Ni hatari kuitangazia dunia habari za ugunduzi usio rasmi

Chunda

Senior Member
Apr 7, 2016
182
251
IMG_0254.JPG


Kama ilivyoripotiwa na gazeti la Raia Mwema toleo Na 505 la tarehe 12-04-2017, Uongozi wa Chuo cha Ufundi Arusha uliitangazia Dunia kwamba Chuo hicho kimegundua aina mpya ya Chopa (Helikopta).

Kulingana na uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hiyo ni kwamba kinachodaiwa kuwa ugunduzi ni sawa tu na mchezo wa watoto kuigiliza kutengeneza gari kama wanavyoyaona barabarani. Cha ajabu ni pale ambapo habari hiyo ya ugunduzi wa helikopta Tanzania ilivyosambaa Duniani kama vile ni jambo la kweli lililofanyiwa utafiti na kugundulika.

Tanzania ni sehemu ya Dunia yenye wasomi wanaoaminika na kutambuliwa Duniani. Tungekuwa kisiwa tunakoishi peke yetu tungeweza kujifanyia mambo ya kienyeji kama tunavyotaka. Lakini kwa kuwa sisi ni sehemu ya Dunia inafaa tuende kama Dunia inavyotaka kwa mambo yanayohusu utafiti na ugunduzi.

Inapotokea habari kama hizi za ugunduzi ambao haujafanyiwa utafiti na ambao bado haujathibitishwa na mamlaka za kitaifa zinazotambulika, kurushwa nje ya nchi na hasa pale ambapo habari hizo siyo za uhakika ni kasoro kubwa sana kwa nchi mbele ya uso wa kimataifa. Inakuwa mbaya zaidi pale ambapo taarifa hizo zinapotolewa na Taasisi ya Serikali inayoshughulika na Elimu, Utafiti na Ushauri wa kitaalamu.

Habari za ugunduzi kama hizi zingeandikwa na mafundi wa mtaani ingeweza kuonekana ni jambo la kawaida. Lakini zinapoandikwa na Taasisi ya elimu ya juu inayoaminika kuwa ni ya wasomi ambao huamini katika utafiti ni jambo la ajabu na la kutia aibu, ndani na nje ya nchi.
 
Duh, hiyo ni kali. Helikopta inatengenezwa bila hata michoro katika Taasisi ya Elimu ya Juu kwa karne hii?
 
Mizaha ya aina hii itatufikisha wapi? Wenye mamlaka ikiwa ni pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi na Mamlaka ya mawasiliano ya anga wanayo taarifa za ugunduzi huo?

Ikiwa siyo jambo lililo rasmi kama uongozi wa chuo unavyodai, ilikuwa na maana gani kulitangaza kimataifa? Ikiwa hatuwezi kutengeneza pikipiki, pawatila, mashine za kukamua juisi za matunda yanayooza mashambani wakati wa misimu ya matunda, fikra za helikopta japo ni mzaha ni muafaka kwa Tanzania hivi sasa?
 
Mjema kama yumo humu atoe ufafanuzu maana niliona ndio alipewa airtime kutudanganya kuwa wanao uwezo wa kutengeneza chopa
 
Hivi pale chuo cha usafirishaji (NIT) kilichopo Dar walishaanza kutoa mafunzo ya urubani kama walivyotangaza miaka kama mitatu hivi iliyopita?
 
Aysee haifai kujibana lazima kicheko kitoke tyuu hata ujibane vip.

Ila poa tuendelee na ujenzi wa taifa.
 
Victor Meena et al safari hii Paul Sariwat imempa bei gani....? . next week tutegemea story gani ya kuchafua chuo cha Ufundi Arusha ...?.

View attachment 494823

Kama ilivyoripotiwa na gazeti la Raia Mwema toleo Na 505 la tarehe 12-04-2017, Uongozi wa Chuo cha Ufundi Arusha uliitangazia Dunia kwamba Chuo hicho kimegundua aina mpya ya Chopa (Helikopta).

Kulingana na uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hiyo ni kwamba kinachodaiwa kuwa ugunduzi ni sawa tu na mchezo wa watoto kuigiliza kutengeneza gari kama wanavyoyaona barabarani. Cha ajabu ni pale ambapo habari hiyo ya ugunduzi wa helikopta Tanzania ilivyosambaa Duniani kama vile ni jambo la kweli lililofanyiwa utafiti na kugundulika.

Tanzania ni sehemu ya Dunia yenye wasomi wanaoaminika na kutambuliwa Duniani. Tungekuwa kisiwa tunakoishi peke yetu tungeweza kujifanyia mambo ya kienyeji kama tunavyotaka. Lakini kwa kuwa sisi ni sehemu ya Dunia inafaa tuende kama Dunia inavyotaka.

Inapotokea habari kama hizi za ugunduzi ambao haujafanyiwa utafiti na ambao bado haujathibitishwa na mamlaka za kitaifa zinazotambulika, kurushwa nje ya nchi na hasa pale ambapo habari hizo siyo za uhakika ni kasoro kubwa sana kwa nchi mbele ya uso wa kimataifa. Inakuwa mbaya zaidi pale ambapo taarifa hizo zinapotolewa na Taasisi ya serikali.

Habari za ugunduzi kama hizi zingeandikwa na mafundi wa mtaani ingeweza kuonekana ni jambo la kawaida. Lakini zinapoandikwa na Taasisi ya elimu ya juu inayoaminika kuwa ni ya wasomi ambao huamini katika utafiti ni jambo la ajabu na la kutia aibu, ndani na nje ya nchi.
 
Mizaha ya aina hii itatufikisha wapi? Wenye mamlaka ikiwa ni pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi na Mamlaka ya mawasiliano ya anga wanayo taarifa za ugunduzi huo?

Ikiwa siyo jambo lililo rasmi kama uongozi wa chuo unavyodai, ilikuwa na maana gani kulitangaza kimataifa? Ikiwa hatuwezi kutengeneza pikipiki, pawatila, mashine za kukamua juisi za matunda yanayooza mashambani wakati wa misimu ya matunda, fikra za helikopta japo ni mzaha ni muafaka kwa Tanzania hivi sasa?

Ni lini Chuo cha Afundi Arusha ilifanya press conference na kuitangazia dunia kuhusu helikopta ?!!.... suala la helikopta liliibuliwa na vyombo vya habari tu, tena wakati wa ziara ya alikuwa katibu mkuu wa ziara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia alipokuja kuzindua maabara ya hydraulics. pia si dhambi watu kutengeneza helikopta na si kweli kuwa hakuna michoro wala andiko kuhusu hiyo helikopta.
 
Victor Meena et al... hivi hii sio hatua ?!...

View attachment 494823

Kama ilivyoripotiwa na gazeti la Raia Mwema toleo Na 505 la tarehe 12-04-2017, Uongozi wa Chuo cha Ufundi Arusha uliitangazia Dunia kwamba Chuo hicho kimegundua aina mpya ya Chopa (Helikopta).

Kulingana na uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hiyo ni kwamba kinachodaiwa kuwa ugunduzi ni sawa tu na mchezo wa watoto kuigiliza kutengeneza gari kama wanavyoyaona barabarani. Cha ajabu ni pale ambapo habari hiyo ya ugunduzi wa helikopta Tanzania ilivyosambaa Duniani kama vile ni jambo la kweli lililofanyiwa utafiti na kugundulika.

Tanzania ni sehemu ya Dunia yenye wasomi wanaoaminika na kutambuliwa Duniani. Tungekuwa kisiwa tunakoishi peke yetu tungeweza kujifanyia mambo ya kienyeji kama tunavyotaka. Lakini kwa kuwa sisi ni sehemu ya Dunia inafaa tuende kama Dunia inavyotaka.

Inapotokea habari kama hizi za ugunduzi ambao haujafanyiwa utafiti na ambao bado haujathibitishwa na mamlaka za kitaifa zinazotambulika, kurushwa nje ya nchi na hasa pale ambapo habari hizo siyo za uhakika ni kasoro kubwa sana kwa nchi mbele ya uso wa kimataifa. Inakuwa mbaya zaidi pale ambapo taarifa hizo zinapotolewa na Taasisi ya serikali.

Habari za ugunduzi kama hizi zingeandikwa na mafundi wa mtaani ingeweza kuonekana ni jambo la kawaida. Lakini zinapoandikwa na Taasisi ya elimu ya juu inayoaminika kuwa ni ya wasomi ambao huamini katika utafiti ni jambo la ajabu na la kutia aibu, ndani na nje ya nchi.
 
Huenda ni jaribio zuri, ila lipo jambo la kufikirisha kidogo. Kuna mapungufu gani katika helikopta zilizopo lililopelekea utengenezaji au ugunduzi mpya? Ni tofauti gani iliyopo kati ya helikopta zinazoruka zilizopo na hii mpya inayodaiwa kugunduliwa? Ikiwa kwa muujiza wa Mwenyezi Mungu ukifanikisha helikopta hiyo ikaweza kuruka, soko lake ni kina nani na wako wapi?
 
Huenda ni jaribio zuri, ila lipo jambo la kufikirisha kidogo. Kuna mapungufu gani katika helikopta zilizopo lililopelekea utengenezaji au ugunduzi mpya? Ni tofauti gani iliyopo kati ya helikopta zinazoruka zilizopo na hii mpya inayodaiwa kugunduliwa? Ikiwa kwa muujiza wa Mwenyezi Mungu ukifanikisha helikopta hiyo ikaweza kuruka, soko lake ni kina nani na wako wapi?
Victor meena et al.. Kiwango chako cha kufikiri kumbe ni kidogo hivi.. Soma kidogo historia ya helikopta Dunia... Utakuwa unachekesha Dunia kisema wahusika wamegundua helikopta. Siamini kiwango chako cha kufiriki kimefika hapa !! hivi umetumia fedha kiasi gani kwa sariwati kushawishi kuakaandika story kama hii. ?..
 
Hahaa! Naona Tz ndo kwanz 2po enz za akina wright brothers Anyway let us focus the way forward
 
Bado kidogo, tutakunjakunja vyuma tuweke na ingini chakavu na kusema tumegundua apolo ya kwenda mwezini!
 
unagunduaje kitu kilichogunduliwa tayar, ?
amna ugunduzi apo, iyo chaboo!
 
Back
Top Bottom