Ni busara kuhoji mali za mwenza wako akiwa hoi kitandani?

Ngugu wanachohitaji hapa ni mali zote zieleweke ili zisipotee. Wanajua ndugu yao ana mali nyingi na ana biashara nyingi anazifanya tatizo hakuna mwenye detail za kutosha kuweza kuzifuatilia endapo chochote kitatokea. Hivi niandikavyo bado yuko ICU.

Kumbuka mkewe ni mama wa nyumbani asiyejua lolote, watoto wanamahitaji mengi na hakuna cha kuwasaidia zaidi ya mali za baba yao.
Ujinga ndio huu sasa, kama wanajuwa ndugu yao ana mali nyingi sasa hapa unaomba ushauri wa nini? si wanazijuwa hizo mali?

Wakati mwingine muwe na akili si kila anayepaki magari 5 nyumbani kwamba kwake anayamiliko wengine ni madalali tu, hata mimi kuna wakati nikimwambia shemeji yenu sina pesa huwa haamini anadhani namdanganya kumbe ukweli huwa nakuwa sina pesa kweli.
 
wanaume sasa msipowaamini wake zenu kiasi cha wao kujua asset zenu mnawaamini kina nani jamani!

ona sasa mambo ya kuanza kuulizana vitandani ICU ''eti beby niliwahi kusikia kuwa una kampuni ya uwindaji ngorongoro file lake liko wapi?''uuuuwih hamad kabla hujamjibu vizuri unazidiwa anakutingishaje mabega sio ili upone hapana ili uendelee kumwelekeza zilipo mali zingine!
cha kutufanya tuonekane wachawi kwa mama zenu au dada zenu ni nini jamani!
kwa walio na hii tabia hebu jirekebisheni!
mke wako ni wewe ndani yake!hebu badilikeni jamani!

Wanahofia usalama wao, baadhi ya wanawake wakisharidhika na mali za mumewe sio hatari kukutanguliza......But kama una mke wa ukweli kila mpango wa familia unaratibiwa na wanandoa
 
naona hizi ni familia 2 zinaishi mji mmoja kazi kweli kweli kwenye ndoa nyumba zimeficha mengi sana ila Mungu anajua kila kitu
 
Naombeni ushauri ili niweze kumshauri rafiki aliyeniuliza kama anaweza kumhoji mumewe kuhusu mali na vitu vingine alivyonavyo maana huyo mumewe amepata ajali mbaya sana na hali yake hairidhishi kama ataendelea kuishi.

Mwanamume huyo ni mfanyabiashara na inaonekana ana mali nyingi tu ambazo mkewe hazitambui vizuri. Baadhi ya ndugu wamemshauri amhoji mumewe kabla hajafa ili mali na vitu vingine visipotee vije wasaidia watoto baadaye.

Mke anasita akijiuliza mumewe atajisikiaje? Jamii itamuelewa? Mke ni mama wa nyumbani na alizoea kufanyiwa kila kitu, sasa nahisi ndugu wanawasiwasi kuwa endapo mume atakufa mali nyingi zitapotea.

Naomba ushauri wenu, huyu mama afanyeje? je ni busara kuhoji? ataeleweka kwa jamii?
bila shaka huyo mwanamke ni mmachame tu, au penginewe ni wewe..issue ni hivi ana roho dhaifu mbele ya uhai anakumbuka mali tu...kwa taarifa yako hua mtu anaitwa msimamizi wa mirathi huyo hutafuta mali zote za marehemu..sasa asiwaze sana..mali zote zitawekwa wazi na zile ambazo hazijui sio kesi mana mumewe mwenyewe hakumwambia..yani kama ni mim ndo mume unaniuliza swali hilo...utaniua kabisa...ushauri wanaume na waafrika kiujumla tuwe tunaandika usia ..ova...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom