Ng'ombe azaa ndama mwenye kichwa cha binadamu

Ng'ombe azaa ndama mwenye kichwa cha binadamu

zaleo

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2011
Posts
1,902
Reaction score
766
Habari kutoka Halmashauri mpya ya Busokelo Wlayani Rungwe zimenifikia jana, kwamba katika Kijiji cha Mbigili hapo juzi ng'ombe mmoja aliyekuwa na mimba amejikuta akizaa ndama mwenye kichwa cha binadamu. Ng'ombe huyo alikuwa anaendelea kuzaa kwa kutanguliza miguu ya ndama, lakini ghafla akashindwa kuendelea na kukaa chini. Akaishiwa nguvu na kulegea kabisa. Waliokuwapo jirani wakataka kumsaidia, lakini kichwa cha ndama kiligoma kutoka hadi walipolazimisha kutoa kichwa, na kushitukia wanaonana na kichwa cha mtu kabisa. Ng'ombe mzazi hakuendelea kuishi, akafariki muda mfupi baadaye.

haijajulikana bado kwa kina ni nini mazingira yaliyopelekea jambo hilo kutokea. Wenzetu walioko Busokelo watatufaa kutuletea naelezo zaidi. lakini labda kwa sababu ambazo wengine wanajiuliza uhusiano, Malkia wa mfalme wa eneo hilo anayejulikana kwa jina la Chief Kabakuli Mwaiswelo alifariki dunia siku hiyohiyo na makazi yake yanapakana na mmiliki wa ng'ombe huyo. Jambo linaloashiria kwamba huenda ni tukio lenye mizizi ya kimila. Mungu aiweke roho ya marehemu Malkia mahali pema peponi.
 
Hapo hakuna cha malikia wala mizimu bali niuzinzi kwa mifugo tu.

Hapo bado, kifuatacho nikuanza kufiatua kitu live.
 
Weka picha tuone. Au hata ukitumia digital camera picha zinaungua?
 
Kuweni makini, it is not possible for different species of animals to interbreed, especially for the man and cow which are very unrelated.
 
Habari zenu wapendwa, mi ni mwanacham mpya, but kwenye hili naamini ni miujiza ya mungu tu, anatukumbusha uwepo wake kwan binadam tunajisahau. Asubuhi njema!
 
Usisahau kwamba kijijini hakuna uchunguzi wa kina. Bahati mbaya kijijini pale hata kituo cha polisi hakipo, wakati uohuo wana msiba mkubwa jirani kiasi kwamba ni rahisi kwa wanakijiji kuoanisha matukio hayo mawili na kutoa jibu la kimila badala ya kwenda polisi ambako hakuna wa kumshitaki. Picha inaweza kuwapo kama alikuwapo mtu mwenye kamera hapo jirani, vinginevyo jambo kama hilo laweza kuchukuliwa kama uchuro mwingine na wazee hawawezi kuruhusu liendelee kuanikwa. Walioko Busokelo hata hivyo, wanaweza kutuletea mbichi na mbivu na hata picha kama wanaweza kuipata. Utandawazi siku hizi umeenea hadi vijijini kwa digital.
 
Habari kutoka Halmashauri mpya ya Busokelo Wlayani Rungwe zimenifikia jana, kwamba katika Kijiji cha Mbigili hapo juzi ng'ombe mmoja aliyekuwa na mimba amejikuta akizaa ndama mwenye kichwa cha binadamu. Ng'ombe huyo alikuwa anaendelea kuzaa kwa kutanguliza miguu ya ndama, lakini ghafla akashindwa kuendelea na kukaa chini. Akaishiwa nguvu na kulegea kabisa. Waliokuwapo jirani wakataka kumsaidia, lakini kichwa cha ndama kiligoma kutoka hadi walipolazimisha kutoa kichwa, na kushitukia wanaonana na kichwa cha mtu kabisa. Ng'ombe mzazi hakuendelea kuishi, akafariki muda mfupi baadaye.

haijajulikana bado kwa kina ni nini mazingira yaliyopelekea jambo hilo kutokea. Wenzetu walioko Busokelo watatufaa kutuletea naelezo zaidi. lakini labda kwa sababu ambazo wengine wanajiuliza uhusiano, Malkia wa mfalme wa eneo hilo anayejulikana kwa jina la Chief Kabakuli Mwaiswelo alifariki dunia siku hiyohiyo na makazi yake yanapakana na mmiliki wa ng'ombe huyo. Jambo linaloashiria kwamba huenda ni tukio lenye mizizi ya kimila. Mungu aiweke roho ya marehemu Malkia mahali pema peponi.

Mkuu, wewe umeona kwa macho yako au umesimuliwa?
 
Kuweni makini, it is not possible for different species of animals to interbreed, especially for the man and cow which are very unrelated.

mkuu unafikiri watu walivyo na haraka ya kufanya jumping conclusion wanaweza kufikiri kwa upana zaid? Wengine unakuta wanatambua kabisa na wamesoma hiyo biology kidogo sekondari lakin kwa uvivu wa kuwaza wanasema binadam na ng'ombe wanaweza kupata mtoto! Hata cross breeding ina depend na species! Eg cow with buffalo or cat with leopard etc....
 
Mkuu, wewe umeona kwa macho yako au umesimuliwa?
Mkuu, habari inajieleza vizuri sana "Habari imenifikia jana...." Niko mbali sana, lakini maelezo yametoka kwa source iliyohudhuria msibani pale na kushuhudia kabla ya kurusha habari hiyo. ndo maana nikaomba uchambuzi wa kina kwa wadau walioko kule jirani. Upo?
 
Picha, picha pichaaaaa iko wapi? Vinginevyo wewe liongo!
 
Back
Top Bottom