Ngúgí Wa Thiong'o awahutubia Wahispania kwa lugha ya Gíkúyú baada ya Rais wa Cataluña kumtunuku tuzo la Premi Internacional Catalunya

Mimi ningewashauri wakenya mje Tanzania kujifunza ni jinsi gani Nyerere alivyoweka msingi wa matumizi wa hizi lugha ili ziweze kutumika bila kuleta hathari mbaya ya ukabila.

Watanzania 98% huko vijijini hutumia lugha zao za makabila, kwasababu huko vijijini zaidi ya 99% ya wanaoishi ni kutoka katika kabila moja, uwezekano wa kuweka makundi kwa misingi ya ukabila ni Kama haupo kwasababu wote ni kabila Moja.

Unapokuja katika ofisi za serikali au mijini hali ibabadilika sana, watu wamechanganyika kutoka mikoa na makabila mbalimbali, kila mtu akianza kuzungumza lugha yake inakua ni fujo na watu wanajitenga, hata kupata huduma katika ofisi za serikali kunaanza kuathiriwa.

Typical Example ni Nchi ya Belgium ambayo imegawanyika kutukana na lugha, ukiingia Hotels za Brussels ukizungumza "Flemish" ambayo ni lugha kuu ya Kaskazini mwa Belgium, sio rahisi kupata huduma wanataka uzungumze kifaransa ambayo ni lugha kuu ya kusini mwa Belgium.
 
Kama inatamkwa "ngo" kwa nini inaandikwa "ngu"?
These are alphabets in Kikuyu: a b c d e g h i ĩ j k m n o r t u ũ w y..

Na pia za ziada: mb, nd, nj, ng, ng', NY, th

Also when it comes to vowels there are 7 basic vowels, kama unafahamu Kiitaliano inakuwa rahisi kwa sababu pia wao huwa na saba 😎

a, e, I, o, u na ( ĩ, ũ)
a (low /central), e (ɛ Mid-low/Front), i (high/front), ĩ (e Mid-high/Front), o (ɔ Mid-low /Back), u (High/Back), ũ (o Mid-high/Back).

Mfano neno Gĩkũyũ utalitamka
kama Gekoyo.
 
Mimi ningewashauri wakenya mje Tanzania kujifunza ni jinsi gani Nyerere alivyoweka msingi wa matumizi wa hizi lugha ili ziweze kutumika bila kuleta hathari mbaya ya ukabila.

Watanzania 98% huko vijijini hutumia lugha zao za makabila, kwasababu huko vijijini zaidi ya 99% ya wanaoishi ni kutoka katika kabila moja, uwezekano wa kuweka makundi kwa misingi ya ukabila ni Kama haupo kwasababu wote ni kabila Moja.

Unapokuja katika ofisi za serikali au mijini hali ibabadilika sana, watu wamechanganyika kutoka mikoa na makabila mbalimbali, kila mtu akianza kuzungumza lugha yake inakua ni fujo na watu wanajitenga, hata kupata huduma katika ofisi za serikali kunaanza kuathiriwa.

Typical Example ni Nchi ya Belgium ambayo imegawanyika kutukana na lugha, ukiingia Hotels za Brussels ukizungumza "Flemish" ambayo ni lugha kuu ya Kaskazini mwa Belgium, sio rahisi kupata huduma wanataka uzungumze kifaransa ambayo ni lugha kuu ya kusini mwa Belgium.
aisee mnatuaibisha watz wote tuaonekana mazwazwa kwa mabandiko ya ki-layman kama haya.
 
chief go and consult books utanue mawazo ili unapoandika chochote humu usijiabishe.
Chief ukiogopa kujiabisha hutojifunza maishani, sema kile unachokijua ili watu wajue mapungufu yako ili wakurejebishe, nina uhakika hiki nilichoandika kuhusu matumizi ya lugha za asili katika kuendeleza ukabila ni sahihi Sana, ndio sababu huoni watu wakipinga kwa hoja.
 
Haya mambo ya kutokuenzi lugha zetu huwa 'cool' ukiwa kijana, haswa vijana wa mjini, pale unanyoosha kiswahili cha kimjini na kingereza pia, nakumbuka enzi zetu tukiwa vijana, tulikua tunaonana washamba tukiongea kwa lugha zetu, ilikua inatubidi kutumia Kiswahili na Kingereza muda mwingi, ila kadiri umri unavyosonga na kuanza kukomaa kiakili, kuna baadhi ya mambo unaanza kuyaona ya kitoto, mzee Mpare wa miaka 50 utajiona wa hovyoo sana unapokaa na wazee wenzako wanazungumza kwa lugha yao ya asili Kipare ilhali hamna chochote unachokielewa.
 
Haya mambo ya kutokuenzi lugha zetu huwa 'cool' ukiwa kijana, haswa vijana wa mjini, pale unanyoosha kiswahili cha kimjini na kingereza pia, nakumbuka enzi zetu tukiwa vijana, tulikua tunaonana washamba tukiongea kwa lugha zetu, ilikua inatubidi kutumia Kiswahili na Kingereza muda mwingi, ila kadiri umri unavyosonga na kuanza kukomaa kiakili, kuna baadhi ya mambo unaanza kuyaona ya kitoto, mzee Mpare wa miaka 50 utajiona wa hovyoo sana unapokaa na wazee wenzako wanazungumza kwa lugha yao ya asili Kipare ilhali hamna chochote unachokielewa.

Hata mimi nilishtuka nikiwa kwenye 20s ikabidi nijifunze lugha yangu ukubwani.

Sielewi mtu mzima anapokasirika watu wakiongea lugha yao. Kama huelewi ujue kuwa huhusiki kwenye mazungumzo.
 
These are alphabets in Kikuyu: a b c d e g h i ĩ j k m n o r t u ũ w y.. Na pia za ziada: mb, nd, nj, ng, ng', NY, th Also when it comes to vowels there are 7 basic vowels, kama unafahamu Kiitaliano inakuwa rahisi kwa sababu pia wao huwa na saba a, e, I, o, u na ( ĩ, ũ)
a (low /central), e (ɛ Mid-low/Front), i (high/front), ĩ (e Mid-high/Front), o (ɔ Mid-low /Back), u (High/Back), ũ (o Mid-high/Back). Mfano neno Gĩkũyũ utalitamka
kama Gekoyo.
Great. This explanation is on point.
 
Kiswahili ni mchanganyiko wa lugha ya mabwana (waarabu) na watumwa (Wabantu). Kiarabu ni zaidi ya 35% ya Kiswahili.

Sasa mtu tofauti na wewe akijitenga shida yako ni nini? Kitendo cha kuwa na lugha tofauti maana yake nyie ni watu tofauti.

Tufunge makanisa na misikiti kama tunalenga kutengeneza identity moja.
Sio kweli, Somalia ni jamii moja na lugha moja lakini wanapigana.

Huwezi kumwambia mtu akatae asili yake ili awe mtumwa wa identity bandia ya mzungu.

Lazima tukubali kuwa sisi ni watu tofauti na historia tofauti. Huwezi kulazimisha watu tofauti waishi pamoja kwa kupuuza tofauti zao.

Kwa nini hatupambani kuondoa dini za kigeni kwa sababu ni msingi wa matatizo mengi Afrika?
Nakubaliana na hoja yako hii mia kwa mia. Waafrika wengi wanaona sifa kupagawa na dini za kigeni huku mila, tamaduni na lugha zetu za asili, ambazo ndio urithi wetu, wakiziona duni na zisizofaa.
 
Nakubaliana na hoja yako hii mia kwa mia. Waafrika wengi wanaona sifa kupagawa na dini za kigeni huku mila, tamaduni na lugha zetu za asili, ambazo ndio urithi wetu, wakiziona duni na zisizofaa.
Wakenya wacheni ubishi usio kuwa na faida yoyote, kwanini hampendi kukosolewa?. Nchi nyingi zinatumia lugha zao bila kubaguana. Tatizo ni hizi nchi ambazo tayari kuna tatizo la ukabila kama Kenya, lugha ni chombo muhimu sana katika kuwaunganisha, msingekuwa na ukabila tusingewapigia kelele, mbona Zambia hatuwasemi wakati hata wao pia wanazungumza lugha zao?.

Lazima mkubali kwamba nchi yenu imeathiriwa sana na ukabila, ni busara sana kama mngejiepisha na mambo yote yanayosababisha kuzidi kuwagawa, moja na kitu cha haraka kinachotengeneza "barriers" katika jamii yoyote ni lugha. Tafadhalini sana punguzeni ukaidi mjifunze kwa Tanzania katika hili, Kiswahili kumetusaidia sana kutuunganisha na kumaliza ukabila, hata hili pia mnapinga?
 
Back
Top Bottom