kwa kusoma majibu ya huyu anayejiita salma juma nimegundua tabia hizi toka kwake kwa huu muda mfupi tu niliofuatilia hii thread yake.
1-mkali
2-jeuri
3-hapendi kukosolewa bali anapenda kusifiwa tu
4-anajifanya yeye mtakatifu hamkosei mumewe/si mkosaji hata kidogo
5-ni mtu wa kujikweza si wa kujishusha
6-anachoamini yeye analazimisha na wengine waamini hivyohivyo pasipo kuhoji .
7-ni mtawala
8-anapenda kupokea misaada si mtoaji wa misaada
9-mkaidi
hizo tabia za huyu dada hauwezi kuzigundua haraka ila mpaka usome thread yake na maoni ya wanajf pamoja na majibu yake kwa wanajf.
mwanamke wa aina hii kujenga nyumba yake ni ngumu sana.
huyo mwanamme kuishi na mwanamke wa aina hii miaka yote hii anastahili pongezi.
mwanamke wa aina hii hastahili kuolewa bali kuwa single parent tu.
nadhani tungepata bahati ya kusikiliza upande wa mumewe angesema zaidi ya haya niliyoyasema.
pole sana salma nawe labda ndivyo ulivyoumbwa, ila fahamu hakuna binadamu mtakatifu wote waja wa mungu tuna mapungufu yetu, ndiyo maana tuna mungu,makanisa na misikiti ili tukaombe msamaha huko na kuomba baraka,hekima,utu,na busara ktk maisha yetu. Hiyo ndoa yako haina matatizo makubwa sana ila wewe umelazimisha yawe makubwa na magumu kwa hizo tabia zako chache nilizoorodhesha hapo juu,
pole sana ila kwa mungu yote yanawezekana.