Ni utoto au ulimbukeni?

Ni utoto au ulimbukeni?

tang'ana

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2015
Posts
12,054
Reaction score
16,509
Kuna hii tabia ya watu ambao sio mke na mume kuwekana picha zao kule watsapp na kuandika status kama my hubby to be etc. Hivi ni sahihi kumuanika mtu ambae ni mpenzi tu ambae anytime mnaweza kumwagana?
 
Mimi whatsapp na mitandao ya kijamii naipa heshima kubwa na siwezi weka picha huko....
Wanatambishiana tu
 
Sio tatizo, inategemea mnaishi vipi .mnamategemeo gani? Mmefikia steji gani ya kuelekea marriage?? Na culture tuu ya nyinyi wahusika...
Kuweka wazi inasaidia kujihami dhidi ya wezi wa wapenzi wa wenzao...
Pia hasara yake ni kujifanyia exposure isiyokuwa na maaana..mkibwagana aibu saana
 
Hebu mi nikimbie nisije kamatwa na huyo mbuni teh teh teh
 
Ni utoto na ulimbukeni pia,mtu mama yako wala baba yako hawamfahamu,unamweka kwenye profile then unaandka na status... mi nadhani hii inategemeana na parenting style ya mweka picha pamoja na heshima ya wazazi wa huyo mweka picha,kama mtu familia yako ni ya heshima huwezi kufanya hivyo,na hii itaendelea tu kwasababu hivi ninavyoandika kuna mtu anabalehe au kuvunja ungo,na kwa hali hiyo,labda anajaribu kuweka..
 
inategemea na jinsi walivyo shibana, alafu pia kila mtu anamamuzi na matakwa yake binafs so sizan kama kuweka picha ya mpenzio n ulimbuken
 
Kuna mmoja aliniweka nilipogundua tu na ndio mwisho wetu.
 
Mwanamke yoyote ambaye ninamahusiano naye kimapenzi, akiweka picha yangu kwenye profile yake, na mimi naweka yake, ikiambatana na status "nimem-mwaga sasa hiviii"
 
Mwanamke yoyote ambaye ninamahusiano naye kimapenzi, akiweka picha yangu kwenye profile yake, na mimi naweka yake, ikiambatana na status "nimem-mwaga sasa hiviii"

Teh teh teh teh,mweeehh....JF raha jmn
 
ni kitu kisichowezekana kwang nakuweka ili iweje cku hz hakuna wa kumuamini na 2kimwagana je? hapo aibuu HUO NI ULIMBUKENI
 
Waache wakiweka inakunyima usingizi? Nchi hii ni ya Haki.. Everybody lives according to his or her Own Principles.. Waacheni Wakiweka Ni Sawa wewe Ukificha usipo weka ni sawa. Wala Hakuna shida kuhusu hilo. Mkuu Mbona inakuuma? Haya ni Mambo madogo tu yakueleweka.
 
Maisha ni namna unavoamua mwenyewe, kama ww unavoamua kutoweka mwingine kaamua kuweka. Hii ni personal, fanya yanayokuhusu ndo bora zaidi
 
Back
Top Bottom