Ni tàkwa la kimaadili kuiamini Serikali

Ni tàkwa la kimaadili kuiamini Serikali

Superbug

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
16,466
Reaction score
42,602
Sio sahihi raia kutilia Shaka taarifa za Serikali. Tukumbuke ina dhamana kubwa kuliko sisi wote mmoja mmoja.

Serikali inafanya Mambo kwa mujibu wa sheria na matakwa ya kikatiba kwa maslahi mapana ya nchi na taifa kwa ujumla.

Kuteleza kumo kwani Serikali haziongozwi na malaika.

Niwajibu wetu kuamini taarifa za Serikali.
 
Amini wewe sio lazima kila mtu aziamini taarifa zao. Na sababu ya kutokuziamini ziko wazi.
 
Unakumbuka zilitangazwa ajira 13000 za waalimu, watu wakatilia shaka idadi iliyotolewa, ndipo serikali ikasema tumetoa 8000?

Unamwambiaje Lissu na wenzake kuhusu serikali kutaka akatibiwe kwanza Muhimbili na si nje ya nchi baada ya lile shambulio,ulitaka waiamini serikali na kumpeleka Lissu Muhimbili?

Hayo ni machache.
 
Back
Top Bottom