Alikuwa ni mpenzi ambaye tulidumu kwa muda wa mwaka mmoja na nusu. Niligundua kanificha mambo mengi muda wote niliokuwa naye. Aliwahi zaa mtoto akafariki, ila mimi alinidanganya kuwa ana mtoto na anaishi na dada yake. Pia nilikuja kugundua baadae kuwa anatembea na mume wa mtu, hii ndio ilikuwa sababu kubwa ya kumuacha. Tatizo nililo nalo hivi sasa ikiwa ni miezi sita tangu tuachane, hanitoki kabisa mawazoni. Naombeni ushauri ni namna gani nitaweza kumtoa mawazoni ili niendelee na maisha yangu?