GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,571
- 108,921
Siku zote nitasimama katika ukweli na katikati bila kuwa ' Mnafiki ' au Kumuonea fulani na hivyo ndivyo nitakavyokuwa siku zote. Kwa masikitiko makubwa kabisa nimekuwa nikifuatilia sehemu mbalimbali hasa Mitandoni humu na kujikuta sasa naanza kupata wasiwasi juu ya muelekeo wa Watanzania wengi.
Yaani Watanzania badala ya kuwekeza nguvu zetu nyingi katika Kumuombea Afya Njema Ndugu yetu ( Mtani wangu ) Ruge Mutahaba kutokana na matatizo yake ya ' Figo ' ambayo yanamsumbua kwa Kipindi kirefu tu sasa wengi wetu tumeanza kuhamisha Goli na kuanza ' Kumsingizia ' Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Makonda kwamba amemlisha ' Sumu ' inayomuua taratibu kwakuwa tu inasemekana wana ' Uadui ' japo Mimi GENTAMYCINE naamini kuwa umeshaisha na Wawili hawa wapo vizuri tu.
Najua leo GENTAMYCINE nitawaudhi wale ambao ' wanamchukia ' Mkuu wa Mkoa Makonda kwa sababu zao mbalimbali ila mtanisamehe tu kwakuwa huwa napenda ' Haki ' na ' Usawa ' baina ya Wawili unaochagizwa na ukweli pamoja na uhalisia wa jambo husika.
Nimeona mahala kuna Mtu mmoja ( anayeaminika sana na Watanzania wenye mrengo wa Kushoto ) akisema kwamba hata Bosi Ruge Mutahaba nae pia anaamini na ana uhakika wa 100% kuwa Ugonjwa wake huo unatokana na kuwekewa ' Sumu ' inayomuua taratibu na huyo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Makonda.
Kama ni kweli Mtani wangu Ruge Mutahaba maneno haya ameyasema Yeye basi nitaanza Kumpunguzia ' marks ' zangu za ' Umakini ' ambazo nimemuwekea tokea nianze Kumfahamu kwakuwa ni Mtu mmoja ambaye namkubali sana na hasa kutokana na uwezo wake mkubwa mno wa Ubunifu, Uthubutu na Utendaji Kazi wake. Ila mpaka sasa siamini kama kweli Ruge amesema haya maneno ambayo huyo ' Mtanzania Mghaibuni ' anayaeneza.
Kwa sababu za Kimaadili na hasa kwa taarifa za Afya ya Mtu huwa si desturi nzuri kwa Mtu kuanza ama Kuuzungumzia au hata Kuutaja Ugonjwa wa Mtu lakini hapa niseme tu ya kwamba tatizo hilo la Figo la Ruge Mutahaba halijaanza leo na tena kwa taarifa ambazo nimepewa ni kwamba kumbe hili tatizo la Figo limekuwa likimsumbua Ruge hata kabla Makonda hawaja ama Mkuu wa Wilaya au hivi Mkuu wa Mkoa na nimesikitika na bado naendelea kusikitika kuona sasa anahusishwa nalo.
Hata kama tunamchukia ila tujitahidi muda mwingine kutokuwa ' Wazushi ' mwishowe tukajikuta tunajichumia bure dhambi kwa Mwenyezi Mungu. Muda mwingine tufanye mambo kwa kumuogopa Mola / Allah. Najua kuwa Makonda kuna muda anakera na kuudhi na hata Mimi GENTAMYCINE huwa ' ananishangaza ' na nimekuwa nikimsema mno hapa Jamvini JF lakini kwa hili tunalomuhusisha nalo nina uhakika wa 100% kwamba wengi wetu tunaomsingizia na kumuhisha nalo tunajichumia bure dhambi na ipo siku zitakuja Kututesa.
Tumseme Mtu kwa haki na siyo kwa Kumsingizia ama Kumzushia kwani siyo jambo zuri na halina Tija wala Afya Kwetu.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda endelea na Kazi zako za Kiutendaji ila Mimi kama GENTAMYCINE nakuomba kama itakuwa chini ya uwezo wako na najua unaweza na una Mamlaka kama Mkuu wetu wa Mkoa hebu livalie njua upesi sakata la akina Maua Sama, Soudy Brown na Shaffih Dauda ili basi waweze kuachiwa hata kwa dhamana. Sitaki pia kuamini kwamba unahusika kwa wao kuwepo ndani huko waliko sasa ila nakuomba tu ' wapiganie ' ili wawe huru na naamini watajirekebisha na maisha yataendelea.
Nitashukuru sana kama Ombi langu hili utalifanyia Kazi na najua hutoniangusha GENTAMYCINE katika hili. Akhsante.
Nawasilisha.
Yaani Watanzania badala ya kuwekeza nguvu zetu nyingi katika Kumuombea Afya Njema Ndugu yetu ( Mtani wangu ) Ruge Mutahaba kutokana na matatizo yake ya ' Figo ' ambayo yanamsumbua kwa Kipindi kirefu tu sasa wengi wetu tumeanza kuhamisha Goli na kuanza ' Kumsingizia ' Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Makonda kwamba amemlisha ' Sumu ' inayomuua taratibu kwakuwa tu inasemekana wana ' Uadui ' japo Mimi GENTAMYCINE naamini kuwa umeshaisha na Wawili hawa wapo vizuri tu.
Najua leo GENTAMYCINE nitawaudhi wale ambao ' wanamchukia ' Mkuu wa Mkoa Makonda kwa sababu zao mbalimbali ila mtanisamehe tu kwakuwa huwa napenda ' Haki ' na ' Usawa ' baina ya Wawili unaochagizwa na ukweli pamoja na uhalisia wa jambo husika.
Nimeona mahala kuna Mtu mmoja ( anayeaminika sana na Watanzania wenye mrengo wa Kushoto ) akisema kwamba hata Bosi Ruge Mutahaba nae pia anaamini na ana uhakika wa 100% kuwa Ugonjwa wake huo unatokana na kuwekewa ' Sumu ' inayomuua taratibu na huyo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Makonda.
Kama ni kweli Mtani wangu Ruge Mutahaba maneno haya ameyasema Yeye basi nitaanza Kumpunguzia ' marks ' zangu za ' Umakini ' ambazo nimemuwekea tokea nianze Kumfahamu kwakuwa ni Mtu mmoja ambaye namkubali sana na hasa kutokana na uwezo wake mkubwa mno wa Ubunifu, Uthubutu na Utendaji Kazi wake. Ila mpaka sasa siamini kama kweli Ruge amesema haya maneno ambayo huyo ' Mtanzania Mghaibuni ' anayaeneza.
Kwa sababu za Kimaadili na hasa kwa taarifa za Afya ya Mtu huwa si desturi nzuri kwa Mtu kuanza ama Kuuzungumzia au hata Kuutaja Ugonjwa wa Mtu lakini hapa niseme tu ya kwamba tatizo hilo la Figo la Ruge Mutahaba halijaanza leo na tena kwa taarifa ambazo nimepewa ni kwamba kumbe hili tatizo la Figo limekuwa likimsumbua Ruge hata kabla Makonda hawaja ama Mkuu wa Wilaya au hivi Mkuu wa Mkoa na nimesikitika na bado naendelea kusikitika kuona sasa anahusishwa nalo.
Hata kama tunamchukia ila tujitahidi muda mwingine kutokuwa ' Wazushi ' mwishowe tukajikuta tunajichumia bure dhambi kwa Mwenyezi Mungu. Muda mwingine tufanye mambo kwa kumuogopa Mola / Allah. Najua kuwa Makonda kuna muda anakera na kuudhi na hata Mimi GENTAMYCINE huwa ' ananishangaza ' na nimekuwa nikimsema mno hapa Jamvini JF lakini kwa hili tunalomuhusisha nalo nina uhakika wa 100% kwamba wengi wetu tunaomsingizia na kumuhisha nalo tunajichumia bure dhambi na ipo siku zitakuja Kututesa.
Tumseme Mtu kwa haki na siyo kwa Kumsingizia ama Kumzushia kwani siyo jambo zuri na halina Tija wala Afya Kwetu.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda endelea na Kazi zako za Kiutendaji ila Mimi kama GENTAMYCINE nakuomba kama itakuwa chini ya uwezo wako na najua unaweza na una Mamlaka kama Mkuu wetu wa Mkoa hebu livalie njua upesi sakata la akina Maua Sama, Soudy Brown na Shaffih Dauda ili basi waweze kuachiwa hata kwa dhamana. Sitaki pia kuamini kwamba unahusika kwa wao kuwepo ndani huko waliko sasa ila nakuomba tu ' wapiganie ' ili wawe huru na naamini watajirekebisha na maisha yataendelea.
Nitashukuru sana kama Ombi langu hili utalifanyia Kazi na najua hutoniangusha GENTAMYCINE katika hili. Akhsante.
Nawasilisha.