Nifikie wapi kuitalii Zanzibar kwa wiki moja?

Nifikie wapi kuitalii Zanzibar kwa wiki moja?

Myomb_0

Member
Joined
Apr 17, 2013
Posts
72
Reaction score
51
Habari wakuu,

Natumaini ni wazima wote licha ya changamoto ya covid19.

Naomba ushauri kwa wale waliopo Zanzibar au waliowahi kupatembelea;

Ni hotel gani nzuri ambayo una huduma nzuri lkn pia ipo karibu na vivutuo vya utalii?

Pia, kwa honey moon mnashauri hoteli gani?

Pia, mnashauri nitembelee sehemu gani nikiwa Zanzibar?
 
Zanzibar kiujumla vivutio vyake vipo scattered ila distance kutoka kituo kimoja hadi kingine sio mbali sababu eneo la kisiwa sio kubwa. Kivutio kikubwa cha Zanzibar ni Stone Town ambapo ndio City Centre ya Zanzibar. Kwa ajili ya honeymoon hotel nzuri ni zile ambazo ziko nje ya Stone Town (Shamba) maana hotels za Stone Town karibia zote hazina private beach.

Ingia Google search hotels in Kiwengwa au hotels in Nungwi utaona hotels nyingi tu na rates zake hivyo kutokana na budget yako utachagua. Kutoka Stone Town mpaka Nungwi au Kiwengwa ni mwendo wa saa moja kwa gari. Ingawa pia kama unapenda kuzurura na kufanya manunuzi bora ubaki Stone Town, kuna migahawa mingi na maduka huwezi kua bored pia unaweza kutembelea Prison Island kutokea hapo. Kuna hotels kama Tembo, Serena zina Sea view na ni affordable na Park Hyatt kama una msuli kiasi. Au pia unaweza kwenda Hotel Verde ipo dk 15 kutoka Stone Town na ina private beach and it's affordable (hapa hakuna ulabu)

N:B: Hotels nyingi na migahawa kwa sasa zimefungwa kutokana na Corona.
 
[QUOTE="Myomb_0, pos

Naomba ushauri kwa wale waliopo Zanzibar au waliowahi kupatembelea.






Naungana nawe nami naomba msaada wa kujua kama kuna guest hause za bei ya kawaida kama 20,000 au 25,000. Maana naambiwa hakuna kitu kama hicho ila ni mahotel tu ya bei ngumu.
 
Back
Top Bottom