Nikikumbuka nacheka sana

Nikikumbuka nacheka sana

Gochavez

Senior Member
Joined
Apr 30, 2013
Posts
171
Reaction score
155
Nilipokuwa shule ya msingi kuanzia la 4 hadi la 7 maksi zangu za hesabu kwenye mitihani zilikuwa zinacheza kwenye 03%hadi 08%.Matokeo yalikuwa yanatangazwa mbele ya darasa! yanapotangazwa mwalimu anaanza kuwaita wanafunzi kwa kuanzia maksi za chini kwenda juu (0-100), kwa hiyo darasa lote linajua makaratasi yakiletwa lazima niitwe kama si wa kwanza basi wa pili.Siku moja mwalimu akaanza kuita majina,mpaka akafikia kwenye maksi 30%,40%,50%,60% ,70% bado tu mi hajaniita. Watu wakaanza kuniangalia waliokuwa karibu wakaanza kuniuliza...."" eeeh umepasua hujaitwa, ilikwaje??"Nili anza kuvimba kichwa, huku mwalimu anaendelea kugawa tu makaratasi. Yakabaki makaratasi ya waliopata 80%-90% bado mi sijaitwa tu. Mara akabaki na karatasi moja mkononi, darasa lote macho kwangu hawaamini kinachotokea maana bado sijapata karatasi. Mwishoni mwalimu akaangalia juu,kisha akasema"Kuna ng'ombe hajaandika jina kapata 0% aje achukue karatasi lake...
 
Good,kama kweli vle,mpaka leo bado kiazi?
 
Nimerudia kuisoma tena,ti ti ti ti teh teh teh haa ha
 
Unakausha huendi kuchukua karatasi hhhhhaaa
 
Hapo lazma ukatae kua ule co mtihan wako,,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom