Maandamano:
Mapendekezo ya serikali kutaka kuleta sheria ya kuzuia maandamano kutaligharimu taifa kama sio leo ni kesho au kama sio kesho ni keshokutwa. Maandamano ni namna ya watu kuelezea hisia zao zinaweza kuwa furaha au huzuni, mathalani ikiwa ni hisia za huzuni, chuki na hasira zinapozuiwa zinakua hivyo upo wakati unafika ambapo njia nyingine za hatari hutumika na wananchi kuelezea hayo kwa viongozi wao. Hayo yakitumika gharama yake kwa taifa ni kubwa sana, nadhani ni wakati muafaka serikali itafute suluhu ya matatizo ya wananchi wake na sio kwenda kufanya kichaka cha kujifichia sheria wanazoweza kuzitunga!
Nashauri serikali ipime na ione inafanya hayo kwa faida ya nani kama ni kisiasa au ni kuwakomoa wananchi? Na je wamepima madhara ya baadae kwa Taifa letu?
Mapendekezo ya serikali kutaka kuleta sheria ya kuzuia maandamano kutaligharimu taifa kama sio leo ni kesho au kama sio kesho ni keshokutwa. Maandamano ni namna ya watu kuelezea hisia zao zinaweza kuwa furaha au huzuni, mathalani ikiwa ni hisia za huzuni, chuki na hasira zinapozuiwa zinakua hivyo upo wakati unafika ambapo njia nyingine za hatari hutumika na wananchi kuelezea hayo kwa viongozi wao. Hayo yakitumika gharama yake kwa taifa ni kubwa sana, nadhani ni wakati muafaka serikali itafute suluhu ya matatizo ya wananchi wake na sio kwenda kufanya kichaka cha kujifichia sheria wanazoweza kuzitunga!
Nashauri serikali ipime na ione inafanya hayo kwa faida ya nani kama ni kisiasa au ni kuwakomoa wananchi? Na je wamepima madhara ya baadae kwa Taifa letu?