Ni kweli binadamu wote duniani ni sawa?

Ni kweli binadamu wote duniani ni sawa?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
57,362
Reaction score
90,669
Huu msemo kwamba binadamu wote ni sawa huwa na maana gani?

Mbona kuna baadhi ya binadamu mfano Wajapan na Wazungu huwa wanafanya mambo yanaonekana kama ni viumbe kutoka sayari nyingine!
20250905_175516.jpg
 
Nahisi walimaanisha tupo sawa kwa kuwa wote ni "Social creatures", wote tunahitaji kupenda na kupendwa, kuwa miongoni mwa jamii, wote tuna zaliwa tuna pitia matatizo na wote tuna kufa
 
Jibu lipo kwenye swali lako unamaanisha usawa wa nini ? Unaongelea Wajapan, Je unamaanisha chizi wa Japan ni zaidi ya Genius wa Aboriginal kule Australia ?!!; Necessity is the mother of all invention..., kwahio binadamu wote kwa ujumla wana akili ya kuweza kupambana na tatizo linalowakumba kwa wakati husika..., Pia huitaji umati wa watu kufanya vitu pioneers wachache wanaweza kufanya...

Tukirudi kwenye Binadamu wote ni sawa ni kwamba kwenye Mambo ya Haki na Sheria inabidi tuangalie watu wote kwa usawa bila upendeleo na kwa jicho la specie wote ni sawa sababu tuna characteristics zinazofanana
 
Jibu lipo kwenye swali lako unamaanisha usawa wa nini ? Unaongelea Wajapan, Je unamaanisha chizi wa Japan ni zaidi ya Genius wa Aboriginal kule Australia ?!!; Necessity is the mother of all invention..., kwahio binadamu wote kwa ujumla wana akili ya kuweza kupambana na tatizo linalowakumba kwa wakati husika..., Pia huitaji umati wa watu kufanya vitu pioneers wachache wanaweza kufanya...

Tukirudi kwenye Binadamu wote ni sawa ni kwamba kwenye Mambo ya Haki na Sheria inabidi tuangalie watu wote kwa usawa bila upendeleo na kwa jicho la specie wote ni sawa sababu tuna characteristics zinazofanana
Hata kwenye haki na sheria hakuna usawa.
 
Hata kwenye haki na sheria hakuna usawa.
Kuwepo na kutakiwa kuwepo ni mambo mawili tofauti kabisa..., kwahio kwa jicho la haki hakuna sababu ya kum-treat mtu mmoja zaidi ya mwingine....; hio ndio target / objective tunayotaka kufikia watu wenye busara; Kuna kipindi cha wafalme na malkia, mabwana na watwana baadhi ya wachache walikuwa more worth than others (that was the order of the day)
 
Kuna kitabu nilikisoma, Kinaitwa INSHA TATU ZA KIFALSAFA ZA MWALIMU NYERERE.
Ndani yake kulikua na insha tatu za mwalimu Julius nyerere.
Moja wapo ya hizo insha ni hii mada unayozungumzia hapa, Juu ya Uswawa wa binadamu.

Kwa haraka haraka nikikumbuka aliyosema Mwalimu Nyerere kupitia ile insha yake ni kuwa.
Binadamu wote ni sawa katika ubinadamu wao, Mfano Akataja vitu kama mahitaji ya msingi ya binadamu, Roho za binadamu na vyengine vyote ambavyo vinafanya binadamu kuwa sawa.

Mfano akasema Maji ni sawa katika umaji wao haijalishi ni meusi, machafu au masafi, Bado yatakua maji tu yalioundwa na Hydrojeni na Oksijeni mbili.

Na kadhalika akasema pia.

Binadamu sio sawa kwa mantiki ya vipawa vyao, Upekee wao na mambo mengine.

Akatoa na mfano kuwa ukimpeleka mtoto wako shule na ikifika muda wa kurudi nyumbani unategemea umpate mwanao yule uliye mpeleka shule.
Na sio sababu binadamu ni sawa basi uletewe mtoto mwengine ambae sio wako, Sababu mtoto wako atakua na vipawa au vitu tofauti na mtoto mwengine.

Hitimisho akasema Binadamu hawawezi kuwa sawa, Hilo litakua jambo ambalo litaleta matatizo makubwa sana.
Japokuwa watu wana nadi na kutaka usawa lakini haliwezekani.
Na ili taifa na dunia iwe salama lazima kuwe na utafauti hatuwezi wote tukawa sawa.


NB: Ni muda umepita tangu nikisome, kama kuna mtu kapitia hivi karibuni ataongezea vitu humu.
 
Kuwepo na kutakiwa kuwepo ni mambo mawili tofauti kabisa..., kwahio kwa jicho la haki hakuna sababu ya kum-treat mtu mmoja zaidi ya mwingine....; hio ndio target / objective tunayotaka kufikia watu wenye busara; Kuna kipindi cha wafalme na malkia, mabwana na watwana baadhi ya wachache walikuwa more worth than others (that was the order of the day)
Hamuwezi fika
 
Everyone is Unique

Kila siku tunashangaana
Yani binadamu anamshangaa binadamu mwenzake
 
huku tupo primitive
Wao wamejitengenezea mfumo ambao utawafanya wafike mbali
Huku kuna mifumo inayotufanya tuendelee taratibu

Hasa Elimu na Technology
 
Kuna kitabu nilikisoma, Kinaitwa INSHA TATU ZA KIFALSAFA ZA MWALIMU NYERERE.
Ndani yake kulikua na insha tatu za mwalimu Julius nyerere.
Moja wapo ya hizo insha ni hii mada unayozungumzia hapa, Juu ya Uswawa wa binadamu.

Kwa haraka haraka nikikumbuka aliyosema Mwalimu Nyerere kupitia ile insha yake ni kuwa.
Binadamu wote ni sawa katika ubinadamu wao, Mfano Akataja vitu kama mahitaji ya msingi ya binadamu, Roho za binadamu na vyengine vyote ambavyo vinafanya binadamu kuwa sawa.

Mfano akasema Maji ni sawa katika umaji wao haijalishi ni meusi, machafu au masafi, Bado yatakua maji tu yalioundwa na Hydrojeni na Oksijeni mbili.

Na kadhalika akasema pia.

Binadamu sio sawa kwa mantiki ya vipawa vyao, Upekee wao na mambo mengine.

Akatoa na mfano kuwa ukimpeleka mtoto wako shule na ikifika muda wa kurudi nyumbani unategemea umpate mwanao yule uliye mpeleka shule.
Na sio sababu binadamu ni sawa basi uletewe mtoto mwengine ambae sio wako, Sababu mtoto wako atakua na vipawa au vitu tofauti na mtoto mwengine.

Hitimisho akasema Binadamu hawawezi kuwa sawa, Hilo litakua jambo ambalo litaleta matatizo makubwa sana.
Japokuwa watu wana nadi na kutaka usawa lakini haliwezekani.
Na ili taifa na dunia iwe salama lazima kuwe na utafauti hatuwezi wote tukawa sawa.


NB: Ni muda umepita tangu nikisome, kama kuna mtu kapitia hivi karibuni ataongezea vitu humu.

Huatuezi kuwa sawa, kiakili ,ustaraabu namna ya kuchanganua mambo, kupambana na mazingira uwezo wakufikiri na kuamua,

mfano mdogo tu kwenye michezo timu za waarabu wakaskazini (timu za taifa) zinafanya vizuri kwasababu wachezaji wao wanauwezo mkubwa wakutumia akili lakini kwenye vipawa tupo sawa au tunaweza kuwazidi,
 
Binadamu wote ni sawa. Fortunes ndizo zinafanya wengine waonekane na akili au wana uwezo kuliko wengine. Wajapan hao hao kabla ya Meiji Restoration walikuwa wanaonekana kama wanyama wa pori mbele ya wazungu. Wachina walikuwa wanaonekana kama jamii gonjwa hivi. Wagermanic waliwaona waslavic duni. Hata hapa kwetu, jamii zilizopata mali mali, elimu na maendeleo sababu ya wazungu kukaa sana kwao zinajiona bora.
 
Back
Top Bottom