Ni zamu ya nabii na mtume Mwamposa, wengine tupa kuleeee

Kama anadhani ni rahisi hivyo kupata wafuasi na kupiga pesa uwanja uko wazi kafungue kanisa kama hujafunga ndani ya mwezi.Sababu mtu kama Mimi nikaja nisipopata miujiza ninaotaka kama ulitangaza kunivutia wakati huna uwezo wa kufanya miujiza nisipopata hunioni na nitakutangaza vibaya kuwa tapeli.Watanzania wabishi hadi uone mtu wamemkubali na wanajaa nyomi ujue ana kitu.Kama unadhani ni kitu rahisi jaribu.

Ni biashara kubwa sana kwenye bara hili maana wengi wetu kufikiria hakupo tena. Tunaweka auto pilot. Tunaenda kwa kupenda hiyo tunayoiita miujiza
Kweli wajinga ndio wanaoliwa
 
Miujiza ilikua zamani wakati binadamu hawajapiga hatua za kimaendeleo kwenye sekta ya afya. Magonjwa yote ambayo mungu alikua akiwalaani wanadam enzi hizo siku hizi yana dawa na mengine yame tokomezwa kabisa.
 
Miujiza ilikua zamani wakati binadamu hawajapiga hatua za kimaendeleo kwenye sekta ya afya. Magonjwa yote ambayo mungu alikua akiwalaani wanadam enzi hizo siku hizi yana dawa na mengine yame tokomezwa kabisa.
Acha hizo dengue tu Hapa tiba haipo haijapatikana shida ohh hakuna Cha hatua ya maendeleo Wala Nini.Dengue tu inapelekesha Kama nini
 
Sijui kakobe aka tortoise ,hakuna cha mama rwakatale sijui gwaji boy au huyu Mzee Wa upako na ulabu ni muda wa mwamposa mji mzima umehamia huko.

Jamaa anamafuta sijui yanatoka wapi.anamagazeti sijui ndio mambo gani achilia mbali maji ya upako.

Wahitimu walikosa ajira,walikosa watoto,wanaotaka vyeo,wanataka kupandishwa madaraja, wenye magonjwa yasiyo na tiba ,wanataka ndoa na kupata wenzi wote wamehamia huko

Jamaa amajaza kama wote vile


Hongera zake ni kupiga pesa ndio muda kabla wengina hawajaibuka

Kila nabii na muda wake
Umezungumzia kupiga pesa basi jua kanuni ni kwamba kila mfanya biashara na soko lake.

Hakuna zama za mfanya biashara mmoja kutamba, kimsingi soko ni kubwa linaongozwa na demand and supply, mbali na hapo consumers wanafuta kanuni ya dunia sinia pakua unachoweza.

Hiyo ndo biashara sijajua kama hiyo biashara ya kupiga pesa kwa unabii inafuata kanuni hzo.
 
Kuna siku nilienda pale nikahesabu kwa haraka haraka kuna sadaka kama saba.....mafuta, maji, gazeti, kuchangia ujenzi, sadaka ya shukrani, sadaka ya kawaida na mchango kwa ajili ya redio.

Ila hata siachi kwenda mweee
 
Back
Top Bottom