Raia wa Tanzania wenye asili ya Rwanda (wenye uraia) wamekamatwa na wanahojiwa kwenye kituo cha polisi Benaco. Ngombe wao walikamatwa, ni siku ya nne sasa, wakafungiwa kwenye mnada wa Kafuha, Ngara. Mnada wa Kafuha umejengwa kwa matofari, na ngombe hawajala majani kwa siku ya nne wala kunywa maji. Baadhi ya ngombe walitoroka na waliporudi vijijini, wamekatwakatwa miguu na wenyeji, wamelala wanakufa kwa kuvuja damu. Najua humu ndani watu watasema, wauwawe tuu! Wateswe tu! Lakini huu ni ukatiri ! kwa binadamu na wanyama