Nilipokutana na katibu mkuu wa CHADEMA Dk Wilbrod Slaa baada ya kushindwa vibaya na CCM kwenye uchaguzi ulioisha siku za karibuni nilizungumza nae mambo makuu mawili (wanajamvi mtaongezea mengine) ambayo pengine yamechangia ya huenda yakapelekea kutoa matokeo yaleyale kama hayatafanyiwa kazi.
i)Nilimkumbusha aangalie tofauti kubwa inayojitokeza baina ya wananchi wanaojitokeza kupiga kura na wale waliojiandikisha tofauti ni kubwa sana. Ni wastani wa 30%-40% ndio wanaojitokeza kupiga kura .Hata kwenye hizi chaguzi ndogo zilizopita hali ni hiyo hiyo. Nikamkumbusha hata 2010 Rais wa nchi alichaguliwa na watu wasiozidi mil 5 kati ya takribani watu mil 20 waliojiandikisha. Sasa ukitoa wale waliopoteza au KUUZA shahada zao kwa hiari baada ya kurubuniwa na wanasiasa(hasa CCM),pia ukiondoa wale wanaoshindwa kufika kwenye vituo vya kupiga kura kwa hofu ya vurugu zinazozuka muda mfupi kabla ya uchaguzi,sababu inayotolewa na wengi ambao hawajitokezi kupiga kura ni kutokuwa na imani na wagombea husika.
Hivyo inawezekana kabisa CCM ikawa inashinda hizi chaguzi kwa sababu tu watu wengi hawajitokezi kupiga kura na si kuwa wanakubalika kama wanavosema wenyewe. Nilimshauri waongeze bidii kwenye mpango mkakati yao,ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya kutosha na ya dhati ili wananchi wajitokeze kupiga kura kwenye chaguzi zijazo.Yanaweza yakapatikana matokeo tofauti na ilivyo sasa. Pia nilimtahadharisha kuwa wasitegemee CCM kulifanya hilo la kutoa elimu. Katibu mkuu wa CCM Mh A.Kinana aliwahi kutoa kauli kwamba anaridhika na mahudhurio katika chaguzi.Kwa CCM hata akitokea mpiga kura mmoja kati ya mia,ilimradi hiyo kura moja ni ya kwao hawana tatizo kabisa. Wanachotaka ni ushindi tu.
ii)Pia nilikubaliana nae kwamba kutoboreshwa daftari la wapiga kura kunachangia CCM kupata ushindi mkubwa ikiwa ni pamoja na chaguzi zilizoisha punde. Nimemtahadharisha kama wataenda kushiriki kwenye chaguzi za CHALINZE na KALINGA bila ya daftari la wapiga kura kuboreshwa watarajie KIPIGO KITAKATIFU kutoka CCM na pia nikamchekesha baada ya kumwambia aandae kabisa sababu za kuwadanganya wana CHADEMA kutokana na kushindwa kwao kwenye hizo chaguzi.
Inafahamika mara ya mwisho daftari la wapiga kura liliboreshwa mwaka 2009 kuelekea uchaguzi 2010. Ni zaidi ya miaka MITANO sasa.Kuna idadi kubwa ya vijana kati ya miaka 18-28 hawamo kwenye daftari la wapiga kura ,achilia mbali waliopoteza shahada zao(inakadiriwa zaidi ya watu mil 5 hawamo).Ni idadi hii ya watu mil 5 ndio ilimuweka Rais madarakani.
Na nikamkumbusha ni hao hao vijana wengi walio kwenye hiyo rika nililotaja hapo juu ndio mtaji mkubwa wa CHADEMA na ndio hao hao CCM kwa makusudi wanawanyima haki yao ya msingi ya kupiga kura. Fahamuni suala la kucheleweshwa kuboresha daftari la wapiga kura halifanywi kwa bahati mbaya.Na hakika msipoangalia mtaendelea kujaza maelfu ya wananchi katika mikutano yenu ambao ndio hao hao walio kwenye hilo rika nililotaja hapo juu ambao hawamo kwenye daftari la wapiga kura. Ni juzi tu katibu mkuu wa CCM Ndugu A.Kinana alitoa kauli kwamba anaridhika na idadi ya wanaojitokeza kupiga kura na haoni sababu ya kuboreshwa daftari la wapiga kura.
i)Nilimkumbusha aangalie tofauti kubwa inayojitokeza baina ya wananchi wanaojitokeza kupiga kura na wale waliojiandikisha tofauti ni kubwa sana. Ni wastani wa 30%-40% ndio wanaojitokeza kupiga kura .Hata kwenye hizi chaguzi ndogo zilizopita hali ni hiyo hiyo. Nikamkumbusha hata 2010 Rais wa nchi alichaguliwa na watu wasiozidi mil 5 kati ya takribani watu mil 20 waliojiandikisha. Sasa ukitoa wale waliopoteza au KUUZA shahada zao kwa hiari baada ya kurubuniwa na wanasiasa(hasa CCM),pia ukiondoa wale wanaoshindwa kufika kwenye vituo vya kupiga kura kwa hofu ya vurugu zinazozuka muda mfupi kabla ya uchaguzi,sababu inayotolewa na wengi ambao hawajitokezi kupiga kura ni kutokuwa na imani na wagombea husika.
Hivyo inawezekana kabisa CCM ikawa inashinda hizi chaguzi kwa sababu tu watu wengi hawajitokezi kupiga kura na si kuwa wanakubalika kama wanavosema wenyewe. Nilimshauri waongeze bidii kwenye mpango mkakati yao,ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya kutosha na ya dhati ili wananchi wajitokeze kupiga kura kwenye chaguzi zijazo.Yanaweza yakapatikana matokeo tofauti na ilivyo sasa. Pia nilimtahadharisha kuwa wasitegemee CCM kulifanya hilo la kutoa elimu. Katibu mkuu wa CCM Mh A.Kinana aliwahi kutoa kauli kwamba anaridhika na mahudhurio katika chaguzi.Kwa CCM hata akitokea mpiga kura mmoja kati ya mia,ilimradi hiyo kura moja ni ya kwao hawana tatizo kabisa. Wanachotaka ni ushindi tu.
ii)Pia nilikubaliana nae kwamba kutoboreshwa daftari la wapiga kura kunachangia CCM kupata ushindi mkubwa ikiwa ni pamoja na chaguzi zilizoisha punde. Nimemtahadharisha kama wataenda kushiriki kwenye chaguzi za CHALINZE na KALINGA bila ya daftari la wapiga kura kuboreshwa watarajie KIPIGO KITAKATIFU kutoka CCM na pia nikamchekesha baada ya kumwambia aandae kabisa sababu za kuwadanganya wana CHADEMA kutokana na kushindwa kwao kwenye hizo chaguzi.
Inafahamika mara ya mwisho daftari la wapiga kura liliboreshwa mwaka 2009 kuelekea uchaguzi 2010. Ni zaidi ya miaka MITANO sasa.Kuna idadi kubwa ya vijana kati ya miaka 18-28 hawamo kwenye daftari la wapiga kura ,achilia mbali waliopoteza shahada zao(inakadiriwa zaidi ya watu mil 5 hawamo).Ni idadi hii ya watu mil 5 ndio ilimuweka Rais madarakani.
Na nikamkumbusha ni hao hao vijana wengi walio kwenye hiyo rika nililotaja hapo juu ndio mtaji mkubwa wa CHADEMA na ndio hao hao CCM kwa makusudi wanawanyima haki yao ya msingi ya kupiga kura. Fahamuni suala la kucheleweshwa kuboresha daftari la wapiga kura halifanywi kwa bahati mbaya.Na hakika msipoangalia mtaendelea kujaza maelfu ya wananchi katika mikutano yenu ambao ndio hao hao walio kwenye hilo rika nililotaja hapo juu ambao hawamo kwenye daftari la wapiga kura. Ni juzi tu katibu mkuu wa CCM Ndugu A.Kinana alitoa kauli kwamba anaridhika na idadi ya wanaojitokeza kupiga kura na haoni sababu ya kuboreshwa daftari la wapiga kura.
Ochutz,
Kwa bahati mbaya huna ujasiri wa kuandika jina lako la kweli, hivyo siwezi kujua Kama kweli ulinipa ushauri au umetunga tu. Ebu jiulize katika akili ya kawaida, Mimi na wewe ( au Chadema) nani angelimshauri mwenzake, wake moja Kati ya lengo la OPeration Pamoja Daima ni kuishinikiza Serikali kuboresha Daftari Hilo. Hayo yamesemwa na Mbowe, Lisu na Slaa! Kati yako wewe na Slaa ni nani Hana uelewa au nani ampe ushauri mwenzake. Ni vema tusifanye ushabiki katika mambo mazito.
Kama kweli ukielewa na una nia njema, badala ya kutuma ujumbe kwa Slaa, ungeandika kwenye Gazeti ili uishinikize Serikali kwa kuwa kazi ya kuboresha daftari ni ya Serikali na NEC yake. Aidha ungelikuwa na ujasiri wa kupostiwa kwa ID yako ningelijua Kama tuliongea la, kwa sasa hoja yako haina maana yeyote,