Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,486
- 30,166
Hivi Jeshi la Polisi linawafanya watanzania wote ni wapumbavu na malofa wanaoweza kuwadanganya wapendavyo??
Tumesikia taarifa waliyotoa jana katika kuuvunja mkutano wa ACT wazalendo kuwa eti wameuvunja mkutano huo kwa madai kuwa wamehofia kutokea kuvunjika amani kutokana na taarifa za kiintelejensia walizo nazo kuwa kikundi cha CUF cha Lipumba kina mpango wa kuwafanyia fujo chama hiko cha ACT wazalendo!
Sababu zilizotolewa ni za uwongo wa hali ya juu ambazo hakuna mtanzania yeyote anayeweza ziamini
Kwanza, nini wajibu wa Jeshi letu la Polisi nchini??
Inajulikana wazi kuwa Jeshi la Polisi nchini wajibu wake mkubwa kabisa, ni kuwalinda raia na Mali zao.
Sasa inakuwaje tena hao raia wanaopaswa kulindwa na Jeshi la Polisi, Jeshi hilo hilo lenye silaha za kivita, liwaogope raia ambao hawana hata visu, kuwa eti wana mpango wa kuwafanyia vurugu hao ACT wazalendo katika mikutano wao??
Hivi ni mkutano gani ungeweza kuwa wa hatari zaidi, ni ule wa Profesa Lipumba wa majuzi wakati wakimuidhinisha Profesa Lipumba katika uenyekiti wake wa "magumashi" au ni huu mkutano wa Maalim Seif wa kuwaeleza sera wanachama wao wa ACT wazalendo??
Ilikuwaje hili Jeshi la Polisi likatoa ulinzi mwanzo hadi mwisho katika mkutano wa Profesa Lipumba na wakati huo huo mkutano wa ACT wazakendo wakidai kuwa "wanawaogopa" hao wafuasi wa Lipumba, hadi kuwalazimisha kuuvunja mkutano huo??
Kama alivyonukuliwa Rais Magufuli mwanzoni mwa mwezi huu, wakati akiliongelea suala la utekwaji kwa mfanyibiashara maarufu nchini kuwa Jeshi la Polisi lisiwafanye watanzania wajinga, kwa kuwaongopea kuhusu "movie" yao waliyocheza ya kutekwa kwa Mo, ambapo hadi Leo hajakamatwa mtuhumiwa yeyote na Kamanda Mambosasa alionekana kunywa nao chai akina Mo!
Hatuna budi watanzania kwa ujumla wetu tukatae kufanywa wajinga na Jeshi hili la Polisi, kwa kutoa visingizio vyao visivyo na kichwa wala miguu, ili mradi wahalalishe katika kutumika kwao na chama tawala cha CCM
Tumesikia taarifa waliyotoa jana katika kuuvunja mkutano wa ACT wazalendo kuwa eti wameuvunja mkutano huo kwa madai kuwa wamehofia kutokea kuvunjika amani kutokana na taarifa za kiintelejensia walizo nazo kuwa kikundi cha CUF cha Lipumba kina mpango wa kuwafanyia fujo chama hiko cha ACT wazalendo!
Sababu zilizotolewa ni za uwongo wa hali ya juu ambazo hakuna mtanzania yeyote anayeweza ziamini
Kwanza, nini wajibu wa Jeshi letu la Polisi nchini??
Inajulikana wazi kuwa Jeshi la Polisi nchini wajibu wake mkubwa kabisa, ni kuwalinda raia na Mali zao.
Sasa inakuwaje tena hao raia wanaopaswa kulindwa na Jeshi la Polisi, Jeshi hilo hilo lenye silaha za kivita, liwaogope raia ambao hawana hata visu, kuwa eti wana mpango wa kuwafanyia vurugu hao ACT wazalendo katika mikutano wao??
Hivi ni mkutano gani ungeweza kuwa wa hatari zaidi, ni ule wa Profesa Lipumba wa majuzi wakati wakimuidhinisha Profesa Lipumba katika uenyekiti wake wa "magumashi" au ni huu mkutano wa Maalim Seif wa kuwaeleza sera wanachama wao wa ACT wazalendo??
Ilikuwaje hili Jeshi la Polisi likatoa ulinzi mwanzo hadi mwisho katika mkutano wa Profesa Lipumba na wakati huo huo mkutano wa ACT wazakendo wakidai kuwa "wanawaogopa" hao wafuasi wa Lipumba, hadi kuwalazimisha kuuvunja mkutano huo??
Kama alivyonukuliwa Rais Magufuli mwanzoni mwa mwezi huu, wakati akiliongelea suala la utekwaji kwa mfanyibiashara maarufu nchini kuwa Jeshi la Polisi lisiwafanye watanzania wajinga, kwa kuwaongopea kuhusu "movie" yao waliyocheza ya kutekwa kwa Mo, ambapo hadi Leo hajakamatwa mtuhumiwa yeyote na Kamanda Mambosasa alionekana kunywa nao chai akina Mo!
Hatuna budi watanzania kwa ujumla wetu tukatae kufanywa wajinga na Jeshi hili la Polisi, kwa kutoa visingizio vyao visivyo na kichwa wala miguu, ili mradi wahalalishe katika kutumika kwao na chama tawala cha CCM