Nikikasirika mvua inanyesha

Nikikasirika mvua inanyesha

Ziege

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2014
Posts
337
Reaction score
139
Kuna jambo la ajabu ambalo sijui ni Kwa nini inatokea hivi.
Kwamba ninapohitilafiana na mke wangu nikikasirika mara nyingi mvua inanyesha ni jambo ambalo limenitokea zaidi ya Mara tatu sijui nini maana yake wataalam msaada wenu Juu ya tukio hili.
 
Mvua kunyesha haina uhusiano wowote na wewe kukasirika...kwanza kumbe imetokea Mara tatu tu...acha kujishtukia bro...!
 
Kuna jambo la ajabu ambalo sijui ni Kwa nini inatokea hivi.
Kwamba ninapohitilafiana na mke wangu nikikasirika mara nyingi mvua inanyesha ni jambo ambalo limenitokea zaidi ya Mara tatu sijui nini maana yake wataalam msaada wenu Juu ya tukio hili.

Wewe utakuwa na Nyota ya Umasihi au Unabii.
 
Wewe ni hazina kwa taifa,kwa uwepo wako bwawa la mtera haliwezi kukauka so tumeshapata suluhisho la kudumu la umeme,kilimo pia kitapiga hatua hata kama si kwa kasi lakini angalau sasa tutakuwa na uhakika wa mvua.Kitu kilichobaki sasa ni kuongea na mke wako na kuona jinsi gani anaweza kukukasirisha angalau kwa masaa 14 kwa siku.
 
Wewe ni hazina kwa taifa,kwa uwepo wako bwawa la mtera haliwezi kukauka so tumeshapata suluhisho la kudumu la umeme,kilimo pia kitapiga hatua hata kama si kwa kasi lakini angalau sasa tutakuwa na uhakika wa mvua.Kitu kilichobaki sasa ni kuongea na mke wako na kuona jinsi gani anaweza kukukasirisha angalau kwa masaa 14 kwa siku.
Hahahaa ngachoka
 
Hamia mikoa yenye ukame kama Singida na Dodoma halafu uwe unagombana na mkeo kila siku, utalisaidia taifa katika kutekeleza sera yake ya kilimo kwanza ambayo imekuwa ni ndoto kutokana na ukosefu wa mvua.
 
Kama unaishi dar uhamie kabisa huko huko Dodoma maana sisi dar hatutaki mvua kawasaidie na dodoma
 
Nimeuliza nimeambiwa kuna jambo linakunyemelea karibu tanga nikuoneshe mtu akusaidie
 
Back
Top Bottom