Mchukue mama uishi nae....afu sitisha huduma zote kwa hao watoto...kama wana uwezo wa kumtukana mama kiasi hicho basi wana uwezo wa kujipatia huduma zote muhimu.....na na huyo konikodi wa matusi ndo awahudumie wadogo zake.....mpaka akili itakapomkaa sawa na atakapojua umuhimu wako na huyo mama....
Sawa. Watoto je?
shukrani ya punda hiyo .... achana nao...au waite ongea nao waeleze ukweli mother atasepa hapo ubaki na hivo vidubwasha visivyokuwa na shukrani huku ukikosa baraka za mama kwa kuwa kasha tangulia ...
We kaka how old are those watoto? Kama wako above 18 pleeeeeeeeeeeeeze muwache mama yako aishi maisha ya amani jamani kha!!! Watafutie room (hapo umewasaidia sana) tena kama wako village ndo vizuri maana maisha sio complicated. Wataftie room mbili kama me na ke then provide their basic needs wakiwa huko huko na wasimsumbue mama au ISHI NA MAMA YAKO WEWE MWENYEWE na huko kijijini tafuta mtu umpangishe ailinde nyumba then hao wadogo waishi humo na huyo mpangaji kama watamletea mizaha. Tena tafuta mpangaji mkorofi (mkurya atafaa zaidi).
Pole kwa kuachiwa mizigo isiyo na lazima mweee! Baba zetu wanatutaftiaga majangaa!!!Yametukuta pia haya
Mkuu nakushukuru. Japo naishi mbali huwa najitahidi sana kwenda nyumbani kusalimia. Kila nikienda huwa tunafanya vikao vya familia kupitia mambo yote hayo. Wazee mashuhuri marafiki zetu ninawaita ili watoe ushauri kwa hao watoto lakini ikipita wiki tu mambo yanaanza. Kwa ujumla nimejitahidi sana lakini sioni mafanikio. Unaweza kufanya ,azungumzo nao, mfano siku moja.....baada ya kuongea nao, wiki moja baadaye nilikuta barua ameandika mtoto mmoja akisema....nanukuu"wadogo zangu hapa tunapoishi ni kama ndege tu. Huyu kaka yetu anatusaidia lakini hatupendi. Tujihadhari naye" Kwakweli nilitaka kuchanganyikiwa kwa kusoma ujumbe ule!
Ahsante dadangu.pole sana kwa tatizo ....
mchukue mama yko anahtaji kuwa na amani na furuha kwa sasa ameteseka vya kutosha juu yenu pindi baba yenu amuache...dada zako wana kazi i hope soo wamchukue wakae nae au wewe
maaumuzi yahitajika tna ya busara ongea na ndugu zako kama wapo aunt/baba wadogo muone hao watoto wataishije huko kijijini ..
Sasa ndugu yangu mpaka hapo bado unasubiri nini kuachana nao japo kwa muda tu ili wajifunze then ndo urudishe msaada? mana mwisho wa siku wanaweza hata kumfanyia kitu kibaya huyo mama yako, hamumuhurumii bibi wa watu jamani? hapana bwana, me mama yangu anavyoniuma siwez kuthubutu kusikia kitu cha namna hiyo tena zaidi ya mara mbili alafu nikaendelea na maisha yangu as if nothing is happening, hao wanahitaji fundisho, kama kuambiwa ww mwenyewe umeshakiri wameshaambiwa sana sasa hivi kilichobaki ni vitendo ili waelewe, wanahitaji kufunzwa na ulimwengu hao, hiyo huruma yako itakuja kukuletea balaa na wao washakusoma ndo mana wanakudharau
ama kweli zigo la misumari halibebeki kwa kichwa..
mtu wa diploma sio under 18 tena, huyo ni matured kabisa na akili zake.
jambo la kuanza kumtusi mzazi wangu lilikuwa si la kujadili... aisee ningewafanyia bombing tu wasepe kwa amani!
an old woman of 70 cant stand a harsh talk with 21 years old bratty kids...!
wachape lapa... ni wakati wa ulimwengu sasa kufunza..
Mtoto mkubwa anasoma Diploma in Accountancy (namsomesha kwa kinguvunguvu maana ndugu zangu wote hawapendi). Huyu yupo chuoni. Wa pili amemaliza VETA (naye nililipa karo mpaka dadazangu wengine wamentenga), huyu ndio tatizo. He is 19 now. Wengine wawili wapo Sekondari Form 3 kitindamimba yupo Std 6. Huyo wa VETA ana walioko Sekondari wamekuwa mwiba sana kwa mama yangu. Lakini niwafanyeje??
Ndo mana nikakuuliza how old are they? Nadhani option ya kuishi na mama iko poa. Waishi wenhewe kwenye nyumba ulomjengea mama then kadiri ya uwezo wako uwasaidie ukishindwa si basi bwana? Kwa nini uumize kichwa?Ahsante kwa ushauri wako mzuri. Huoni kuwa nitaongeza gharama ya kutunza familia, sasa zitakuwa tatu: ya kwangu, mama na hao watoto?
Mtoto mkubwa anasoma Diploma in Accountancy (namsomesha kwa kinguvunguvu maana ndugu zangu wote hawapendi). Huyu yupo chuoni. Wa pili amemaliza VETA (naye nililipa karo mpaka dadazangu wengine wamentenga), huyu ndio tatizo. He is 19 now. Wengine wawili wapo Sekondari Form 3 kitindamimba yupo Std 6. Huyo wa VETA ana walioko Sekondari wamekuwa mwiba sana kwa mama yangu. Lakini niwafanyeje??
Mkuu nakushukuru. Japo naishi mbali huwa najitahidi sana kwenda nyumbani kusalimia. Kila nikienda huwa tunafanya vikao vya familia kupitia mambo yote hayo. Wazee mashuhuri marafiki zetu ninawaita ili watoe ushauri kwa hao watoto lakini ikipita wiki tu mambo yanaanza. Kwa ujumla nimejitahidi sana lakini sioni mafanikio. Unaweza kufanya ,azungumzo nao, mfano siku moja.....baada ya kuongea nao, wiki moja baadaye nilikuta barua ameandika mtoto mmoja akisema....nanukuu"wadogo zangu hapa tunapoishi ni kama ndege tu. Huyu kaka yetu anatusaidia lakini hatupendi. Tujihadhari naye" Kwakweli nilitaka kuchanganyikiwa kwa kusoma ujumbe ule!