Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,943
Hizi taasisi za mataifa ya Afrika sijui kama zina faida yoyote nyingine zaidi ya kutoa ajira kwa baadhi ya watu!!
Leo ni siku ya 3 tangu maandamano makubwa yaanze nchini Kenya, yanayotishia uwezekano wa kutokea maafa makubwa ya uhai wa watu na mali. Mpaka sasa vifo 13 vimethibitika na wakuu wa mahospitali, lakini wanasema kuna uwezekano mkubwa waliouawa ni zaidi ya hao 13.
Maandamano yalikuwa ya amani, mpaka polisi walipoanza kutumia risasi za moto na kuua waandamanaji.
Kenya ni mwanachama wa EAC, ni mwanachama wa AU, mambo haya mabaya na ya hatari yanayotokea kwa nchi mwanachama wa EAC na AU, lazima yatakuwa na athari kwa jumuia hizi kama taasisi na yana athari kwa mataifa wanachama, kama nchi jirani. Lakini jambo linaloshangaza sana, mpaka sasa, si jumuia ya EAC, AU wala nchi mwanachama mmoja mmoja ambayo imetoa kauli yoyote au kufanya jitihada za kuhakikisha ndugu zetu hawa hawaishii kwenye ubaya wa kutisha. Labda nchi wanachama zote zinaongozwa na viongozi Chura Viziwi!!
Mataifa ya mbali, kama US wamekwishatoa kauli ya kuikemea Serikali ya Kenya kwa mauaji ya waandamanaji.
Pongezi nyingi kwa viongozi wa dini wa Kenya waliomtaka Ruto kuwarudisha wanajeshi makambini, na suala la kuyalinda maandamano libakie mikononi mwa Polis, maana ndiyo kazi yao, kwa mujibu wa katiba ya Kenya.
Hii EAC na Au inaonekana haina msaada kwa wananchi wa Afrika. Watu wanaweza kuuawa kwa mamia kwenye nchi mwanachama na taasisi hizi zikawa kimya tu. Kama EAC na AU haziwezi kuwahakikishia usalama wananchi wa mataifa wanachama, kimsingi taasisi hizi zinakuwa hazina maana yoyote, maana kwa mwanadamu, jambo la kwanza muhimu kuliko yote, ni uhai wake.
Leo ni siku ya 3 tangu maandamano makubwa yaanze nchini Kenya, yanayotishia uwezekano wa kutokea maafa makubwa ya uhai wa watu na mali. Mpaka sasa vifo 13 vimethibitika na wakuu wa mahospitali, lakini wanasema kuna uwezekano mkubwa waliouawa ni zaidi ya hao 13.
Maandamano yalikuwa ya amani, mpaka polisi walipoanza kutumia risasi za moto na kuua waandamanaji.
Kenya ni mwanachama wa EAC, ni mwanachama wa AU, mambo haya mabaya na ya hatari yanayotokea kwa nchi mwanachama wa EAC na AU, lazima yatakuwa na athari kwa jumuia hizi kama taasisi na yana athari kwa mataifa wanachama, kama nchi jirani. Lakini jambo linaloshangaza sana, mpaka sasa, si jumuia ya EAC, AU wala nchi mwanachama mmoja mmoja ambayo imetoa kauli yoyote au kufanya jitihada za kuhakikisha ndugu zetu hawa hawaishii kwenye ubaya wa kutisha. Labda nchi wanachama zote zinaongozwa na viongozi Chura Viziwi!!
Mataifa ya mbali, kama US wamekwishatoa kauli ya kuikemea Serikali ya Kenya kwa mauaji ya waandamanaji.
Pongezi nyingi kwa viongozi wa dini wa Kenya waliomtaka Ruto kuwarudisha wanajeshi makambini, na suala la kuyalinda maandamano libakie mikononi mwa Polis, maana ndiyo kazi yao, kwa mujibu wa katiba ya Kenya.
Hii EAC na Au inaonekana haina msaada kwa wananchi wa Afrika. Watu wanaweza kuuawa kwa mamia kwenye nchi mwanachama na taasisi hizi zikawa kimya tu. Kama EAC na AU haziwezi kuwahakikishia usalama wananchi wa mataifa wanachama, kimsingi taasisi hizi zinakuwa hazina maana yoyote, maana kwa mwanadamu, jambo la kwanza muhimu kuliko yote, ni uhai wake.