Nilikutana na jini wa kike

Nilikutana na jini wa kike

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,951
Nilikuwa najiuliza kila siku niweze kusema hili jambo leo nimepata nimeona ngoja niseme.

Jambo lenyewe lilikuwa kama ifuatavyo:-
Ni kama miaka 10 hivi iliyopita wakati tunasoma chuo. Nilikuwa napendelea sana kwenda beach za kigamboni kuvinjari siku za weekend.

Ilikuwa siku ya jmosi, kama ilibyokuwa kawaida yetu wakati ule kuogelea, huku tukiwafundisha warembo namna ya kuogelea. Wakati mingine tulikuwa tukimaliza kabisa stori zote ndani ya maji na tukitoka kwenye maji tumekuwa wepesiiii.

Watoto wazuri walikuwa wanapenda sana kuogelea na mimi nadhani ilitokana na sura yangu ya mvuto na ucheshi nilikuwa nao. Ni warembo wengi sana wamepita mikoni mwangu. Na jinsi wakati ule livyokuwa kiwembe, sikuacha kuchana popote nilipopita. Nilikuwa na tabia ya kuweka kumbukumbu kila wembe wangu unapopita ninaandika kwenye kitabu changu cha kumbukumbu.

Hebu sasa tuachane na swala hilo la kufundisha warembo wengi kuogelea tuongelee hii issue nyeti ambayo nimekaa nayo moyoni miaka yote hii kumi bila kumwabia yeyote. Nimeona sehemu nzuri yakuwea kuongea yangu ya moyoni ni humu JF.

Sasa basi kwa tabia zangu zile za kupita kila sehemu na nyoa vichwa tofauti tofuati, siku ile nilikwaa mkoko mzuri sijawahi kuuone katika dunia hii. Wakati naogelea na warembo wakiwa wamenizunguka nikamuona kwa mbaali mrembo mkali sana. Aah sikufanya ajizi nikajisogeza kama kawaida yangu. Nilianza kutema sumu zangu. Mtoto mrembo, kavaa nguo za kuogelea zimechora umbo lake namba nane, meno meupe pee. Dah! Akanitajia jina lake kuwa anaitwa Tausi.

Timbwili langu likaanza sasa. Mara nikaliamsha dude. Nikasema Tausi si tusogee mbele zaidi tuogelee maana hapa maji ni machafu. Mtoto akatabasamu na kusema sawa. Nilimshika mkono na kuanza kusogea mbali zaidi na kadamnasi.

Nilizungusha mkono wangu kwenye kiuno chake. Mtoto mlaini mno. Mtoto alinisogelea karibu joto la mahaba likaongezeka. Mrembo alikuwa akinukia manukato aina ya "Filomena perfume" Huku pumzi yake ikawa inaongezeka, huku kinywa chake kikitoa pumzi ya mahaba.

Ngoja nikatishe stori hapo. Nilijikuta navamia tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya bila hata kufikiria chochote. Sasa basi mtoto alinizamisha chini ya bahari. Nikajikuta nipo kwenye dunia nyingine kabisa.

Nimeitwa kidogo nje narudi kuwapa issue hii ...
 
Ukirudi usisahau kuanza kwa kusema "hadithi inaendelea" maana hata hukuanza na "hadithi hadithi" ili hadhira iitikie "hadithi njoo, UONGO njoo"
 
Nimerudi sasa. Si unajua sisi huku tunakaa uswazi jambo dogo tu lazima kieleweke. Kitaa chetu hakuna cha dogo, hakuna cha kupotezea. Ukipita bila kusalimia lazima wazee wa kitaa wakufanyie kikao. Ukija mitaa yetu huku kama umetoka maeneno ya Masaki, Mbezi nk lazima ufuate protocol kusalimia wazee wa kitaa.

Sasa basi hebu tuendelee na hili swala la jini Tausi...
Rafiki yangu katika maisha yangu sijawahi kufika kileleni. Hakika siku hiyo ndiyo ilikuwa ya kwanza.
Nilizamishwa chini ya bahari yaani chini kabisa. Nikajikuta nipojuu ya kitanda huku Tausi akiwa juu yangu. Kitanda kile kilikuwa kimezungushiwa vito vya thamani. Kilikuwa kinang'aa sana. Madini niliyoyagundua pale ni dhahabu tu, maana nimewahi kuwa mmoja wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu maeneo ya Nyangalata Kahama.
Utamu ulikuwa wa hali ya juu sana chini ya bahari. Ngoja nikusimulie vitu nilivyoviona huko ambavyo huku kwetu hakuna kabisa:-

Kwanza chini ya bahari kuna viumbe wanafanana kabisa na watu. Na asilimia kubwa wanatumia lugha ya kiswahili. Kwa hiyo kwangu haikuwa ngumu sana kuongea na viumbe hao. Chini ya bahari technolojia yao iko juu sana, maana TV za huko ni za 4D. Yaani unaona, unasikia unahisi na kama harufu ya ubwabwa unapikwa kwenye TV unapata harufu yake. Dah!! sijui niendelee. Maana naogopa huyu jini asije akarudi tena.

 
Liwalo na liwe maji ukiyavulia nguo ni sharti kuyaoga.
Ngoja natumbua jipu hili:-
Mambo mengi sana niliyaona huko chini ya bahari.
Baada ya kumaliza shughuli zote mimi na Tausi. Nilijikuta nimezungukwa kila upande. Tausi akasimama akasema baba huyu ndiye nilikuwa ninamtafuta siku zote hizo nimeenda huku na huko. Leo yupo hapa nyumbani. Wote walio kuwa pale wakapiga makofi huku kelele za shangwe zikipigwa.

Mimi nilibaki kuduwaa tu sijui niko wapi. Nilikuwa natetemeka sana. Baadae akatokea mzee hivi wa makamo akasema mwanagu asante sana kwa jitihada zako ulizozifanya. Sasa hivi nitakusamehe umetuletea zawadi.

Mzee akanigeukiwa akaniambia, unajua nyie wanadamu ni wadhaifu sana, katika ulimwengu wetu huu wa majini wewe ni kitoweo tu. Umeletwa hapa ili tufanye tambiko. Baada ya siku saba tutakuchinja na ili sisi tuendelee kuishi milele.

Unajua wanajamvi naogopa sana kuongelea swala hili. Japo nasikia sasa sauti kwa mbaali Tausi akiniita naikumbuka sauti yake...
 
Nilikuwa najiuliza kila siku niweze kusema hili jambo leo nimepata nimeona ngoja niseme.

Jambo lenyewe lilikuwa kama ifuatavyo:-
Ni kama miaka 10 hivi iliyopita wakati tunasoma chuo. Nilikuwa napendelea sana kwenda beach za kigamboni kuvinjari siku za weekend.

Ilikuwa siku ya jmosi, kama ilibyokuwa kawaida yetu wakati ule kuogelea, huku tukiwafundisha warembo namna ya kuogelea. Wakati mingine tulikuwa tukimaliza kabisa stori zote ndani ya maji na tukitoka kwenye maji tumekuwa wepesiiii.

Watoto wazuri walikuwa wanapenda sana kuogelea na mimi nadhani ilitokana na sura yangu ya mvuto na ucheshi nilikuwa nao. Ni warembo wengi sana wamepita mikoni mwangu. Na jinsi wakati ule livyokuwa kiwembe, sikuacha kuchana popote nilipopita. Nilikuwa na tabia ya kuweka kumbukumbu kila wembe wangu unapopita ninaandika kwenye kitabu changu cha kumbukumbu.

Hebu sasa tuachane na swala hilo la kufundisha warembo wengi kuogelea tuongelee hii issue nyeti ambayo nimekaa nayo moyoni miaka yote hii kumi bila kumwabia yeyote. Nimeona sehemu nzuri yakuwea kuongea yangu ya moyoni ni humu JF.

Sasa basi kwa tabia zangu zile za kupita kila sehemu na nyoa vichwa tofauti tofuati, siku ile nilikwaa mkoko mzuri sijawahi kuuone katika dunia hii. Wakati naogelea na warembo wakiwa wamenizunguka nikamuona kwa mbaali mrembo mkali sana. Aah sikufanya ajizi nikajisogeza kama kawaida yangu. Nilianza kutema sumu zangu. Mtoto mrembo, kavaa nguo za kuogelea zimechora umbo lake namba nane, meno meupe pee. Dah! Akanitajia jina lake kuwa anaitwa Tausi.

Timbwili langu likaanza sasa. Mara nikaliamsha dude. Nikasema Tausi si tusogee mbele zaidi tuogelee maana hapa maji ni machafu. Mtoto akatabasamu na kusema sawa. Nilimshika mkono na kuanza kusogea mbali zaidi na kadamnasi.

Nilizungusha mkono wangu kwenye kiuno chake. Mtoto mlaini mno. Mtoto alinisogelea karibu joto la mahaba likaongezeka. Mrembo alikuwa akinukia manukato aina ya "Filomena perfume" Huku pumzi yake ikawa inaongezeka, huku kinywa chake kikitoa pumzi ya mahaba.

Ngoja nikatishe stori hapo. Nilijikuta navamia tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya bila hata kufikiria chochote. Sasa basi mtoto alinizamisha chini ya bahari. Nikajikuta nipo kwenye dunia nyingine kabisa.

Nimeitwa kidogo nje narudi kuwapa issue hii ...
kindergatennnnnnnnnnnnnnnnnnn
 
Liwalo na liwe maji ukiyavulia nguo ni sharti kuyaoga.
Ngoja natumbua jipu hili:-
Mambo mengi sana niliyaona huko chini ya bahari.
Baada ya kumaliza shughuli zote mimi na Tausi. Nilijikuta nimezungukwa kila upande. Tausi akasimama akasema baba huyu ndiye nilikuwa ninamtafuta siku zote hizo nimeenda huku na huko. Leo yupo hapa nyumbani. Wote walio kuwa pale wakapiga makofi huku kelele za shangwe zikipigwa.

Mimi nilibaki kuduwaa tu sijui niko wapi. Nilikuwa natetemeka sana. Baadae akatokea mzee hivi wa makamo akasema mwanagu asante sana kwa jitihada zako ulizozifanya. Sasa hivi nitakusamehe umetuletea zawadi.

Mzee akanigeukiwa akaniambia, unajua nyie wanadamu ni wadhaifu sana, katika ulimwengu wetu huu wa majini wewe ni kitoweo tu. Umeletwa hapa ili tufanye tambiko. Baada ya siku saba tutakuchinja na ili sisi tuendelee kuishi milele.

Unajua wanajamvi naogopa sana kuongelea swala hili. Japo nasikia sasa sauti kwa mbaali Tausi akiniita naikumbuka sauti yake...
Mkuu, umekula viroba nini
 
Majin Tausi yote huwa na jinsia mbili hivyo kuwa makini sana mkuu
 
Liwalo na liwe maji ukiyavulia nguo ni sharti kuyaoga.
Ngoja natumbua jipu hili:-
Mambo mengi sana niliyaona huko chini ya bahari.
Baada ya kumaliza shughuli zote mimi na Tausi. Nilijikuta nimezungukwa kila upande. Tausi akasimama akasema baba huyu ndiye nilikuwa ninamtafuta siku zote hizo nimeenda huku na huko. Leo yupo hapa nyumbani. Wote walio kuwa pale wakapiga makofi huku kelele za shangwe zikipigwa.

Mimi nilibaki kuduwaa tu sijui niko wapi. Nilikuwa natetemeka sana. Baadae akatokea mzee hivi wa makamo akasema mwanagu asante sana kwa jitihada zako ulizozifanya. Sasa hivi nitakusamehe umetuletea zawadi.

Mzee akanigeukiwa akaniambia, unajua nyie wanadamu ni wadhaifu sana, katika ulimwengu wetu huu wa majini wewe ni kitoweo tu. Umeletwa hapa ili tufanye tambiko. Baada ya siku saba tutakuchinja na ili sisi tuendelee kuishi milele.

Unajua wanajamvi naogopa sana kuongelea swala hili. Japo nasikia sasa sauti kwa mbaali Tausi akiniita naikumbuka sauti yake...
Mbona huendeleii na story, hata kama umetunga we malizia tu...
 
Back
Top Bottom