Kumbe kuna hitaji la wavulana kupewa elimu ya kutongoza ili iwasaidie kuwa wanaume.... Bunge lijalo nitapeleka hoja binafsi kwa Spika au sabuufa.... NB KURA ZIKITOSHA MWEZI WA 10.
Lol. sasa kama mtu wa dini na wewe una nia safi kweli yakuoa jipange nenda kwa peleka posa salam atazikuta kwao,
haya mambo ya kukutana barabarani sio mchezo mwema...
Mpaka unataka kuoa bado domozege wala hayuko serious ni woga wako tu huo na madomozege wako hivyo sasa mpaka namba ya simu umepewa unashindwa hata kutuma msg au na mkono nao mkonozege
hao wakaka wa jf wanao kuomba no yake kuwa makini nao. Cha kukusaidia mm iyo kazi naiweza kumpa mistari mdada mwenzangu si shida. Kama utakubali kunilipa niunganishe nae nimpikeee aive wew utakuja kula kilicho iva mm shida yangu faranga. Hapo vip?
Oooh! Sorry,tafakari sana uone la kufanya,Jf kwa style hii ni vigumu kupata uamuzi sahihi,hebu jiamini kidume ondoa soni,mwendee bint muelezee kuhusu hisia zako kwake,mbona simple kiasi sana na hivi una namba yake.
Jenga kujiamani. Mpaka umepewa namba ya simu ujue una chance nzuri tu na kizuri unaonekana una nia nzuri. Mweeleze jinsi unavyopenda anavyoipenda imani yake. Mwleze unapenda ukimwa wake/ utulivu wake na kuwa ungependa kuongea nae zaidi. Kwa kuwa lengo lako ni zuri na Mungu atakusimamia.
Mazoea hujengwa kwa kuwa karibu na mtu,omba siku moja kwenda nae out na ikishindikana basi we nenda hata huko kwenye dini yake na anza kuzoea mazingira anayopenda yeye na utaona ni rahisi sana kumpata,jambo lolote ukilijua mazingira yake huwa si gumu kulikamilisha kama una mipango nalo.