Niliitwa mshirikina/mchawi kisa kuwarushia mchele ndege

craq

JF-Expert Member
Mar 22, 2017
859
1,865
Katika harakati za kutafuta maisha na kujipatia pesa ya mkate nilibahatika kufungua frame yangu ambayo ilikuwa inahusika na ICT services kama kufunga networks nk ,pia kwa pembeni frame iliyofuatia niliwaajiri vijana 3 ambao walikuwa ni mafundi Ac na fridge hivyo tukipata dili aidha ya kufungia majumba za watu,kutengeneza,kusafisha nk kazi inakuwa inaendelea kama kawaida..

Kuna tabia nilijiwekea na imekuwa kama mazoea pale ofisini kuna miti imetuzunguka hivyo ndege hujazana mida ya jioni ,wakati wa kufunga ofisi na kuondoka huwa nachukua mchele na kuwarushia na wale ndege kwa furaha hulia na kuimba na kula zile punje za mchele,wale ndege mpaka wamenizoea ikifika jioni lazima utawakuta mtini na kama muda ukichelewa utawasikia wakilia basi naenda duka la jirani na kuchukua punje kadhaa na kuwarushia.Hakika urafiki wangu na hao ndege pamoja na njiwa umekuwa mkubwa mpaka wamenizoea nahisi siku nisipokuwa ofisini huwa wanasikitika na kuhudhunika

Sasa kumbe waswahili walikuwa wananichunguza na wakanikariri na maneno yakaanza mara mimi ni mshirikina ,mchawi ,nimepewa masharti na mganga na biashara yangu inategemea nyota na masharti na kitendo ninachofanya ni matekelezo ya masharti ya mganga.

Hayo maneno walikuwa wakiyazungumza chini chini na kusambaziana na kila ikifika jioni wakawa wananichunguza kama nitawarushia mchele hao ndege au laa.Bahati nzuri kuna msamaria mwema ananiheshimu na akanitonya na kunieleza hali halisi na kwa utafiti wangu nimehakikisha ni kweli naitwa mshirikina ,wale ndege eti ndio wanavuta watu kwenye biashara.

Mie nimebaki nacheka tu sababu siku zote nilikuwa sifahamu kama kuna watu walikuwa wananihisi mshirikina mpaka sasa hivi kisa tu kuwapa mchele ndege ..

Sasa waungwana mie nilikuwa ninafanya fair tu kuwapa chakula ndege na urafiki tu wa kawaida na hao viumbe ile nikiwaona wanaruka ruka na kufurahi wakila,na tukirudi nyuma mimi nilikuwa mfugaji mzuri tu wa Njiwa haswa aina ya fantail tausi,spidi ,vibwenzi,chotara nk labda athari ya ufugaji na mahusiano hayo yameniathiri.

Nataka kusitisha kuwarushia ndege hao mchele ili vijimaneno yamalizike na taswira yangu isiharibike lakini pia nataka niendelee tena nizidishe maradufu kama maneno izidi kusemwa,kuwarushia mchele ndege imekuwa nongwa khaa

Sema waTanzania wenzangu tubadilikeni ,vijimaneno,umbeya haufai tena wengine vidume kabisa wana ndevu hata mshipa wa haya hawana
 
Katika harakati za kutafuta maisha na kujipatia pesa ya mkate nilibahatika kufungua frame yangu ambayo ilikuwa inahusika na ICT services kama kufunga networks nk ,pia kwa pembeni frame iliyofuatia niliwaajiri vijana 3 ambao walikuwa ni mafundi Ac na fridge hivyo tukipata dili aidha ya kufungia majumba za watu,kutengeneza,kusafisha nk kazi inakuwa inaendelea kama kawaida..

Kuna tabia nilijiwekea na imekuwa kama mazoea pale ofisini kuna miti imetuzunguka hivyo ndege hujazana mida ya jioni ,wakati wa kufunga ofisi na kuondoka huwa nachukua mchele na kuwarushia na wale ndege kwa furaha hulia na kuimba na kula zile punje za mchele,wale ndege mpaka wamenizoea ikifika jioni lazima utawakuta mtini na kama muda ukichelewa utawasikia wakilia basi naenda duka la jirani na kuchukua punje kadhaa na kuwarushia.Hakika urafiki wangu na hao ndege pamoja na njiwa umekuwa mkubwa mpaka wamenizoea nahisi siku nisipokuwa ofisini huwa wanasikitika na kuhudhunika

Sasa kumbe waswahili walikuwa wananichunguza na wakanikariri na maneno yakaanza mara mimi ni mshirikina ,mchawi ,nimepewa masharti na mganga na biashara yangu inategemea nyota na masharti na kitendo ninachofanya ni matekelezo ya masharti ya mganga.

Hayo maneno walikuwa wakiyazungumza chini chini na kusambaziana na kila ikifika jioni wakawa wananichunguza kama nitawarushia mchele hao ndege au laa.Bahati nzuri kuna msamaria mwema ananiheshimu na akanitonya na kunieleza hali halisi na kwa utafiti wangu nimehakikisha ni kweli naitwa mshirikina ,wale ndege eti ndio wanavuta watu kwenye biashara.

Mie nimebaki nacheka tu sababu siku zote nilikuwa sifahamu kama kuna watu walikuwa wananihisi mshirikina mpaka sasa hivi kisa tu kuwapa mchele ndege ..

Sasa waungwana mie nilikuwa ninafanya fair tu kuwapa chakula ndege na urafiki tu wa kawaida na hao viumbe ile nikiwaona wanaruka ruka na kufurahi wakila,na tukirudi nyuma mimi nilikuwa mfugaji mzuri tu wa Njiwa haswa aina ya fantail tausi,spidi ,vibwenzi,chotara nk labda athari ya ufugaji na mahusiano hayo yameniathiri.

Nataka kusitisha kuwarushia ndege hao mchele ili vijimaneno yamalizike na taswira yangu isiharibike lakini pia nataka niendelee tena nizidishe maradufu kama maneno izidi kusemwa,kuwarushia mchele ndege imekuwa nongwa khaa

Sema waTanzania wenzangu tubadilikeni ,vijimaneno,umbeya haufai tena wengine vidume kabisa wana ndevu hata mshipa wa haya hawana
Usirudi nyuma,wacha waseme na endeleza ukarimu wako kwa hao viumbe.Binadamu tumeumbwa kusema
 
What a coincidence! Mimi huwa nawawekea mchele barazani kwangu kila asubuhi, maana naishi kwenye apartment! Wakati naishi na wazee nilikuwa nawawekea kwenye garden! Its really a beautiful feeling indeed! Usiache endelea na tabia hii na Mola at akubariki ndugu yangu!
 
Katika harakati za kutafuta maisha na kujipatia pesa ya mkate nilibahatika kufungua frame yangu ambayo ilikuwa inahusika na ICT services kama kufunga networks nk ,pia kwa pembeni frame iliyofuatia niliwaajiri vijana 3 ambao walikuwa ni mafundi Ac na fridge hivyo tukipata dili aidha ya kufungia majumba za watu,kutengeneza,kusafisha nk kazi inakuwa inaendelea kama kawaida..

Kuna tabia nilijiwekea na imekuwa kama mazoea pale ofisini kuna miti imetuzunguka hivyo ndege hujazana mida ya jioni ,wakati wa kufunga ofisi na kuondoka huwa nachukua mchele na kuwarushia na wale ndege kwa furaha hulia na kuimba na kula zile punje za mchele,wale ndege mpaka wamenizoea ikifika jioni lazima utawakuta mtini na kama muda ukichelewa utawasikia wakilia basi naenda duka la jirani na kuchukua punje kadhaa na kuwarushia.Hakika urafiki wangu na hao ndege pamoja na njiwa umekuwa mkubwa mpaka wamenizoea nahisi siku nisipokuwa ofisini huwa wanasikitika na kuhudhunika

Sasa kumbe waswahili walikuwa wananichunguza na wakanikariri na maneno yakaanza mara mimi ni mshirikina ,mchawi ,nimepewa masharti na mganga na biashara yangu inategemea nyota na masharti na kitendo ninachofanya ni matekelezo ya masharti ya mganga.

Hayo maneno walikuwa wakiyazungumza chini chini na kusambaziana na kila ikifika jioni wakawa wananichunguza kama nitawarushia mchele hao ndege au laa.Bahati nzuri kuna msamaria mwema ananiheshimu na akanitonya na kunieleza hali halisi na kwa utafiti wangu nimehakikisha ni kweli naitwa mshirikina ,wale ndege eti ndio wanavuta watu kwenye biashara.

Mie nimebaki nacheka tu sababu siku zote nilikuwa sifahamu kama kuna watu walikuwa wananihisi mshirikina mpaka sasa hivi kisa tu kuwapa mchele ndege ..

Sasa waungwana mie nilikuwa ninafanya fair tu kuwapa chakula ndege na urafiki tu wa kawaida na hao viumbe ile nikiwaona wanaruka ruka na kufurahi wakila,na tukirudi nyuma mimi nilikuwa mfugaji mzuri tu wa Njiwa haswa aina ya fantail tausi,spidi ,vibwenzi,chotara nk labda athari ya ufugaji na mahusiano hayo yameniathiri.

Nataka kusitisha kuwarushia ndege hao mchele ili vijimaneno yamalizike na taswira yangu isiharibike lakini pia nataka niendelee tena nizidishe maradufu kama maneno izidi kusemwa,kuwarushia mchele ndege imekuwa nongwa khaa

Sema waTanzania wenzangu tubadilikeni ,vijimaneno,umbeya haufai tena wengine vidume kabisa wana ndevu hata mshipa wa haya hawana
Wamezaliwa wanasema...na sio kama ukiacha watakosa la kusema. Fanya unalojua ni jema maneno waachie wao.
 
Endelea kuwarushia. Tena uwe unawapiga na picha unaturushia na humu. Anzisha na kakampeni ka kulisha na kupenda wanyama. Pia hakikisha unawaelimisha hao mburula kuhusu umuhimu na maana ya unachokifanya. Watanzania wengi ni wajinga sana.
 
What a coincidence! Mimi huwa nawawekea mchele barazani kwangu kila asubuhi, maana naishi kwenye apartment! Wakati naishi na wazee nilikuwa nawawekea kwenye garden! Its really a beautiful feeling indeed! Usiache endelea na tabia ii na Mola at akubariki ndugu yangu!
Kuna kile kitabu cha primary kuna hadithi ya mzee anafuga ndege hadi mwewe na bundi.unakumbuka?
 
Kuna kuku alikimbilia chumbani kwangu, nikaanza kumfuga, baba mwenye nyumba akaniita akasema huyu kuku anaweza kua katumwa hivyo nimtupe.

Mimi nikaweka ngumu, baada ya muda yule kuku akaanza kutaga, yai moja kila siku. Yule baba mwenye nyumba akanifuata tena akaniomba nimuuzie.

Nikamuuzia, ikawa kuku akiachiwa anakimbilia chumbani kwangu. Baba mwenye nyumba akaona anachoka kila siku kufuata mayai yake ndani kwangu akamla yule kuku.
 
Kuna kuku alikimbilia chumbani kwangu, nikaanza kumfuga, baba mwenye nyumba akaniita akasema huyu kuku anaweza kua katumwa hivyo nimtupe.

Mimi nikaweka ngumu, baada ya muda yule kuku akaanza kutaga, yai moja kila siku. Yule baba mwenye nyumba akanifuata tena akaniomba nimuuzie.

Nikamuuzia, ikawa kuku akiachiwa anakimbilia chumbani kwangu. Baba mwenye nyumba akaona anachoka kila siku kufuata mayai yake ndani kwangu akamla yule kuku.
Jamani poor kuku!
 
Tangu siku nilipogundua kuwa unapofanikiwa idadi ya fitina na majungu yanayokuhusisha na uchawi ndo huongezeka huwa sina hofu tena na nikiona mtu wanasema mchawi kwa kuwa tu anamaendeleo au vinginevyo sichangii hiyo mada. we Fanya kile roho inapenda
 
Mkuu Kaza Kamba Watasema Watachoka Tu Mimi Huwa Naenjoy Sana Nikiwa Nyumbani Nawarushia Punje Za Mchele Na Mtama Hadi Raha Kuwatazama Na Wakizoea Ukifika Muda Tu Lazima Waje
 
Mkuu ni heri uendelee na wema wako kwa hao ndege kuliko kusikiliza maneno ya walimwengu
wahenga walisema "Bora umfadhiri mbuzi utakunywa mchuzi na sio binadamu wana maudhi".
 
Maneno huumba mkuu, kama wanasema kuwa kujaa kwa ndege ndio kujaa kwa wateja wako basi hawajui kuwa wanakubashiria heri. Endelea kulisha ndege kama kawaida na waache waseme.
Binadamu tumeumbwa kuongea hasa pale tunapokosa la kufanya, kama lisingekuwa la kulisha ndege hakika wasingekosa lingine la kukusemea.
Kipimo cha mafanikio yako ni idadi ya uongo unaotungwa juu yako. Usishangae kesho akazuka mwingine na kuanza kulisha ndege pia akidhani ni siri ya mafanikio yako na hapo ndio ujue ukiona unasemwa sana juwa hayo ni matamanio yao juu ya ulichonacho.
 
Kaka crag ni mazoea mazuri sana hayo wala usiache, ki ukweli hao ndege watakujua wote na watakuwa wanakuja wengi tu , nilishwahi kufanya hivyo, nilikuwa kila asubuhi nafungua dirisha na kuwatupia mikate na walizoea hasa, na siku ukichelewa kuamka utashangaa wanakuja kugonga kioo cha dirisha kwa kelele sana

We endelea tu, ukweli wewe mwenyewe na Mungu wako ndio unaujua
 
Kuna kuku alikimbilia chumbani kwangu, nikaanza kumfuga, baba mwenye nyumba akaniita akasema huyu kuku anaweza kua katumwa hivyo nimtupe.

Mimi nikaweka ngumu, baada ya muda yule kuku akaanza kutaga, yai moja kila siku. Yule baba mwenye nyumba akanifuata tena akaniomba nimuuzie.

Nikamuuzia, ikawa kuku akiachiwa anakimbilia chumbani kwangu. Baba mwenye nyumba akaona anachoka kila siku kufuata mayai yake ndani kwangu akamla yule kuku.
Hawa viumbe wana mjua mzuri kwao na mbaya wao
 
Back
Top Bottom