Ni wizi huu?

Ni wizi huu?

cc_africa

Senior Member
Joined
May 30, 2010
Posts
121
Reaction score
2
Hali zenu wakuu.

Kuna baadhi ya watu wamejitolea kuja kutuletea kadi za vijana za CCM kwa ajili ya kumchagua mbunge wa jimbo letu.

Tatizo ni kwamba, wakati wa kutuandikisha, wamechukua ID number ya kadi ya kupigia kura pamoja na jina na mwaka nk.

Je kwanini wachukue ID number? Na inahusu nini?
 
Hali zenu wakuu.

Kuna baadhi ya watu wamejitolea kuja kutuletea kadi za vijana za CCM kwa ajili ya kumchagua mbunge wa jimbo letu.

Tatizo ni kwamba, wakati wa kutuandikisha, wamechukua ID number ya kadi ya kupigia kura pamoja na jina na mwaka nk.

Je kwanini wachukue ID number? Na inahusu nini?
Hiyo hairuhusiwi. Ndizo mbinu zao wanazotumia kuiba kura. We utapewaje kadi kama siyo mwanachama? Au kuna kingine zaidi ulichopewa hutaki kutuambia?
 
Wametoa kadi ya CCM ya vijana.tatizo ni kwmba, id number ya kadi ya kupigia kura yanini? Niliamua kufika ofisi za umoja wa vijana CCM,na wamesema haina umuhimu. Je nini lengo lao haswa kuchukua id number? Hebu nisaidieni pengine muna ufahamu zaidi wa kujua lengo lao haswa ni nini?
 
Jina lako kama huko CCM siku ya kupiga kura litakuwa halipo!
 
Wewe una akili kweli wewe CC-AFRICa?! yaani mtu mzima na akili zako unapewa kadi kijinga jinga unapokea? au wamekupa kidogo hutaki kutuambia...Unajua watu kama nyie ndo mnatakiwa mnachapwa viboko kumi na mbili mnatiwa ndani halafu mkitoka vingine kumi na mbili mkawaonyeshe ndugu zenu
 
Back
Top Bottom