Sasa wanataka kukopeshwa hela au kupewa na nani??? Yaani movie waandae wenyewe halafu bajeti tulalamikiwe sisiWenyewe wanalalamika bajeti ila makosa wanayofanya hata hayahusiani na bajeti.
Sijawahi kumkubali wema.. Sauti yake ni maigizo tosha
Yaani hua nikiona jina lako kwenye post yoyote, hua naanza kucheka hata kabla ya kuisoma. Najua tu kuna mtu anachinjwa= anasubiria
Wanalala na heleni wakiamka asbh kama wametoka saloon
Nani hapa tanzania hajui kiswahili na anaangalia bongo movie. Au unawazungumzia watu wa call me j? Kiswahili hajui, itakua kiingerezaOK. Subtitles zinawekwa kwa ajili ya watu wasiojua kiswahili. Ni kama vile akina Rufufu wanavyokutafsiria filamu za kihindi na kikorea kwa KISWAHILI.
Ukiona wamevaa uhusika, mfano tomboy, ni tabia zaoIla movie ya Chausiku walijitahidi jamani, story ilikua tamu na waigizaji walivaa uhusika wa maana,
pia movie ya Kigodoro ilikua poa sana story ilieleweka sema mwishoni kuna sehemu waliharibu ila si mbaya,
Movie ya Mdundiko(ilipata tuzo kubwa tu ya kimataifa ajabu haikutangazwa kiviile sijui kwa kua hakua Ray wala JB) pia ana nyingine yaitwa Kisate.
Movie zingine zenye story nzuri ni za huyu Nice a.k.a Mr. Mtunis, kwa kweli jamaa anajitahidi sana hata makosa ni madogo madogo, movies zake ni kama BARMAID, MREMBO KIKOJOZI, MY DREAM (Riyama alifunika sana humu), TOMBOY(Wolper nae alitisha sana alijua kuvaa uhusika).
Ndiyo mnatakiwa muwekeze ili watengeneze movie nzuri kama za mbele.Sasa wanataka kukopeshwa hela au kupewa na nani??? Yaani movie waandae wenyewe halafu bajeti tulalamikiwe sisi
Mfano hii tamthilia ya siri za familia naona kigezo kikubwa kwa wanawake kuchaguliwa itakuwa ile mizigo yao maana karibu kila utakayemuona kafungasha.Tatzo hawaangalii vipaji bali wanatazama mwonekano wa mtu
Bibie anafungua geti kwa fujo,
Anaenda dukani kwa mangi kununua sumu kwa ajili ya kujiua
Cha ajabu anasubilia chenchi!
mke ana mwekea mumewe sumu kwenye juice alafu anaonja kama sumu imekolea ila yeye hafi mumewe ndo anakufa
Haha..halafu wana ile ya mtu kuongea mwenyewe ambapo kiuhalisia hakuna anayeongea pekee yake kwa sauti kubwa.Mwigizajo yupo mwenyewe ndani. Kapatwa na kiu anasema ngoja ninywe maji kwanza
are you out of your mind? hili neno wamekremishwaUwakute wanaongea na kiingereza ndio hatari.
Hahahaha au lile are you mad or something?????are you out of your mind? hili neno wamekremishwa