NI Zanzibar au Tanganyika inayoonewa????

fikirikwanza

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
7,452
3,065
Kwa nini fedha za Tanganyika zilichukuliwa kununua kitendea kazi cha muungano?? Mtanganyika kama angekuwa mtu wa makeke angedai serikali itoe maelezo kuhusu hilo. Lakini kwa upande mmoja unapata uthibitisho wa Tanganyika inavyojitolea kulea Zanzibar.

Kama kwamba haitoshi baada ya kutoa fedha za rada na rushwa pia, rushwa inarejeshwa nchi na kupewa jina zuri la kawaida kabisa eti chenji ya rada, wala sio rushwa ya rada tena. Mzanzibar ambaye alipewa ofa ya kuimalishiwa ulinzi wa nchi bila kutoa hata senti moja, anataka nae pia apewa hiyo rushwa ya rada, vile tu ni chenji iliyorudi baada ya suala la wizi ktk ununuzi wa rada hiyo kushindwa.

Mzanzibar, hoja yake inamashiko kama kwamba tu, pesa hiyo ilitolewa na kuwekwa kwa ridhaa ya Tanganyika kwenye kikapu cha muungano harafu baadae ikatumika kununua rada. Hapa mtanganyika ndo alitakiwa ahoji nani aliruhusu tanganyika kugawa fedha kama njugu???

Nani anaonewa hapa?? Mtanganyika au Mzanzibar???? Nani anafanya makosa haya, Je Tuchukue hatua gani??

Nawasilisha
 
Kama hii nayo ni hoja ya kujadili basi mtacheza kila ngoma mwaka huu.
 
Watanganyika nao wawepo kwenye serikali ya Zanzibar ambayo ni kubwa kuliko ile ya Muungano tunayogawana nao, huko ya wao wakiwa 100%
 
Eti mtu anauliza tena bungeni eti kwanini hakuna mzanzibar CDF, AG, Speaker, CJ etc kwenye serikali ya muungano. Hataki kujiuliza kuna wanajeshi wangapi jeshini wakizanzibar, hataki kujua ktk muungano kuna uchumi mkubwa na mdogo, hataki kujua kuwa 42mil over 1m ya populations, Hataki kujua kuwa 1978-9 Majenerali wangapi wa TGK na sio ZNZ waliongoza mapigano dhidi ya UGANDA, hataki kujua kwanini Tgk ilitoa pesa ya rada bila kutaka znz ichangie. Hataki kujua kuwa serikali ya JMT ni Serikali ya TGK sio ya ZNZ. If you are small play small not big in all aspects of life.
 
Mtoa hoja inaönekana mzito wa kuelewa, fedha za rada zimetolewa na JMT mimi sielewe kama kuna serikali ya Tanganyika. Sijui ikoje hiyo?
 
Mtoa hoja inaönekana mzito wa kuelewa, fedha za rada zimetolewa na JMT mimi sielewe kama kuna serikali ya Tanganyika. Sijui ikoje hiyo?

Je unafahamu kuwa AG aliliambia bunge kweli fedha hazikutolewa kwenye chombo cha muungano?? au hutaki kusikia neno tanganyika ndo linakupa shida? basi tanzania bara mkuu.
 
Zanzibar haichangii muungano, ile hali hata wizara ya afya ambayo sio ya muungano kuna mzanzibari, je ni hisani ya Watanganyika au uonevu kwa Zanzibar, kuwapa majukumu yasiyo yao???
 
Umeambiwa Zanzibar haijachangia chochote kwenye muungano tangu muungano upatikane!Hii ina maana tunasomesha watoto wa viongozi wa wazanzibar,tunalipa posho ya viongozi hao wa zanzibar,mafuta ya magari na kila aina ya advantage ya viongozi hao kwa pesa za WATANGANYIKA!

Hii ni zaidi ya kuonewa!!:angry::angry:
 
Umeambiwa Zanzibar haijachangia chochote kwenye muungano tangu muungano upatikane!Hii ina maana tunasomesha watoto wa viongozi wa wazanzibar,tunalipa posho ya viongozi hao wa zanzibar,mafuta ya magari na kila aina ya advantage ya viongozi hao kwa pesa za WATANGANYIKA!

Hii ni zaidi ya kuonewa!!:angry::angry:

Zanzibar ichangie muungano jee Zanzibar inafaidika na nini kutoka na hiyo serikali ya muungano!??

Jee Zanzibar ikichangia jee ichangie na nani ikiwa mshirika mwenzake ni hewa!?

Na ingekuwa bora Kama Zanzibar angaliambiwa mapato na matumizi ya muungano ni kiasi gani!

Pia ungelitoa faida inayotokana na mradi ambao Zanzibar alitoa mtaji kuuazisha Wa benki kuu jee Zanzibar ni lini amepewa Faida ya hii biashara?

Ikiwa watoto na viongozi wenu mnashindwa kuwasomesha bure jee mtaweza kuwasomesha Wa Jirani!???

Kama ni kuonewa mnajionea wenyewe mnaowapa wazungu madini yenu bure na nyinyi mkabakishiwa mashimo matupu!??

Au mnaona bora kuwanufaisha wazungu wanaobadilisha majina ya makampuni na mahoteli kila baadae ya miaka mitano kukwepa kodi!!??? Kumbuka moja ilianza na SHERATON, IKAJA ROYAL PALM, IKAJA MOVEN PICK NA SASA SERENA.
 
Zanzibar haichangii muungano, ile hali hata wizara ya afya ambayo sio ya muungano kuna mzanzibari, je ni hisani ya Watanganyika au uonevu kwa Zanzibar, kuwapa majukumu yasiyo yao???

Kama Zanzibar haichangii muungano labda ungalitueleza ninani anaechangia muungano!
 
Wewe huna akili hata kidogo ulikuwa uitwe kafirwekwanza sio fiikiri kwanza jua kua hakuna chanzo chochote cha mapato ya Tanganyika kitachopatikana na kutumika Zanzibar ila kuna cha Zanzibar ambacho kinaweza kisitumuke Zanzibar badala yake kikatumika Tanganyika mfano : misaada kutoka nje
 
Kama Zanzibar haichangii muungano labda ungalitueleza ninani anaechangia muungano!

Kwani wewe akili zako ni kwa ajili ya nini??? Kama Zanz hawachangii maana yake si Tanganyika pekee ndo wanaendesha muungano au hilo nalo unahitaji mwalimu, darasa, na vipindi vya dk 40 40 viwili???
 
Back
Top Bottom