Ni vema polisi wakalipa gharama za matibabu za shujaa huyu

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,311
3,341
Kwanza nianze kwakusema mpaka hapa silaumu kitengo cha polisi kwani huenda hakijafanya hili kwakukosa taarifa.

Leo kupitia taarifa ya habari ya clouds TV ameoneshwa kijana dereva wa bodaboda ambaye kwa ushujaa mkubwa alifanikisha kukamatwa kwa jambazi Dar es Salaam.

Shujaa huyu ambaye aliwachomekea majambazi akiwa kwenye pikipiki na kupelekea yeye pamoja na pikipiki ya majambazi kuanguka jambo ambalo lilifanikisha kukamatwa kwa majambazi hao kwa urahisi na askari.

Shujaa huyu licha ya kupata majeraha kwakuanguka na pikipiki lakini pia alipigwa risasi na jambazi iliopelekea kukimbizwa Muhimbili.

Amepata tiba lakini tatizo ni gharama za matibabu inahitajika 500,000 ili aruhusiwe pesa ambayo yeye hana.

Naamini kama polisi hua mnatangaza mpaka dau la 1,000,000 ili kufanikisha kukamatwa kwa majambazi naamini hamshindwi kulipa 500,000 ya matibabu na hata pesa ya ziada kama motisha kwa ujasiri aliounesha.
 
hawa ndo mashujaa wanaohitajika katika jamii yetu the few who will take heroic actions for the society
 
Najua huamini lakini hivyo ndivyo ilivyo maelezo yanayotolewa huyo bidabida ameonesha ujasiri wa hali ya juu inawezekana hata baadhi ya askari hawana,ni vema angefutwa machozi@mchambuzi
 
image.jpeg
image.jpeg
image.jpeg


Hii ni habari ya dereva wa bodaboda wa Kituo cha Magomeni Kagera Jijini Dsm ambaye miezi kadhaa iliyopita alijitoa kupambana na majambazi waliokuwa wamefanya uhalifu.
Akisimulia huku akilia kwa uchungu,kijana huyo anakumbuka siku aliyoamua kujitolea kuwakamata majambazi waliokuwa wamefanya uhalifu.

Anasimulia kuwa alishuhudia majambazi waliopora na kujeruhi watu,yeye akiwa na bodaboda aliamua "kuwachomekea" pikipiki majambazi hao wakati wanakimbia,akafanikisha kusababisha wadondoke chini,huku hilo likiendelea jambazi mmoja alichomoa bastora kiunoni mwake na kumtandika dereva huyo.Majeraha ya kijana huyo yalisababisha kulazwa kwa muda hospitali ya Taifa ya Muhimbili,akipata matibabu kwa msaada wa wenzake waliojitolea kidogo walichonacho ili ndugu yao apone.

Sasa ni siku ya nne toka ameruhusiwa kutoka hospital,lkn hospital ya Muhimbili "imemzuia" mpaka pale atakapolipa deni lao,kijana huyo amekuwa akilia kutwa kucha sbb hana pesa ya kulipia na hawezi kuruhusiwa kutoka,huku wenzake wa eneo la Kagera wakitishia kwenda kumtorosha maana anadaiwa pesa nyingi hivyo wao hawawezi kumudu ghalama.

Kwa majonzi na masikitiko,kijana huyo amekuwa anashinda kutwa kucha akilia na kuomba msaada
 
Back
Top Bottom