Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,185
- 7,491
Nimeshawishika kuanzisha uzi huu kutokana na tamko la mwana jf huyu;-
Zaidi ya hapo, ni mara ngapi tumesikia kesi za kubambikiziwa na ushahidi wa kubumbwa?
Pia ifahamike kuwa mawakili wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kama ambayo watuhumiwa hushitakiwa kwa mujibu wa sheria na kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria. Kwa mantiki hiyo, hata kama mtuhumiwa anakuwa na kosa kweli, bado ana haki zake kisheria.
Mwisho:
Kama tunaamini utawala wa kisheria ni mzuri, basi tufuateni sheria bila kujali inamnufaisha nani. Sio mtu/upande ukiona unanufaika na sheria unatetea ufuataji wa sheria ila ukiona mwingine ananufaika na sheria hizo hizo unapinga ufuataji wa sheria. Hiyo haifai.
Hebu fikiria "scenario" kama hii kwa mfano.
Unaamka asubuhi, unafungua mlango wa nyumba yako, mbele yako unaona fuko lenye damu, kwa mshangao unaamua kulifungua kwa kutumia vijiti, ndani yake unaona kichwa cha twiga, unashikwa na mshangao zaidi kwamba ni nini kinatokea, wakati unaendelea kushangaa, wanatokea askari, wanakuambia wamepata taarifa kuwa una nyara za serikali, wanakukamata na kukufungulia kesi ya jinai, unaambiwa huna haki ya kuwa na wakili wala kujitetea maana umekamatwa na ushahidi mkononi, Unahukumiwa kifungo cha maisha. Je! haki itakuwa imetendeka? kama haijatendeka, tufanyeje ili iweze kutendeka?
Itakuwa ni vyema kama wanasiasa wataheshimu kazi za mawakili na mahakama kwa ujumla.
Jamani ni hivi; mtu anapotuhumiwa kwa jambo fulani haimaanishi kuwa ni muhalifu mpaka mahakama itakapothibitisha. Yaani kwa mfano wewe hapo unaweza kutuhumiwa kumbaka simba, hautahesabiwa kuwa ni muhalifu mpaka mahakama ithibitishe.Hivi kwa mfano akishindwa hiyo kesi, si nae atatupwa rumande mana katetea wahalifu
Pombe si chai...![]()
Zaidi ya hapo, ni mara ngapi tumesikia kesi za kubambikiziwa na ushahidi wa kubumbwa?
Pia ifahamike kuwa mawakili wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kama ambayo watuhumiwa hushitakiwa kwa mujibu wa sheria na kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria. Kwa mantiki hiyo, hata kama mtuhumiwa anakuwa na kosa kweli, bado ana haki zake kisheria.
Mwisho:
Kama tunaamini utawala wa kisheria ni mzuri, basi tufuateni sheria bila kujali inamnufaisha nani. Sio mtu/upande ukiona unanufaika na sheria unatetea ufuataji wa sheria ila ukiona mwingine ananufaika na sheria hizo hizo unapinga ufuataji wa sheria. Hiyo haifai.
Hebu fikiria "scenario" kama hii kwa mfano.
Unaamka asubuhi, unafungua mlango wa nyumba yako, mbele yako unaona fuko lenye damu, kwa mshangao unaamua kulifungua kwa kutumia vijiti, ndani yake unaona kichwa cha twiga, unashikwa na mshangao zaidi kwamba ni nini kinatokea, wakati unaendelea kushangaa, wanatokea askari, wanakuambia wamepata taarifa kuwa una nyara za serikali, wanakukamata na kukufungulia kesi ya jinai, unaambiwa huna haki ya kuwa na wakili wala kujitetea maana umekamatwa na ushahidi mkononi, Unahukumiwa kifungo cha maisha. Je! haki itakuwa imetendeka? kama haijatendeka, tufanyeje ili iweze kutendeka?
Itakuwa ni vyema kama wanasiasa wataheshimu kazi za mawakili na mahakama kwa ujumla.