Nilichojifunza Jumapili Ya Leo Katika Misa Ya Pentekoste

Nilichojifunza Jumapili Ya Leo Katika Misa Ya Pentekoste

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
3,168
Reaction score
6,089
Dominika hii Kanisa linaadhimisha sherehe ya Pentekoste. Hili ni adhimisho la ujio wa Roho Mtakatifu kwa Kanisa zima siku 50 baada ya Yesu kufufuka.ujio unaoashiria mwanzo wa Kanisa kama jumuiya inayoongozwa na Roho Mtakatifu kukiri,kuishi na kuadhimisha fumbo la Kristo.

INJILI

Yn. 20 :19-23

Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu. Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana.


Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.


Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Mbali na tafakari zingine pia nimejaribu kujiuliza wale wanaohoji mamlaka ya mapadre na maaskofu kuondoa dhambi za waumini ina maana hawasomi wala kufuatilia maandiko? Yesu mwenye alisema

"Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa"

Kwa hiyo unapotubu,kujutia,kulipiza na hatimaye kushiriki Sakramenti ya Kitubio/Maungamo mbele ya Padre yeye amepewa mamlaka ya kukuondolea dhambi zako(kufungua) au kukataa kukuondolea dhambi zako (kufunga) kama jinsi Yesu alivyowaagiza.Hivyo kanisa linapomfungia huduma muumini ni wazi kwamba hata mbinguni amefungiwa na linapofungua hata mbinguni amefunguliwa.

Tumsifu Yesu Kristu
View attachment 2251162
 
Ondoleo la dhambi ndio kilichompeleka Yesu msalabani wala si upate fedha na maisha bora! Mapadre wamepewa mamlaka ya kuondoa dhambi, Yesu aliondoa dhambi wanadamu wakamshangaa!

Dhambi ndogo ndogo unaweza kutubu mwenyewe! Kila misa kuna ondoleo la dhambi lakini zipo dhambi unapaswa kuungama kwa Padri ili upate ondoleo. Hutaki sikukatazi ila ujue mapadre wanayo mamlaka hiyo kama ukitubu inavyopaswa.
 
Back
Top Bottom