Nilidhalilishwa sana, ila mambo yamebadilika!

Nilidhalilishwa sana, ila mambo yamebadilika!

carter

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2009
Posts
3,664
Reaction score
4,272
Habar ya j3 wana jamvi! Polen kwa uchovu wa wkend!

Nakumbuka ni takribani miaka 5 sasa nikiwa nafanya kazi kama papaa chalii mkoni Arusha. Nilichagua kupangiwa kituo cha kazi Arusha ili niwe naishi nyumban as mnajua kazi yenyewe hailipi sana na pia ndo nlikua naanza maisha so ingekuwa ngum kupanga.

Kwa elimu nlikuwa form 6 leaver ila mzee wangu alikuwa na rank kubwa huko kwenye kaz so hakupenda niende chuo akanitupa kwenye geshi.

bas afta kuanza kazi hyo nikapa girlfrend! Ikabid nipange chumba maeneo ya Sanawari ili nipate muda wa kujinafasi na huyu mpenz wangu! Tulikuwa close na tulipendana sana hadi akawa anahamia kwangu kama week then anarud kwao.

janga lililonikuta , siku napita town naelekea makao mapya maeneo ya kenny garden nikamuona mpenz wangu! Yuko na jamaa mdogo tu! Niliumia roho sana.

nikampigia simu hakupokea! Ikabid nim txt kumuuliza alipo! Akaniambia yuko nyumban kwao! Bas na me nikamjibu anifuate kenny garden kula bata! Akazima simu sikumpata tena.

ikabid niende karibu na meza yao! Na me nikaagiza kinywaji! Mfukon nlikuwa na buku 5 tu.nikanywa bia ya kwanza,kufika ya pili nikapata ujasir nikamuita mpenz wangu, akanifuata nikamuuliza mbna ananisaliti? Akaniomba msamaha!

Bas nikamwambia akalete kinywaji chake tujumuike meza moja! Kwel akaleta bia yake na parcel ya take away chips kuku!

yule mwizi wangu kuona nimemchukua mpenz wangu akasepa! Akaniacha na mpenz wangu.

Balaa ni kwamba yule jamaa alitenganisha bili! Akalipa bia zake tu! Zile alizomnunulia mpenz wangu na chips hakuzilipia! So nlivyoletewa ile bili nilihisi kuzima! Bili ya elfu 20 na ushee na mie mfukoni niko na buku 5! Aibu iliyoje? Bas nikamuomba mhudum niache simu ya mpenz wangu kama bond then kesho nirud kulipa! Bas tukaacha simu na tukarud home wapolee.

usiku ulikuwa mrefu sana, ile kumekucha ikabid nimfate mzee wangu na kumwambia sitaki tena kazi ile! Nataka niende chuoni na grade yangu ya 4m 6 haikuwa mbaya! Mzee akakubali, nikaanza chuo na nimemaliza miaka 2 iliyopita na nimepata kaz nzur.

Yule mpenz bado anataka niwe nae nahisi ni gold digger ila sometym namwona kama mkomboz wangu! Manake bila yeye nisingepata challenge ya kwenda kusoma!

Maisha ni safari ndefu wanandugu.. HII ISHU ILINISISIMUA SANA NLIPOMUULIZA MSHKAJI AMEWEZAJE KUWA NA HAPPY RELATION KWENYE NDOA YAKE NDO AKANIPA HUU MKASA! KWA KWELI NILIMPONGEZA KWA USHUJAA NA UPENDO WA KWEL.
 
hahahaahaa nimecheka ati bia ya pili ukapata ujasiri wa kumuita kumbe wenzako kwenye fumaniz si mpaka upate ujasiri wa pombe. mkasa huu ni mzuri na unafundisha sana. wakat mwingine inapobid yafaa usamehe tu kila kitu kinatokea kwa sababu fulani pengine bila kufumania usingeenda kusoma.
 
Habar ya j3 wana jamvi! Polen kwa uchovu wa wkend!
Maisha ni safari ndefu wanandugu.. HII ISHU ILINISISIMUA SANA NLIPOMUULIZA MSHKAJI AMEWEZAJE KUWA NA HAPPY RELATION KWENYE NDOA YAKE NDO AKANIPA HUU MKASA! KWA KWELI NILIMPONGEZA KWA USHUJAA NA UPENDO WA KWEL.

Du hii kali lakini mwisho umetuchanganya hasa kwani jamaa yako ana RELATION KWENYE NDOA ni ipi hiyo na hicho kichangu cha Sanawari au alipata kingine akaoa maana kalimkomboa na pombe kuzijua hadi kakakubali kuweka simu yake Bond ila sometym namwona kama mkomboz wangu! Manake bila yeye nisingepata challenge ya kwenda kusoma!
Ingekuwa hadithi za kina CHAI CHUNGU ni nzuri zana kwa Elimu ya maisha
 
Yule mpenz bado anataka niwe nae nahisi ni gold digger ila sometym namwona kama mkomboz wangu! Manake bila yeye nisingepata challenge ya kwenda kusoma!
Sometimes, mafanikio huja kwa njia ya maumivu makubwa. Nakumbuka niliwahi kuajiriwa ofisi moja kubwa ya bima huko wanakotumia namba za SU nikapata boss fulani mkorofi na ana ubaguzi hakuna mfano. Huwa sipenda dharau, hivyo nikaacha kazi kwa hasira, nikarudi mtaani. Huko mtaani hali haikuwa shwari, nikachapwa sana na maisha. Ilikuwa hatari, trip za mwenge mpaka magomeni kwa miguu ilikuwa kawaida tu kama kwenda dukani kununua vocha. Nilikuwa mtu wa juhudi na kujituma kufanya kazi za nguvu, lakini kadiri nilivyokuwa najituma kazi ndivyo life iliendelea kubana. Niliomba kazi ofisi mbali mbali bila mafanikio. Interview nilikuwa napiga mpaka tatu kwa siku, lakini holaaa!

Nilibanwa na maisha nikawa napumulia mashine. Hali ilivyokuwa inaelekea pabaya nikaamua kufanya maamuzi ya kurudi mkoani kuendelea na shughuli za kilimo. Nakumbuka nilitafuta nauli kwa takriban wiki tatu bila mafanikio. Ilikuwa situation mbaya.

Ktk hali hiyo ndiyo nikashangaa kupigiwa simu na kampuni fulani ambayo nilifanya interview wakati nilipokuwa naendelea kuadhibiwa na maisha. Nikapata kazi ya maana sana ambayo mshahara wake wala sikuamini kama ni wangu. Nilibadilika ndani ya miezi michache sana.

Kwa hiyo kaka hayo ni mapito tu, na huyo alikuja kukufikisha hapo ulipo. Kama asingekuwa yeye pengine angekuja mwingine. Zingatia kama tabia zake ni mbaya au ni za kihuni, hakuna sababu yeyote ya kutumia mapito yako na yake kuhalalisha maisha yako kuwa ya dhiki, kudharauliwa kutokana na tabia mbaya za huyo mdada na kuletewa magonjwa nyumbani. lakini kama alijirekebisha, basi niwatakie kila la kheri!
 
vituko huwa haviishi humu ndio maana napenda sana jf
 
mi siwezi nikisalitiwa tu mara moja tunaachana
 
Du hii kali lakini mwisho umetuchanganya hasa kwani jamaa yako ana RELATION KWENYE NDOA ni ipi hiyo na hicho kichangu cha Sanawari au alipata kingine akaoa maana kalimkomboa na pombe kuzijua hadi kakakubali kuweka simu yake Bond ila sometym namwona kama mkomboz wangu! Manake bila yeye nisingepata challenge ya kwenda kusoma!
Ingekuwa hadithi za kina CHAI CHUNGU ni nzuri zana kwa Elimu ya maisha

jamaa ndo kamuoa huyo binti. Na niliona wako happy kwenye ndoa yao! So ikabid nimuulize siri ya upendo wao ni nin manake watu wengi wanaogopa ndoa! Ndio akanipa huo mkasa ulivyompata!

so anajua mwanzon mke wake alimsaliti manake hakuwa na cash nzur! So alvyo graduate na kuajiriwa mapenz yakaanza upya! Ndo mana anamfikiria mke wake kama gold digger but hataki kuamin hvyo sana anamchukulia kama challange iliyobadilisha maisha yake jumla.!
 
hahahaahaa nimecheka ati bia ya pili ukapata ujasiri wa kumuita kumbe wenzako kwenye fumaniz si mpaka upate ujasiri wa pombe. mkasa huu ni mzuri na unafundisha sana. wakat mwingine inapobid yafaa usamehe tu kila kitu kinatokea kwa sababu fulani pengine bila kufumania usingeenda kusoma.

Ni kwel mkuu! Aibu ya kuachiwa bili si mchezo! Ilikuwa ni hasira tosha ya kwenda kusoma!

yan kila jambo linatokea kwa maana yake! Either positive or negative!
 
ahahaaa...story zingine raha sana

Yan unaweza kuchukulia story, bt hii ni moja wapo ya safar katika maisha! Ni jambo lakuchekesha sana mtu unapokumbuka stor za zaman uki compare na status au situation uliyonayo saiv.

Mungu ni mwema.
 
mi siwezi nikisalitiwa tu mara moja tunaachana

Inategemea mkuu, ujue kuna kupenda kwel na kuna kutamani. So inapotokea kufumanij inatdgemea na upendo ulionao kwa huyo mpenz wako.

Na mpaka umfumania mpenz wako manake iko sababu ya yeye kutoka nje so una fix hyo loop hole na kuendelea na maisha upya.
 
"Love is not maximum emotion. Love is maximum commitment."
― Sinclair B. Ferguson
 
Mzee umenikumbusha mbali...Mimi mtu alifanya mapaka nikastrugle kununua gari...
 
Inategemea mkuu, ujue kuna kupenda kwel na kuna kutamani. So inapotokea kufumanij inatdgemea na upendo ulionao kwa huyo mpenz wako.

Na mpaka umfumania mpenz wako manake iko sababu ya yeye kutoka nje so una fix hyo loop hole na kuendelea na maisha upya.
naweza kumpenda ila sasa kumwamini ndo ishu
 
Mzee umenikumbusha mbali...Mimi mtu alifanya mapaka nikastrugle kununua gari...

Ni hatari sana, ila unaweza ukaona uzur wake kwa sasa! May be mwanzon ulikasirika kuona anapiga kishoka kwenye gar ya mtu mwingine

ila hasira yako ikawa challenge ya wewe kununua gar! Ni positive move japo mwanzon ilikuumiza kichwa.
 
Back
Top Bottom