ya kuhamishia wasomaji wako kwenye kitabu.nafikiri ingekusaidia kuvuta attention ya watu kabla ya kuwa direct kwenye kitabu chako.
Ila yote na yote..ubarikiwe sana na Bwana kwa kukubali wito wa kumtumikia.
 
Pole na hongera kwa kuitikia mwito wa kuwa pastor, ila kwa ushauri ungeendeleza kisa chako kwa urefu kidogo hapa JF kabla ya kuhamishia wasomaji wako kwenye kitabu.nafikiri ingekusaidia kuvuta attention ya watu kabla ya kuwa direct kwenye kitabu chako.
Ila yote na yote..ubarikiwe sana na Bwana kwa kukubali wito wa kumtumikia.
Asante kwa ushauri
 
Mara nyingi ninapo kaa chini, na kutafakari safari nzima ya maisha yangu,

kule Mungu alikonitoa, mpaka hapa aliponifikisha, naishiwa maneno ya kumshukuru.

Ndio maana hata sasa ninasema ya kwamba Yeye ni Eben-Ezer, nikimaanisha ya kuwa Mungu ndiye amenisaidia, kufika hatua hii niliyofikia.

Maneno ya kitabu cha Zaburi 119:17 yanayosema; "Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, ili nipate kujifunza amri za Mungu” yanaelezea sana ushuhuda mzima wa maisha yangu.

Magumu, shida na mahangaiko yote niliyopitia vimetumika kama daraja la kunivuta karibu sana na Mungu.

Zaidi ya mimi binafsi kuokolewa, ninaamini ushuhuda wa maisha yangu unaniweka kwenye nafasi ya kuwa msaada kwa wengi walio katika changamoto kama nilizopitia mimi.
Mchungaji ni vyema utoe ushuhuda wako hapa watu wasome wenyewe kule Mungu amekutoa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom