Nilikuwa sijaamini mpaka nilipohakikishiwa na mtu wa karibu kwamba mfalme wa kisiwa cha hapo Guam analindwa na wanajeshi wa nchi tofauti

Yaite mapovu ila Mkuu Daudi Mchambuzi ungetumia uwezo wako wa kuchambua kwa upande wa pili maana kuna hombwe la uongozi. Viongozi wanahama, mnadai wananunuliwa. Ruzuku inaliwa mnajifanya hamjui. Viongozi wanatema chuki, mnadai ndiyo demokrasia ya kukosoa. Kweli "Nyani hajui kundule!"

Majuu husema "charity begins at home" siye tuna msemo "Toa boriti jichoni kwako ..." au "Ya Ngoswe mwachie Ngoswe mwenyewe". Mnaandika mengi ya chuki na kejeli lakini kumbe hamjui upande wenu watu wanatembea uchi. Wafunikeni.
upo nje ya mada kabisa.

Punguza jazba.
 
Acheni uchochezi na wivu, nchi yetu imepiga hatua sana mpaka wanajeshi wa nchi nyingine wanajikuta wanashindwa kujizuia mpaka wanaamua kuja kuomba ajira kwenye nchi yetu, hili ni jambo la kupigiwa mfano duniani kote. Hakuna nchi yoyote iliyoweza kuweka "vivutio vya wanajeshi" kama nchi yetu tukufu. Na hizi ni "juhudi" kubwa za raisi wetu mtukufu na sasa ni dhahiri shairi tunaenda kuishinda hii "vita ya kiuchumi".

Inaburudisha sana wanajeshi wa nchi jirani kuja kuomba ajira kwenye jeshi letu ilihali vijana wa JKT tena wasomi wanasota mtaani bila ajira!!!
 
...bado umeamini ujinga ambao kamwe hauwezekani,..nchii hii ni makini vyombo vya usalama visingekubali tz1 alindwe na hao vilaza wa Rwanda never
...nina imani kubwa na vyombo vyetu vya usalama
Huwezi amini kwa sababu huwa huamini nakushauri endelea kutoamini
 
...bado umeamini ujinga ambao kamwe hauwezekani,..nchii hii ni makini vyombo vya usalama visingekubali tz1 alindwe na hao vilaza wa Rwanda never
...nina imani kubwa na vyombo vyetu vya usalama
Shanagaa, hivi kwanza inaanzaje hii yeye nani atoe order ya kulindwa na wanajeshi wanje Ili iweje!
 
Kama mwandishi anamaanisha TZ,anaongopa.Mimi nawafahamu baadhi ya vijana wa usalama wanaolinda pale Ikulu.Walio wengi ni wasukuma ambao tulikuwa tunaishi nao hapa Geita.
Hata yule Kanali anayekaa nyuma ya Rais anafahamika ni mtanzania aliyechukua nafasi ya yule Mhehe.
 
Kama mwandishi anamaanisha TZ,anaongopa.Mimi nawafahamu baadhi ya vijana wa usalama wanaolinda pale Ikulu.Walio wengi ni wasukuma ambao tulikuwa tunaishi nao hapa Geita.
Hata yule Kanali anayekaa nyuma ya Rais anafahamika ni mtanzania aliyechukua nafasi ya yule Mhehe.
Dah, wewe ndo unaleta lingine. Amekwambia vijana wote ni wa kutoka kwa mtu mrefu? Halafu kumbe mmewekana WASUKUMA?
 
Nimesikitika sana sana sana,
Inamaana ukilindwa na wanajeshi wa nchi tofauti hapo hekaluni ndo wanaopigana vita ya uchumi utawashinda?

Nilimpuuza Dada mmoja anaishi anapokaa Mr ticha wa profesa Jay, aliposema kuna mfalme wa Guam analindwa na wanajeshi wa kanchi ka pembeni yake, nilimbishia ni kadhani ni kwakuwa yuko mlengo wa kushoto,

Lakin jana nimeamini kabisa na nimeshangaa sana

Nimeamini so kila habari ni ya kupuuza hata kama ni ya kipuuzi

Mungu awabariki watu wa Guam
Taifa la Guam lililojaa mang'ombe wanajionea sawa tuu
 
Kama hujui kitu uliza, kuuliza siyo ujinga. Hadithi za vijiweni zibaki huko huko ili ulinde heshima yako uliyojijengea JF.

Mada zako siku hizi zina harufu ya chuki ya wazi ikimaanisha ni mmoja wa hao waliokuwa wakifaidika na usimamizi mbovu wa sheria za nchi hii.

HAKIKA NAMBA mnaisoma sasa. Mtabaki kulialia humu JF tu, maana hamna mnaloweza kufanya. Kama mlikuwa na mawazo ya kumwondoa madarakani, nje ya utaratibu wa kura, imekula kwenu, Mkuu.
Mbona povu jingi kiasi hiki?
 
Naamini Mungu ndiye mlinzi wangu tosha. Iweje naingia ndani ya nyumba ya ibada huku nimeva hirizi. ? Why Vatican Popes are protected by Swiss soldiers over decades invece gli Italiani?
Mbona unachanganya Vatican's na Guam? Vatican's ina President, ina Bunge, ina Mahakama? Halafu hujui ile ni nchi iliyondani ya Italy? Usichanganye mambo wewe. Ebu nenda kale labda njaa inakuwehua!!
 
Sasa hao walinda usalama wa Guam wanajisikiaje wanapoona bosi wao analindwa na askali kutoka Venezuela na wao wapo?
Ina maana jeshi la Guam halina ujuzi nasio madhubuti kumlinda kiongozi wa Guam ila Jeshi la Venezuela ni makini zaidi ya Guam.
Sasa huyo Bosi wa Guam anawalipa nini hao Venezuela, kifupi wamekubaliana nini kwa kazi hiyo?
Kuna mwana usalama mmoja aliyeasi Guam kuna maneno mazito alishawahi kuongea zidi ya bosi wa Guam na Venezuela.
Chama kinachotawala Guam kinatakiwa kijifunze sasa kutenganisha siasa na vyombo vya vya usalama vya Guam..
Sasa uzalendo wa huyu kiongozi mkuu wa Guam uko wapi kama analindwa na walinda usalama kutoka Venezuela.
Ina maana yule bosi wa venezuela anajua siri zote za Guam na akitaka kutuuza anatuuza tu... duh hatari sana..
 
Back
Top Bottom