Njoo pmMwanzo sikuamini kabisa katika mambo haya. Lakini si unajua ukiwa na shida unatafuta sehemu yoyote ya kuponea. Lakini huyu sio wale wa tunguli na wapiga ramli. Ni ustadh anatumia quran lakini alichosema ni kwamba napaswa nisomewe na nisafishwe mwili na niweke ubani kwa mkono wangu. Nasubiri unishauri zaidi hapo mkuu
Tayari nimekupm kakaNjoo pm
Poa tutaonana hukoTayari nimekupm kaka
nilikuwa nasubiria jibu kwa hamu hivyo jamani Mshana jrNaomba hili Nisikujibu hapa linagusa imani za wengine, na Sitaki kuwapa nafasi wachafuzi wa Post
Vema asiende huko kwa nia njema kabisanilikuwa nasubiria jibu kwa hamu hivyo jamani Mshana jr
Asante PendaneniMmmmh! Mpaka karne hii watu bado mnaamini ushirikina? Haya huyo bado ni mchumba tu anakushauri muende kwa mganga kwa tatizo mlilonalo, kwa nini msimuamini Mungu? Yaani kama mchumba wako ni mtu wa kwenda kwa waganga, kaa mkao wa kufanyiwa ndumba hadi utasahau watu wa kwenu!!! Mtu ambaye anaamini kwenda kwa waganga ni wa kukaa nae mbali, ni wa kuogopa kuliko EBOLA😵
Wamasai na ninyi MNA Imani za kishirikina? Kushiriki ni Imani, kukushauri kwenda au kutokwenda MTU kama Mimi siwezi kukushauri sababu umeishasema awali una matatizo yako binafsi bila kujua hayo matatizo kila akushaurie akudangana. Kuna matatizo mengine ni psychological unaweza tu kupata counselling na ukapona! Nitafute ntakupa solution.Ni hivi: Nimekuwa na matatizo binafsi yanayonisumbua. Sasa mchumba wangu kanishawishi anipeleke kwa mganga (ustaadh) kwamba ana uhakika pale ndo utakuwa mwisho wa matatizo yangu. Huyo mganga wanafahamiana sababu alishawahi kumtibu.
Sasa najiuliza, niende huko kweli?? Au ndo naenda kutengenezwa nipende milele na kukalishwa sijui wanaita.
NB: Nilishaenda nikatanguliza kiasi flani cha pesa lakini hakuna kazi iliyofanyika kutokana na ubize uliokuwepo, hivyo alituahidi turudi siku mbili baadae. Na nilipofika nyumbani ndo nikaijiwa na hili swali la niende au nisiende? Na je nisipoenda nimkwepe vipi huyu mchumba wangu ili asijue kama nimekwepa na tuendelee vizuri.
Niko njia panda wadau.