Ni wakati wa kumwambia rais ukweli kuwa taifa letu halitajengwa na Wazungu, Wachina wala Waarabu bali watanzania wenyewe

Kyatile

JF-Expert Member
Feb 5, 2017
1,576
1,395
Wakuu,

Kuna imani kuwa Watanzania hawatuwezi kujiendeleza wenyewe na ni viongozi wetu wanatuaminisha hivyo. Matokeo yake mama anatumia muda mwingi nchi za nje kuliko kuifahamu nchi yake. Kinachoendelea ofisi za uma ni vituko na hizo taarifa hawawezi kumpelekea.

Ukweli ni kuwa hao wazungu na waarabu wamejenga nchi zao kwa akili zao, mioyo yao, na nguvu zao. Hawakuendekeza ujinga wa kutokufanya kazi, hawakuzururazurura nchi za wengine kuomba misaada, hawakuendekeza siasa za maji taka, hawakuvumilia kila mtu kula kwa urefu wa kamba yake wala ufisadi huu unaofanyika sasa.

Kama taifa maskini hatuwezi kumudu kubeba mzigo wa wabunge wale wote 400+ bungeni alafu unawalipa posho na mishahara kibao wakati ufanisi wa wengi wao ni sawa na bure.

Hutuwezi kama taifa maskini kumudu kuwa na mawizara yote haya yaliyopo na ukaweza kuwahudumia.

Hutuwezi kumudu gharama na magari ya starehe yanayonunuliwa na serikali kila mwaka kwa ajili ya viongozi.

Hutuwezi kama taifa maskini kuafford rundo la ziara nje ya nchi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada.

Ombi langu raisi afute mawazo finyu ya kuwa wazungu na waarabu watatusaidia kuleta maendeleo. Aelewe kuwa misaada tunayopewa ni short term fixes na haziwezi kujenga maendeleo ya kweli.

Ndiyo maani husikii maziara ya ovyo kwa viongozi wa nchi zinazojielewa.

Aanze program za kuhamasisha kilimo ili tuzalishe chakula kinachotosheleza mahitaji kuanzia nafaka, mafuta pamoja na mazao ya biashara. Tuwe na akiba ya chakula na tuanze kulisha majirani na Afrika yote mpaka Ulaya na Asia.

Tujenge miundo mbinu yetu kwa kasi.

Tuzalishe umeme wa kutosha kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya umeme vinavyopatikana nchini.

Tuanze kusomeshe vijana vyuo vya nchi zilizoendelea huko Ulaya na Asia katika fani za kimkakati na tuwatumie katika maeneo ya hayo.

Baneni matumizi na kuzuia mianya yote ya rushwa. Tungeni sheria kali za kudhibiti rushwa na zifuatwe.

Wastaafu ambao wameshindwa kututoa katika umasikini achaneni nao. Msiwaendekeze. Waacheni wapumzike. Leteni watu wapya wenye ari mpya. Hizi sura tulizozizoea hazina jipya. Zinafiria tu kupata utajiri na mamlaka zaidi. Hivi Wasira, au Mwigulu au Januari au Nape wana lipi jipya la kuleta katika nchi hii?

Tumieni wachache wanaostahili kutumika ila wengi wao hawafai. Achana nao. Achaneni na mambo ya kulipa wenza wa viongozi wakuu. Nafasi hizo zinakuja na manufaa mengi. Kama mtu hawezi kutumika na haridhiki na manufaa yaliyopo sasa asiombe nafasi hizo za uraisi, nk. Acheni upumbavu.

Hamasisheni uzalendo na nyie muwe mfano wa huo uzalendo. Tufanye kazi, tulipe kodi lakini kikubwa zaidi tuone manufaa ya hizo kodi.

Miaka 60 haiendani na maendeleo tuliyo nayo na sababu kubwa ni kuwa na viongozi wengi wabovu wenye uono hafifu na wasio na akili ya kutumia rasilimali tulizo nazo. Huwezi kujenga nchi kwa kuangalia kuwafurahisha watu ndani ya miaka mitano ili wakupe kura. Tujue kuwa wengi wa watu kwenye hii nchi hawaoni mbali.

Tungeni sheria kwa ustawi wa taifa. Ingieni mikataba yenye masilahi ya muda mrefu kwa taifa.

Mama umetembelea nchi nyingi lakini kikubwa tunachokiona sisi huku ni deni la taifa kukua tu na hatuwaoni hao wawekezaji tulio wategemea kuja kuwekeza hasa ukilinganisha na gharama mnazotumia huko mfano kutengeneza sinema ya Royal tour, kusafirisha viongozi katika wingi tunaouona mkiambatana na wasanii akina Steve Nyerere nk

Hii inatuumiza sana kama taifa.
 
Mmm utakuwa umevuta bangi wewe. shirika la tanesco wanaendesha wazawa kutwa nzima umeme kukatika.sisi hatuwezi,tumejaa ubinfsi,uwizi,ujanja ujanja tu htuna lolote.Muuche mama atutafutie wawekezaji.
Tatizo la TANESCO ni kuchaguana kwa kujuana ili kupeana shukrani na kuimarisha urafiki. Maharage Chande wewe unafikiri alichaguliwa kwa merits au uswahiba tu?

Alafu wawekezaji wangapi wameshawekeza tangu aanze kuzunguka huko? Baba yake Rihana?
Hivi hao walioendelea walisaidiwa na nani?

Katika kipindi ambacho mazingira ya dunia na kiwango cha maarifa kilikuwa chini watu walijijenga. Leo dunia imeendelea tunafukiri wazungu ndo waje kutuendeshea TANESCO? Huo ni upumbavu
 
Wakuu,
Kuna imani kuwa Watanzania hawatuwezi kujiendeleza wenyewe na ni viongozi wetu wanatuaminisha hivyo. Matokeo yake mama anatumia muda mwingi nchi za nje kuliko kuifahamu nchi yake. Kinachoendelea ofisi za uma ni vituko na hizo taarifa hawawezi kumpelekea.

Ukweli ni kuwa hao wazungu na waarabu wamejenga nchi zao kwa akili zao, mioyo yao, na nguvu zao. Hawakuendekeza ujinga wa kutokufanya kazi, hawakuzururazurura nchi za wengine kuomba misaada, hawakuendekeza siasa za maji taka, hawakuvumilia kila mtu kula kwa urefu wa kamba yake wala ufisadi huu unaofanyika sasa.

Kama taifa maskini hatuwezi kumudu kubeba mzigo wa wabunge wale wote 400+ bungeni alafu unawalipa posho na mishahara kibao wakati ufanisi wa wengi wao ni sawa na bure.

Hutuwezi kama taifa maskini kumudu kuwa na mawizara yote haya yaliyopo na ukaweza kuwahudumia.

Hutuwezi kumudu gharama na magari ya starehe yanayonunuliwa na serikali kila mwaka kwa ajili ya viongozi.

Hutuwezi kama taifa maskini kuafford rundo la ziara nje ya nchi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada.

Ombi langu raisi afute mawazo finyu ya kuwa wazungu na waarabu watatusaidia kuleta maendeleo. Aelewe kuwa misaada tunayopewa ni short term fixes na haziwezi kujenga maendeleo ya kweli.

Ndiyo maani husikii maziara ya ovyo kwa viongozi wa nchi zinazojielewa.

Aanze program za kuhamasisha kilimo ili tuzalishe chakula kinachotosheleza mahitaji kuanzia nafaka, mafuta pamoja na mazao ya biashara. Tuwe na akiba ya chakula na tuanze kulisha majirani na Afrika yote mpaka Ulaya na Asia.

Tujenge miundo mbinu yetu kwa kasi.

Tuzalishe umeme wa kutosha kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya umeme vinavyopatikana nchini.

Tuanze kusomeshe vijana vyuo vya nchi zilizoendelea huko Ulaya na Asia katika fani za kimkakati na tuwatumie katika maeneo ya hayo.

Baneni matumizi na kuzuia mianya yote ya rushwa. Tungeni sheria kali za kudhibiti rushwa na zifuatwe.

Wastaafu ambao wameshindwa kututoa katika umasikini achaneni nao. Msiwaendekeze. Waacheni wapumzike. Leteni watu wapya wenye ari mpya. Hizi sura tulizozizoea hazina jipya. Zinafiria tu kupata utajiri na mamlaka zaidi. Hivi Wasira, au Mwigulu au Januari au Nape wana lipi jipya la kuleta katika nchi hii?
Tumieni wachache wanaostahili kutumika ila wengi wao hawafai. Achana nao. Achaneni na mambo ya kulipa wenza wa viongozi wakuu. Nafasi hizo zinakuja na manufaa mengi. Kama mtu hawezi kutumika na haridhiki na manufaa yaliyopo sasa asiombe nafasi hizo za uraisi, nk. Acheni upumbavu.

Hamasisheni uzalendo na nyie muwe mfano wa huo uzalendo. Tufanye kazi, tulipe kodi lakini kikubwa zaidi tuone manufaa ya hizo kodi.

Miaka 60 haiendani na maendeleo tuliyo nayo na sababu kubwa ni kuwa na viongozi wengi wabovu wenye uono hafifu na wasio na akili ya kutumia rasilimali tulizo nazo. Huwezi kujenga nchi kwa kuangalia kuwafurahisha watu ndani ya miaka mitano ili wakupe kura. Tujue kuwa wengi wa watu kwenye hii nchi hawaoni mbali.

Tungeni sheria kwa ustawi wa taifa. Ingieni mikataba yenye masilahi ya muda mrefu kwa taifa.

Mama umetembelea nchi nyingi lakini kikubwa tunachokiona sisi huku ni deni la taifa kukua tu na hatuwaoni hao wawekezaji tulio wategemea kuja kuwekeza hasa ukilinganisha na gharama mnazotumia huko mfano kutengeneza sinema ya Royal tour, kusafirisha viongozi katika wingi tunaouona mkiambatana na wasanii akina Steve Nyerere nk

Hii inatuumiza sana kama taifa.
Yes,
Ni kweli kiongozi huyo mkuu wa nchi anasafiri ng'ambo mara kadhaa, sio siri. Uzuri ni kwamba kila akienda na akirudi taarifa ya faida ya safari zake hutolewa kwa umma hadharani mchana kweupe...

vipi wewe mwenzetu,
umefanya nini hapo ulipo achila mbali siku zilizopita, leo. Umeifanyia nini familia na Taifa lako kwa ujumla...
 
Mtanzania hawezi kitu mpaka awekewe mfumo wa kuziba madili na utapeli kazini. Na huo mfumo ukisimamiwa na wawekezaji wa nje ndio utafanya kazi lakini ikiwa ni mtanzania ndio anadhughulika na mfumo hapo ni kama umeongeza daraja jingine la upigaji.
 
mmm kupiga mkelele tu na kubeti.Unaangaika na kiongoz wako akuletee maendeleo hata jembe kushika vijana wa nyakati hii hamtaki.Ningekuelewa kidogo kuwa kiongoz asiangaike kwenda nje maana umetengeneza mtambo wa kuzalisha umeme.Ningekuona wa maana.kila siku unabet nakelele utupigie toka wewee
 
Wakuu,
Kuna imani kuwa Watanzania hawatuwezi kujiendeleza wenyewe na ni viongozi wetu wanatuaminisha hivyo. Matokeo yake mama anatumia muda mwingi nchi za nje kuliko kuifahamu nchi yake. Kinachoendelea ofisi za uma ni vituko na hizo taarifa hawawezi kumpelekea.

Ukweli ni kuwa hao wazungu na waarabu wamejenga nchi zao kwa akili zao, mioyo yao, na nguvu zao. Hawakuendekeza ujinga wa kutokufanya kazi, hawakuzururazurura nchi za wengine kuomba misaada, hawakuendekeza siasa za maji taka, hawakuvumilia kila mtu kula kwa urefu wa kamba yake wala ufisadi huu unaofanyika sasa.

Kama taifa maskini hatuwezi kumudu kubeba mzigo wa wabunge wale wote 400+ bungeni alafu unawalipa posho na mishahara kibao wakati ufanisi wa wengi wao ni sawa na bure.

Hutuwezi kama taifa maskini kumudu kuwa na mawizara yote haya yaliyopo na ukaweza kuwahudumia.

Hutuwezi kumudu gharama na magari ya starehe yanayonunuliwa na serikali kila mwaka kwa ajili ya viongozi.

Hutuwezi kama taifa maskini kuafford rundo la ziara nje ya nchi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada.

Ombi langu raisi afute mawazo finyu ya kuwa wazungu na waarabu watatusaidia kuleta maendeleo. Aelewe kuwa misaada tunayopewa ni short term fixes na haziwezi kujenga maendeleo ya kweli.

Ndiyo maani husikii maziara ya ovyo kwa viongozi wa nchi zinazojielewa.

Aanze program za kuhamasisha kilimo ili tuzalishe chakula kinachotosheleza mahitaji kuanzia nafaka, mafuta pamoja na mazao ya biashara. Tuwe na akiba ya chakula na tuanze kulisha majirani na Afrika yote mpaka Ulaya na Asia.

Tujenge miundo mbinu yetu kwa kasi.

Tuzalishe umeme wa kutosha kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya umeme vinavyopatikana nchini.

Tuanze kusomeshe vijana vyuo vya nchi zilizoendelea huko Ulaya na Asia katika fani za kimkakati na tuwatumie katika maeneo ya hayo.

Baneni matumizi na kuzuia mianya yote ya rushwa. Tungeni sheria kali za kudhibiti rushwa na zifuatwe.

Wastaafu ambao wameshindwa kututoa katika umasikini achaneni nao. Msiwaendekeze. Waacheni wapumzike. Leteni watu wapya wenye ari mpya. Hizi sura tulizozizoea hazina jipya. Zinafiria tu kupata utajiri na mamlaka zaidi. Hivi Wasira, au Mwigulu au Januari au Nape wana lipi jipya la kuleta katika nchi hii?
Tumieni wachache wanaostahili kutumika ila wengi wao hawafai. Achana nao. Achaneni na mambo ya kulipa wenza wa viongozi wakuu. Nafasi hizo zinakuja na manufaa mengi. Kama mtu hawezi kutumika na haridhiki na manufaa yaliyopo sasa asiombe nafasi hizo za uraisi, nk. Acheni upumbavu.

Hamasisheni uzalendo na nyie muwe mfano wa huo uzalendo. Tufanye kazi, tulipe kodi lakini kikubwa zaidi tuone manufaa ya hizo kodi.

Miaka 60 haiendani na maendeleo tuliyo nayo na sababu kubwa ni kuwa na viongozi wengi wabovu wenye uono hafifu na wasio na akili ya kutumia rasilimali tulizo nazo. Huwezi kujenga nchi kwa kuangalia kuwafurahisha watu ndani ya miaka mitano ili wakupe kura. Tujue kuwa wengi wa watu kwenye hii nchi hawaoni mbali.

Tungeni sheria kwa ustawi wa taifa. Ingieni mikataba yenye masilahi ya muda mrefu kwa taifa.

Mama umetembelea nchi nyingi lakini kikubwa tunachokiona sisi huku ni deni la taifa kukua tu na hatuwaoni hao wawekezaji tulio wategemea kuja kuwekeza hasa ukilinganisha na gharama mnazotumia huko mfano kutengeneza sinema ya Royal tour, kusafirisha viongozi katika wingi tunaouona mkiambatana na wasanii akina Steve Nyerere nk

Hii inatuumiza sana kama taifa.
NAKAZIA
 
Yes,
Ni kweli kiongozi huyo mkuu wa nchi anasafiri ng'ambo mara kadhaa, sio siri. Uzuri ni kwamba kila akienda na akirudi taarifa ya faida ya safari zake hutolewa kwa umma hadharani mchana kweupe...

vipi wewe mwenzetu,
umefanya nini hapo ulipo achila mbali siku zilizopita, leo. Umeifanyia nini familia na Taifa lako kwa ujumla...
Manufaa yako wapi? Nimekuuliza semeni wawekezaji wawili tu na wamewekeza mtaji kiasi gani? Na over sometimes tuta-acquire teknolojia gani? Ajira zitatengenezwa ngapi na serikali itapata kiasi gani?

Alafu wewe bado upo kwenye ujinga wa kuambiwa mafanikio kwenye mitandao?
Hakuna mwenye akili anafanya huo ujinga.
 
Manufaa yako wapi? Nimekuuliza semeni wawekezaji wawili tu na wamewekeza mtaji kiasi gani? Na over sometimes tuta-acquire teknolojia gani? Ajili zitatengenezwa ngapi na serikali itapata kiasi gani?

Alafu wewe bado upo kwenye ujinga wa kuambiwa mafanikio kwenye mitandao?
Hakuna mwenye akili anafanya huo ujinga.
kwamba na mimi nichochewe na mihemko na ghadhabu kukueleza habari ya maendeleo makubwa sana nchini, tena yanaonekana mpaka kwa macho ya nyama, mathalalani mabarabara, mareli, mabwawa, mahospitali, mashule, midege mikubwa, makundi ya watalii, maboresho bandarini na angani, viwanda, kilimo, mifugo, uvuvi kwamba huoni kabisa hatua zilizopigwa, ni ngumu kuyaona haya ikiwa umezira moyo unauma...

Kuhusu gharama za uwekezaji,
Uliziba maskio au ulizira kuskia kama kawaida, kwamba hujui wala huelewi
nani kawekeza wapi, kiasi gani na nchi na Wananchi wanafaidika na nini, sasa mimi ndio nikueleze wewe?
Si ulizira....

Katika maeneo yote ya uwekezaji ajira hazikosekani,zipo ajira rasmi na zisizo rasmi.
Zaidi sana ajira za kutosha na za uhakika ni pamoja na kwenye sekta ya kilimo, biashara, mifugo, uvuvi, Michezo na sanaa kwa uchache....

Kupata taarrifa mtandaoni sio ujinga, ni maendeleo ya teknologia katika habari na mawasiliono, na kwahivyo usibeze platform hii muhimu ambayo na wew unaitumia hivi sasa kutaka kujua mengi zaid.

Jambo la muhimu kuzira sio deal, utakosa mengi wenzie wasonga mbele....
 
Mmm utakuwa umevuta bangi wewe. shirika la tanesco wanaendesha wazawa kutwa nzima umeme kukatika.sisi hatuwezi,tumejaa ubinfsi,uwizi,ujanja ujanja tu htuna lolote.Muuche mama atutafutie wawekezaji.
N muhimu kujua yafutayo kwa faida ya mtu mmoja mmoja, jamii na taifa kwa ujumla;
1. Wawekezaji wote wanatafuta faida yao na ya nchi zao. Hakuna anayewekeza ili afaidishe Tanzania.
2. Maendeleo ya nchi yoyote ile, hutegemea raia wake wanavyofanya kazi kwa bidii kwa faida yao binafsi na taifa lao kwa ujumla.
3. Misaada na mikopo kutoka nje kamwe haiwezi kuendeleza taifa na zaidi sana ni kulididimiza.
4. Viongozi wa nchi masikini hutekwa kifikra na nchi tajiri kupitia mikopo na misaada ili kuwanyonya na kuwatesa raia wao bila kujua ukweli huu.
 
Wakuu,

Kuna imani kuwa Watanzania hawatuwezi kujiendeleza wenyewe na ni viongozi wetu wanatuaminisha hivyo. Matokeo yake mama anatumia muda mwingi nchi za nje kuliko kuifahamu nchi yake. Kinachoendelea ofisi za uma ni vituko na hizo taarifa hawawezi kumpelekea.

Ukweli ni kuwa hao wazungu na waarabu wamejenga nchi zao kwa akili zao, mioyo yao, na nguvu zao. Hawakuendekeza ujinga wa kutokufanya kazi, hawakuzururazurura nchi za wengine kuomba misaada, hawakuendekeza siasa za maji taka, hawakuvumilia kila mtu kula kwa urefu wa kamba yake wala ufisadi huu unaofanyika sasa.

Kama taifa maskini hatuwezi kumudu kubeba mzigo wa wabunge wale wote 400+ bungeni alafu unawalipa posho na mishahara kibao wakati ufanisi wa wengi wao ni sawa na bure.

Hutuwezi kama taifa maskini kumudu kuwa na mawizara yote haya yaliyopo na ukaweza kuwahudumia.

Hutuwezi kumudu gharama na magari ya starehe yanayonunuliwa na serikali kila mwaka kwa ajili ya viongozi.

Hutuwezi kama taifa maskini kuafford rundo la ziara nje ya nchi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada.

Ombi langu raisi afute mawazo finyu ya kuwa wazungu na waarabu watatusaidia kuleta maendeleo. Aelewe kuwa misaada tunayopewa ni short term fixes na haziwezi kujenga maendeleo ya kweli.

Ndiyo maani husikii maziara ya ovyo kwa viongozi wa nchi zinazojielewa.

Aanze program za kuhamasisha kilimo ili tuzalishe chakula kinachotosheleza mahitaji kuanzia nafaka, mafuta pamoja na mazao ya biashara. Tuwe na akiba ya chakula na tuanze kulisha majirani na Afrika yote mpaka Ulaya na Asia.

Tujenge miundo mbinu yetu kwa kasi.

Tuzalishe umeme wa kutosha kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya umeme vinavyopatikana nchini.

Tuanze kusomeshe vijana vyuo vya nchi zilizoendelea huko Ulaya na Asia katika fani za kimkakati na tuwatumie katika maeneo ya hayo.

Baneni matumizi na kuzuia mianya yote ya rushwa. Tungeni sheria kali za kudhibiti rushwa na zifuatwe.

Wastaafu ambao wameshindwa kututoa katika umasikini achaneni nao. Msiwaendekeze. Waacheni wapumzike. Leteni watu wapya wenye ari mpya. Hizi sura tulizozizoea hazina jipya. Zinafiria tu kupata utajiri na mamlaka zaidi. Hivi Wasira, au Mwigulu au Januari au Nape wana lipi jipya la kuleta katika nchi hii?

Tumieni wachache wanaostahili kutumika ila wengi wao hawafai. Achana nao. Achaneni na mambo ya kulipa wenza wa viongozi wakuu. Nafasi hizo zinakuja na manufaa mengi. Kama mtu hawezi kutumika na haridhiki na manufaa yaliyopo sasa asiombe nafasi hizo za uraisi, nk. Acheni upumbavu.

Hamasisheni uzalendo na nyie muwe mfano wa huo uzalendo. Tufanye kazi, tulipe kodi lakini kikubwa zaidi tuone manufaa ya hizo kodi.

Miaka 60 haiendani na maendeleo tuliyo nayo na sababu kubwa ni kuwa na viongozi wengi wabovu wenye uono hafifu na wasio na akili ya kutumia rasilimali tulizo nazo. Huwezi kujenga nchi kwa kuangalia kuwafurahisha watu ndani ya miaka mitano ili wakupe kura. Tujue kuwa wengi wa watu kwenye hii nchi hawaoni mbali.

Tungeni sheria kwa ustawi wa taifa. Ingieni mikataba yenye masilahi ya muda mrefu kwa taifa.

Mama umetembelea nchi nyingi lakini kikubwa tunachokiona sisi huku ni deni la taifa kukua tu na hatuwaoni hao wawekezaji tulio wategemea kuja kuwekeza hasa ukilinganisha na gharama mnazotumia huko mfano kutengeneza sinema ya Royal tour, kusafirisha viongozi katika wingi tunaouona mkiambatana na wasanii akina Steve Nyerere nk

Hii inatuumiza sana kama taifa.
Yaani unamleta Mwarabu kuja kuchota rasilimali za nchi Yako Kwa Sababu ya mahaba tu ya kiitikadi.
Mwarabu Ametoka kwenye nchi ambayo uzinzi adhabu yake ni kifo, ufisadi ,adhabu yake ni kifo, Rushwa adhabu yake ni kifo, Riba ni haramu , pombe ni haramu, madawa ya kulevya adhabu yake ni kifo, Halafu unamkabidhi rasilimali zote Za nchi Yako ikiwemo bandari WAKATI Sheria zako ni nyepesi na zina mianya mingi ya Wizi.
Nchi yetu ambayo uzinzi hauna adhabu, ulevi ni starehe ya MTU, Rushwa ni ujanja Wa MTU kula Kwa urefu Wa kamba yake. Ukiiba bil. 250 basi, mawakili , wapelelezi,mahakimu ,majaji na Wananchi wanakupisha kiti ukae Halafu wakuhoji wakiwa wamesimama Huku wakiwa wanataja shida Zao mbele Yako , nchi ámbayo madawa ya kulevya ni Dili la wakubwa, Riba ni Dili la serikali na mabepari kuwanyonga wanyonge.
Bila shaka Mwarabu au machina atashangilia sana kuja kujichotea Mali kwenye nchi kama hiyo kwani atafanya Kazi zake bila hofu ya kuhujumu nchi mana hakuna kitakachoshindikana mbele ya pesa.

Tulitegemea Kabla ya kuwapa Waarabu na wachina rasilimali zetu watitawale basi tumgewatungia Sheria zinazofanana na za kule kwao au wahukumiwe Kwa Sheri ngumu za kwao. Sheria za wazingu wanazozitaka ni nyepesi na hua hawazifuati kwani zinatoa Haki Kwa mtuhumiwa kuliko mlalamikaji
 
Mmm utakuwa umevuta bangi wewe. shirika la tanesco wanaendesha wazawa kutwa nzima umeme kukatika.sisi hatuwezi,tumejaa ubinfsi,uwizi,ujanja ujanja tu htuna lolote.Muuche mama atutafutie wawekezaji.
Mkuu hakuna watu wabinafsi na wajanja janja kama Hao wahindi,waarabu na wachina. Ndio Maana kwao wamwekewa Sheria ngumu sana za kunyongwa Kwa makosa madago madogo kama vile uzinzi. Yaani kukosa uaminifu tu kwenye ndoa MTU anamyongwa sembuse kuiba Mali za umma.
Ushenzi wa wanadamu ndio uliopelekea Mungu akawawelea Sheria Kali Ili wawe watu Wema Kwa Lazima.

Sasa unamteua Kada Wa Chama cha Mapinduzi unamweka bandarini kisha anakuchotea pesa Kwa ajili ya kuhonga urudi madarakani Halafu Unakuja kusikia Naye anajilimbikizia Mali Kwa mamilioni utamwajibisha vipi? Utawelaje Sheria ya kumnyonga WAKATI watawala ndio waliomwambia awachotee pesa za uchaguzi.

Hao Waarabu pia kwa Sheria hizi za kutumia busara tu na akili kichwani wataiba fedha nyingi na kwenda kuwekeza Maeneo mengine. Waarabu hawajaja kuwakilisha Malaika ,wamekuja kufanya biashara. Unawapa 40 % wachote wapeleke kwao kihalali. WAKATI umezuia 10% ya wezi Wa ndani walizokua wanaiba wakanunue mabatí na kujenga kule kisarawe.
Ni ujuha mkubwa sana.
Waarabu watatorosha fedha nyingi sana kushirikiana na wezi Wa ndani na Kwa aibu watawala hawatazungumzia Tena Suala la bandari na hawatakua na mamlaka ya kuwafokea Waarabu na kutangaza kinachoendelea kama walivyofyata mkia kwanye Suala la gesi , Madini ,na Loliondo. Hayo Maeneo tuliambiwa yataleta Mapinduzi makubwa ya kiuchumi na kuanzishwa kwa mfuko maalumu Wa kuweka Akiba Kwa ajili ya vizazi vijavyo . Kumbe ni Kwa ajili ya matumbo Yao na vizazi vyao.

Kiufupi CCM na viongozi wake Wote walipaswa kuwa wamenyongwa Kwa ajili ya Kesho njema ya Taifa hili na vizazi vijavyo . Badala yake taifa limenyongwa Kwa manufaa yao na Wageni Wao.
 
Tatizo la TANESCO ni kuchaguana kwa kujuana ili kupeana shukrani na kuimarisha urafiki. Maharage Chande wewe unafikiri alichaguliwa kwa merits au uswahiba tu?

Alafu wawekezaji wangapi wameshawekeza tangu aanze kuzunguka huko? Baba yake Rihana?
Hivi hao walioendelea walisaidiwa na nani?

Katika kipindi ambacho mazingira ya dunia na kiwango cha maarifa kilikuwa chini watu walijijenga. Leo dunia imeendelea tunafukiri wazungu ndo waje kutuendeshea TANESCO? Huo ni upumbavu
Mfano tu Yule jamaa Wa NHC.
Amechaguliwa Kwa Manufaa yao SIO manufaa ya Taifa.

Yaani kukusanya Kodi ya pango la Nyumba zilizojaa Karibu miji yote Tanzania anashindwa na Badala yake serikali inapitisha ruzuku Tena Ili wakagawane kijanja.
Utaondoaje Umaskini kama unashindwa kucontrol Suala la Makazi Kwa watu wako? Yaani Wizi mkubwa serikalini ni Ili Kila MTU ajijengee kibanda chake na kupangisha . Sasa kama Nyerere alishataifisha Nyumba nyingi Ilikua ni rahisi tu kujenga Nyumba zaidí na za Bei rahisi Ili wanaowaza kuiba Ili wajenge Nyumba za kupangisha wawaze Jambo Lingine la kuwekeza Mwingine Hata viwanda na SIO Nyumba zisizotoa ajira.

Kila Sehemu wanaweka watu Kwa kupeana Kwa manufaa yao SIO Taifa Halafu wanaleta Waarabu na wachina Kwa manufaa yao Tena mana Wanajua wazo kuwa hakuna jipya kutoka nje zaidí ya kundeleza Mikopo na misaada.
Wahuni sio watu wazuri
 
Back
Top Bottom