Ngoma ya escrow kumbe ni standard chartered

Ngoma ya escrow kumbe ni standard chartered

Hana hoja alafu umetumwa kumtetea huyo prof:? mbona mnapopewa hiyo misaada huwa hamutoi maelezo marefu kiasi hiki, za mwizi arobaini tu endelea kutoa maelezo marefu ila wananchi tuna akili zetu za kuchanganua mambo
 
Blah blah blah unajua ada tunayolipa babro kwa ajili ya watoto wetu?

ada inalipiwa kutokana na uwezo wa mzazi kama Harvard, kama wewe kwenye fomu umetaka misifa ya kuonekana unaingiza hela nyingi shauri lako!
 
Watanzania wanasema hela irudi Tanesco, wakidhani ni hela ya umma, kumbe watu wanataka irudi Tanesco ili iende Standard chartered!!

Kwa muda sasa kumekuwapo na tuhuma zinazohusu "wizi" wa fedha za akaunti ya escrow iliyofunguliwa katika Benki Kuu ya Tanzania mwaka 2006. Akaunti hiyo ilifunguliwa kwa ajili ya kuhifadhi fedha zilizokuwa zikilipwa na Shirika la Umeme Tanzania {TANESCO} kwa kampuni ya kufua umeme ya IPTL. Chimbuko la akaunti hiyo ni mgogoro wa tozo hiyo kwamba iligubikwa na utata baada ya kudaiwa kwamba Tanesco ilikuwa ikitozwa fedha nyingi kuliko inavyostahili.

Tuhuma za huo "wizi" hata hivyo hazikuishia tu kwa wahusika wakuu yaani makampuni ya umeme, bali zimetiririshwa hadi kwa watu binafsi ambao kimsingi hawana uhusiano wowote na mgogoro huo wa malipo na wala kuhusika kwa njia yoyote na hicho kinachodaiwa kwamba ni uporaji wa fedha za akaunti hiyo ya Escrow.


Akaunti Escrow ni akaunti ya amana ambayo inawekwa chini ya uangalizi wa mtu wa tatu ili huyo mwangalizi aikabidhi kwa mlengwa pale tu masharti kadhaa yatakapokuwa yamekamilishwa. Hivyo basi akaunti hiyo maalum ya amana ilifunguliwa na kuwekwa chini ya Benki Kuu kama wakala anayesubiria kutekelezwa kwa masharti maalumu ili aikabidhi kwa wenye kumiliki fedha hizo watakapomaliza tofauti zao.

Ni vizuri kuliangalia suala hili la akaunti maalum ya amana kwa namna ambayo itawafanya wale wenye kiu ya kutaka kujua ukweli kukidhi hamu yao.


Fedha iliyokuwa ikiwekwa katika akaunti hiyo ni tozo ya uwezo wa mitambo ya kufua umeme ambayo kampuni ya IPTL ilikuwa ikiitoza Tanesco. Baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Utatuzi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) kupunguza tozo ya IPTL kutoka USD 3.6million kila mwezi mpaka USD 2.6million kila mwezi baadaye TANESCO ilishauriwa vibaya na wanasheria kwamba tozo hiyo bado ni kubwa kuliko mkataba baina ya IPTL na TANESCO Mei 26, 1995 unavyo eleza.

Ubishani uliozuka kati ya mtoa huduma ya umeme yaani IPTL na mtumia huduma ya umeme yaani Tanesco ndio uliosababisha kufunguliwa kwa akaunti hiyo maalum ya amana yaani escrow account katika Benki Kuu ya Tanzania {BoT} kama njia salama ya kutunza fedha hizo hadi mgogoro utakapokuwa umetatuliwa.


Ni muhimu kufanya hivyo ili kuhakikisha kwamba mtoa huduma yaani IPTL hasitishi kufua umeme na mtumiaji wa umeme yaani Tanesco naye hakosi umeme wa kuuza kwa walaji wake. Hiyo ni busara ya kibiashara. Fedha hizo zililipwa katika akaunti hiyo maalum kutokana na hati za madai au ankara kutoka kwa mtoa huduma na si vinginevyo.

Kitu kimoja kilichojitokeza wazi ni kwamba suala la akaunti hiyo maalum limekuwa likibeba sura mpya kila kukicha na la kusikitisha zaidi ni kwamba vyombo vya habari vilivyo vingi ama vimekuwa vikipotosha kwa makusudi au kwa kutokuelewa mada yenyewe ipasavyo. Vipo vyombo vya habari kwa mfano ambavyo vimedai kwamba "Benki ya Standard Chartered ndiyo mmiliki wa mitambo ya IPTL baada ya kupewa mamlaka hayo na mahakama - Deed of Assignment- inayoiruhusu kuchukua na kumiliki mali za IPTL kutokana na kushindwa kulipa mkopo.


Aidha kwa mujibu wa gazeti la Mawio la Alhamisi Novemba 20-26, 2014 mkataba huo uliipatia benki ya SCB haki za IPTL ndani ya mkataba wa kuuziana umeme (PPA) na kumiliki mtambo wa kuzalisha umeme wa IPTL.

Kwa mujibu wa gazeti hilo la Mawio Benki ya Standard Chartered inaidai Tanesco dola za Marekani 258.7 milioni kama deni linalotokana na gharama za umeme uliozalishwa na IPTL na dola za Marekani 138 milioni zinazotokana na mkopo pamoja na riba. Kwa mujibu wa uchambuzi wa Mawio madai hayo ni halali kwa mujibu wa sheria.

Kwa mujibu wa gazeti hilo "nyaraka za serikali zinaonesha kuwa PAP iliamuriwa kulipa wadai wote wa IPTL lakini haikuilipa Benki ya Standard Charted ambayo inajitangaza kuwa ni moja ya wadai.

Ni vyema na busara kuanza uchambuzi huu kwa kufanya nukuu hiyo muhimu sana kutoka katika gazeti la kila wiki la Mawio kwa sababu inatusaidia kuonyesha waziwazi kwamba hiki kinachodaiwa kwamba ni kashfa ya fedha za Escrow kina sura nyingi sana kulingana na maslahi yanayolengwa kutetewa.


Katika muktadha huu ni wazi kwamba anayetetewa hapa ni Benki ya Standard Chartered ambayo inadaiwa kwamba ndiyo yenye haki ya kulipwa fedha kutoka katika akaunti ya Escrow na kwa mantiki hiyo imeishitaki Serikali ya Tanzania katika Mahakama ya Uingereza.

Deni linalodaiwa kwamba Tanesco inadaiwa na Standard Chartered la dola za Marekani linatokana na gharama za umeme uliozalishwa na IPTL na nyingine ni mkopo na riba. Inashangaza kwamba Tanesco inawezaje kudaiwa na Benki ya Standard Chartered wakati aliyezalisha umeme ni IPTL? Abrakadabra hiyo ndiyo inayomfanya ye yote yule mwenye akili timamu kutambua kwamba kuna mchezo wa kiini macho unaochezwa na benki hiyo dhidi ya Tanzania.

Ni wazi kabisa kwamba benki hiyo inalazimisha kuwapo na mgogoro wa kuhusu akaunti ya Escrow kwa lengo moja tu nalo ni kuhakikisha kwamba wanapata nafasi ya kukwapua hizo fedha wanazodai kwamba sio halali kuchukuliwa na IPTL. Kwamba zikichukuliwa na Benki ya Standard Chartered ambayo haijazalisha umeme wala kuwa na ushahidi wowote wa kushiriki katika kuzalisha umeme ni halali kabisa na zikichukuliwa na IPTL ambayo imezalisha umeme na inayo mikataba ya kuuziana umeme na Tanesco si sahihi, ni wizi, ni ujambazi ni hila na kashfa. Hii inahitaji maelezo zaidi kushinda haya yanayotolewa hivi sasa.

Ukweli wa mambo ni kwamba mazungumzo kuhusu fedha za Escrow na hususan habari za kujaribu kuonyesha kwamba umiliki wake ni batili una lengo moja tu nalo ni kuandaa mazingira kwa ajili ya Benki ya Standard Chartered hatimaye kuzichukua fedha hizo kwa kutumia kigezo cha kwamba imemilikishwa mitambo ya IPTL na kwamba ndiyo iliyokuwa na haki ya kulipwa tozo ya uzalishaji umeme na si kampuni nyingine yoyote. Hivyo ndivyo kampuni hiyo inavyodai katika kesi iliyofungua dhidi ya Serikali ya Tanzania huko Uingereza.

Benki ya Standard Chartered inatumia mbinu mbalimbali ili kuhakikisha inafikia lengo lake la kukwapua fedha za kigeni si chini ya dola milioni 200 kutoka kwa serikali ya Tanzania. Moja ya njia inayotumia ni propaganda ambayo hupenyezwa katika vyombo vya habari kwa kutumia majukwaa mbalimbali.


Moja ya njia zinazotumika ni kujaribu kuufanya umma uamini kwamba fedha zilizotoka katika ufungaji wa akaunti hiyo ya Escrow zimeibwa na kwamba wahusika katika huo wizi ni pamoja na viongozi kadhaa wa Serikali.

Kinachosikitisha zaidi ni kwamba kuhusishwa kwa watu hao kunafanyika bila hata ya kuwataka wajieleze kama wanaelewa kile wanachotuhumiwa nacho. Wafadhili wa propaganda hizo hawakubali kujitokeza hadharani moja kwa moja kwa kuhofia kuumbuliwa. Matukio huchukuliwa si kwa ujumla wake bali upande mmoja na kuyatangaza kwa namna ya kukidhi matakwa na matarajio yao tu.

Tumezoea kuambiwa kwamba wakati suala linapokuwa mahakamani kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi basi si sahihi kuendelea kulijadili kwenye vyombo vya habari kwani kwa kufanya hivyo ni sawa kabisa na kuingilia uhuru wa mahakama. Ni wazi kwamba hata suala linapokuwa katika uchunguzi au upelelezi uwe kwa kutumia tume maalum au makachero basi ni muhali kulizungumzia hadharani na kuwatuhumu na hata kuwahukumu watu kwa ujasiri usio na kikomo kwamba ni wezi au mafisadi au wakumbatiaji wa madhila hayo yote. Hili linafanyika kila siku kupitia vyombo vya habari na chimbuko lake ni baadhi ya wabunge na wanasiasa ambao hufanya hivyo huku wakitumia kila aina ya takwimu za kweli na za kughushi au kubuni tu kichwani.

Nini kinachowafanya au kuwapa jeuri hawa watu wanaowatuhumu na kuwahukumu wengine bila ya kujali kwamba hilo halitakiwi wala kupaswa kufanyika bila ya kupitia katika vyombo vya sheria ili kutoka fursa kwa wengine kujitetea? Swali hilo linastahili kujibiwa kwa umakini mkubwa ili kubaini kama kweli hao wanaodai kwamba wanapigania haki ya kiuchumi ya Watanzania ni kweli wanafanya hivyo kwa dhati ya moyo wao kabisa bila ya kuwa na nia nyingine iliyojificha ambayo hawathubutu kuiweka hadharani kwani kwa kufanya hivyo watageuka viroja.


Pamoja na kwamba kuna kesi mahakamani dhidi ya Serikali ya Tanzania ni wazi kwamba ukiwauliza Standard Chartered kilichowapeleka mahakamani wanasema kwamba wanaionea nchi yetu huruma, Hata hivyo, kamwe hakuna atayekuambia kwamba amekuja hapa kwa ajili ya kujaribu bahati yake kama wanaweza kufanya mbinu wakatengeneza fedha ya bure. Ili kufanikisha malengo yao tuhuma hurushwa kwa yeyote na popote. Ili kufanikisha malengo hayo mtu yeyote yule aweza kuunganishwa katika lolote lile ili kufikia lengo.

Ni kwa utaratibu huo huo ndio tunashuhudia jinsi jitihada za Profesa Anna Tibaijuka za kuendeleza mtoto wa kike kielimu zinavyopakwa matope na kukejeliwa mno kwa sababu tu ameomba msaada mahali na akaupata.


Tujiulize inakuwaje wanasiasa wetu wanathubutu kumhukumu Profesa Tibaijuka na kumuita kila aina ya majina machafu. Ametuhumiwa kwamba ni mwizi eti kwa sababu aliomba msaada kwa ajili ya shule ya Babro Johansson ambayo ni kwa madhumuni ya kuwasaidia watoto wa kike kupata elimu.


Profesa Tibaijuka aliomba msaada kwa barua rasmi miaka kadhaa iliyopita na kampuni hiyo haikuweza kumsaidia mapema kutokana na ukata na ni hivi majuzi hali ilipokuwa njema ndipo ikatoa msaada huo.

La kustaajabisha ni kwamba msaada huo haukuwa ni siri na ulitolewa kwa uwazi mkubwa bila ya kificho. Sasa huo ujambazi wa Profesa Tibaijuka umetokea wapi? Kosa lake ni kupatiwa fedha alizoomba kwa ajili ya kuisaidia shule ambayo aliianzisha?

Tunajiuliza hapa, baada ya VIP kuuza hisa zake kwa PAP na kulipwa na PAP stahili yake, ilifanya kosa gani kutoa msaada kwa shule ya Babro Johansson?

Mahitaji na umuhimu wa elimu yanajulikana. Viongozi wanahimiza kila leo umuhimu wa Watanzania kubadilika kuchangia Maendeleo ya Elimu badala ya harusi na sherehe nyinginezo. Leo hii anatokea Mtanzania anaomba msaada wa kuendeleza elimu na anapatikana Mtanzania anakubali kuchangia vizuri maendeleo ya elimu, wawili hawa baadhi ya wanaojiita viongozi wa siasa tena wenye kutaka kuchukua madaraka ya juu kuiongoza nchi, wanalalamika na hata kutamani kutoa roho ya mtu! Watanzania tuzipime dhamira zao. Ni wadanganyifu wasio na uelewa halisi wa matatizo na vipaumbele vya taifa na hivyo kukosa dhamira thabiti ya kuyashughulikia. Wanasukumwa zaidi na tamaa zao binafsi.

Kwa wanaong'ang'ania kudai damu za baadhi ya watu kutokana na hukumu ambayo wao wameipitisha baada ya kufanya kila kitu wao ikiwa ni pamoja na kutuhumu, kupeleleza, kufungua mashitaka, kusikiliza kesi na hatimaye kuhukumu na sasa kutaka kukaza hukumu kwa njia yoyote ile hakuna jambo zuri na jema kama kufanya kile wanachotaka wao yaani kukubali kwamba fedha zote katika akaunti maalum ya escrow ni za serikali na kwamba lazima zirudi serikalini.


Hata hivyo, wakubwa hao hawataki kurudi nyuma na kujiuliza ni kwa njia gani fedha hizo zimeingia katika akaunti hiyo. Aidha, hawataki kujiuliza kwamba kama Tanesco ndio ilikuwa ikitumbukiza fedha katika akaunti hiyo, ilikuwa ikifanya hivyo kwa kutumia vigezo gani. Swali linguine la kujiuliza, je Serikali hutunza pesa zake kwenye Account zake Benki Kuu au kwenye Escrow Account?

Hawaoni mantiki ya kutulia na kujibu swali la msingi kwamba kama Tanesco ingelikuwa inatumbukiza fedha katika akaunti hiyo kwa ajili ya kugharamia tozo la uwezo wa mitambo kuzalisha umeme sasa inakuwaje fedha hizo zirudi tena Tanesco? Ni maswali ambayo wanaojiamini kwamba ukweli wanao wao tu hawataki kuyajibu hata kidogo kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wanaumaliza utamu wa mchezo wao wa kuigiza.


Fedha hizo zinatakiwa zirudi Tanesco ili Benki ya Standard Chartered izichukue kwa madai kwamba ndiye mmiliki halali wa IPTL na kwamba kuna deni kama ilivyoainishwa awali katika makala haya.

Kutokana na ufafanuzi huo hapo juu ni wazi basi kwamba Tanesco ilikuwa ikilipia gharama za huduma ambayo ilikuwa inaipata kutoka kwa IPTL. Hilo halina ubishi.

Lakini pia suala lingine ambalo sasa halina ubishi japo halisemwi makusudi kwa sababu za upotoshaji ni kwamba katika makampuni yote ambayo yanauzia umeme TANESCO, IPTL ndiyo kampuni pekee inayotoza kiwango kidogo cha malipo ya uwekezaji (capacity charges). Suala la kujiuliza hapa ni inawezekanaje IPTL ambayo inatoza kiwango kidogo cha capacity charges ionekane “kuiibia” Serikali kwa kulipwa halali yake wakati makampuni mengine yanatoza capacity charges kwa kiwango cha juu zaidi ya IPTL na hakuna malalamiko.
Swali la kujiuliza ni kwamba ni kitu gani kinachowasukuma watuhumu kutafuta kila njia ya kuonyesha kwamba kuna hitilafu kubwa sana kwa namna ambavyo suala la akaunti hiyo lilivyohitimishwa?

Ukifuatilia kwa karibu na umakini jinsi ambavyo tuhuma zimekuwa zikitolewa ni kwamba kinacholengwa ni fedha zilizokuwa katika akaunti maalumu ambazo ni tozo ya uwezo wa ufuaji wa umeme. Fedha hizo zinagombewa na Benki ya Standard Chartered ambayo ina matawi yake hapa nchini.


Benki hiyo inatumia kila njia kujaribu kuonesha kwamba fedha zilizokuwapo katika akaunti ya Escrow ni fedha ya Serikali. Kwa mantiki hiyo inachojaribu kufanya Benki hiyo ni kuonyesha kwamba fedha akaunti ya escrow si kwa ajili ya kulipia gharama za uwezo wa mitambo kufua umeme la hasha. Bali ni fedha za Tanesco na kamwe hakuna anayestahili kuzipunguza kwa njia yoyote ile.

Cha kushangaza, hata hivyo, ni kwamba benki hiyo, inayodai kuwa iliikopesha fedha IPTL, katika madai yake yaliyopo mahakamani, inadai kuwa yenyewe ndiyo ilistahili kupata fedha zilizokuwa kwenye escrow account! Swali hapa ni je, hiyo asasi ndiyo Serikali? Je, fedha zilizokuwa kwenye escrow account zinakuwa za Serikali na siyo IPTL kwa sababu benki hiyo haijalipwa?

Jitihada za kutaka kuhalalisha kwamba fedha hizo ni mali ya Tanesco na kwamba haziwezi kumegwa hata kidogo zinafanywa na Benki ya Standard Chartered ambayo inataka kutengeneza mazingira ya kuchota fedha kutoka Tanesco kwa madai kwamba ndiyo inayostahili kuwa mlipwaji wa fedha hizo kutokana na deni ambalo kwa mujibu wa madai yao ndio walioikopesha IPTL fedha kwa ajili ya mradi huo wa umeme.

Mchezo ambao benki hiyo inafanya hapa nchini ni kuhakikisha kwamba vyombo vya habari vinaandika habari za kuigonganisha serikali na wananchi kwamba Serikali ni ya mafisadi na inayokumbatia ufisadi, na haina ubavu wowote wa kupambana na rushwa. Aidha, asasi hiyo imevirubuni baadhi ya vyombo vya habari kuandika habari kwamba Mahakama za Tanzania haziaminiki na zinakumbatia ufisadi na kwamba zimekubuhu kwa rushwa.

Cha kushangaza, tuhuma hizi za rushwa kwa Mahakama za Tanzania zinakuja muda mfupi tu baada ya benki ya Standard Chartered kuiambia mahakama New York, nchini Marekani iliposhitakiwa na VIP kuwa Mahakama za Tanzania ndizo zenye uwezo wa kusikiliza na kutatua migogoro ya IPTL.

Mchezo ambao Standard Chartered Bank inaufanya ni kutumia vyombo vya habari kutoa habari zisizo za kweli na za upotoshi ili kuwachochea watu dhidi ya Serikali yao kutokana na nini kinaendelea ndani ya IPTL. Mambo mengi yamesemwa na kuandikwa kuhusiana na Mahakama na watendaji wa Serikali kula rushwa. Madhumuni ya kufanya hivyo ni kutaka kuonyesha kwamba nchini Tanzania haki haiwezi kutendeka.

Madai hayo yote, yanatokea wakati Standard Chartered Bank imefungua kesi London, kwa kisingizio kwamba Mahakama za Tanzania haziwezi kutenda haki

Kwa vipi Standard Chartered Bank inatoa madai kulipwa dola za kimarekani 208 milioni kutoka TANESCO (katika kesi ilivyofunguliwa Mahakama ya usuluhishi (ICSID)) kwa mkopo wa dola milioni 84 kwa IPTL, wakati Serikali ya Tanzania na TANESCO tayari walikwishalipa takribani dola 200 milioni kwa IPTL kufikia mwaka 2006. Kiasi hicho kingelitosha kulipia mkopo uliokuwa umechukuliwa na kulipa gawiwo kwa VIP na MECHMAR. Mpaka mwaka 2013 VIP ilikuwa haijalipwa hata senti moja kwa jina lolote.

Kampuni ya Mechmar ilitumia fedha zilizodaiwa na IPTL kutoka Serikali ya Tanzania na TANESCO kwa kujilipa yenyewe na Kampuni ya Wartsila madeni hewa (kwa makubaliano na benki ya Danaharta na baadaye Standard Chartered Bank (Hong Kong) Ltd.


Standard Chartered Bank (Hong Kong) Ltd inajaribu kutekeleza mpango haramu dhidi ya IPTL kwa kutumia dhamana ya Serikali ya Tanzania na hivyo Serikali ina sababu za kutaka Standard Chartered Bank ithibitishe kama inaidai IPTL.

Mpaka sasa ukweli ni kwamba Standard Chartered Bank imekwepa kutoa ushahidi kuwa ina madai yoyote dhidi ya IPTL na kwa sababu hiyo na zingine VIP na IPTL/PAP wameifungulia kesi za madai ya fidia na hasara ya TZS 787bilioni na USD 3bilioni katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

source: mtandao
Nani kasema Rugemalila kumpa Prof Tibaijuka bilioni 1.6 ni kosa, hakuna. Kinachosemwa hapa ni kwamba pesa aliyopewa Prof Tibaijuka ni ya wizi, ilitoka kwenye akaunti ya Escrow. Unaweza kujiuliza Prof angejuaje: utetezi dhaifu sana. Kupokea mali au pesa ya wizi ni kosa na ndiyo sababu kutokana na kiwango cha fedha hiyo kuwa kikubwa wenye akili tunaamini Prof alijua huu ni mgawo wa shukrani.
Umejipinda sana kutetea wizi huu, mara nyingine ujumbe kama huu waandikie wajinga wenzio.
 
Somo letu kwenye sakata la escrow kama jamii sisi ni watu wa majungu mno, waongo, wenye wivu wa (kike kwa mujibu wa Benjamini Mkapa) na tamaa sana including uchu wa wamadaraka. Maana motive kubwa ni kuzibiana na kuchafuana ili kwenda kufaidika kimslahi na rasilimali za taifa.

Mpaka dakika hii hakuna mtu aliethibitisha kosa linalostahili adhabu ya kisheria iliyopo ndani ya Tanzania sanasana kwa wale walio CCM labda makosa ya kimaadili kutokana na kanuni za chama chao kama katiba yao inavyoelezea. Waliopo serikarilini maswali yanayoibuka jinsi ya keweka ethics na kuzuia conflict of interest. Lakini hakuna sheria au mwongozo bunge unaoweza kumuwajibisha mtu yeyote mpaka dakika hii zaidi ya waropokaji tu.

Mwanzo wengine tulikuwa tunasoma post za watu na evidence zilizopo lakini after JF exclusive ya ripoti ya CAG ni wazi hakuna kesi kwenye swala la malipo ata hiyo capacity charge ndio iliyotumika kuondoa tax washiriki walikuwa Tanesco, IPTL na TRA baada ya kuwekeana madai waka afiki exemption agreement ya Tax; ni vitu vya kawaida kwenye madeni ya serikari. Ambapo common-sense prevails na deni lingekuwa kubwa zaidi kama TRA wangedai IPTL kodi.

Hela yenyewe iliyokuwa kwenye escrow account ni kati ya wabia wa IPTL, kwa kukurupuka unaweza dhania mahakama ilipendelea kwenye shauri lakini ukifuatilia mambo ya deeds za partnerships na contract laws unakuta maswala ya vitiating factors yanachangia kuamua kesi zenye malengo ya kuvunja mikataba au misunderstanding kati ya wabia. Kwa sababu standard charter si mmbia wa mwanzo anaweza akatafutiwa na kutafutiwa solution nyengine.

Ndio maana kulikuwa na kesi mahakamani kuhusu mgogoro wa wabia, tunachojua mercher aliacha hisa zake benki, hakuna anaejua mkataba wa VIP na mercher ulikuwa vipi kimakubaliano?

Facts zilizopo Standard charter ambae alipata mkataba probably through asset stripping company baada ya benki iliyokuwa inamdai mercher kufulisika lakini atujui alikuwa ana negotiate vipi na VIP mwenye 30%, kwenye kudai hela yake. Hapo kuna maswala ya duress ambayo VIP anaweza tumia kutoka kwenye mkataba kwa sababu yeye anakuwa kama principal na standard charter awezi amua vingine.

VIP anaweza fungua shauri la anti-participatory breach kwakuwa mercher akutimiza wajibu wake na jaji anaweza toa remedies according to facts presented in the court kwa sababu standard charter si mmbia hata wakienda huko Brella, tuna sheria ya civil procedures, contract law na business act zote zina cover hivyo vitu on the jurisdiction kwa makampuni yaliyo funguliwa Tanzania.

Kama Standard Charter alikuwa anataka kuwa mmbia VIP anaweza amua nitakulipa deni lako au gharama za mercher kwa sababu sikuelewana na wewe. Mpaka dakika hii hakuna anaejua standard charter alikuwa anataka nini hasa aingie kwenye ubia kwa lazima wa IPTL, alipwe hela or what exactly where there demands.

VIP kutokana na nafasi yake anaweza negotiate na yeyote kuchukua hisa za mercher na huyo jamaa achukue majukumu aliyoyaacha mmbia wa awali including madeni (as in standard Standard Charter au kumalizana nae kwa namna nyengine) ndio maana kesi bado hipo mahakamani. Kwa maana hiyo so far ni watu tu wameamua kuvurugiana baada ya kukosa. This is why we need strong laws za kudhibiti conflict of interest na kuwekana sawa kwenye kupokea zawadi kwa wafanyakazi wa serikari.

Watu wanaweza kuwa kweli walipiga dili lakini hakuna sheria iliyovunjwa na wala hakuna ushahidi wa influence ya those who have received funds form either side of their shareholder, kwanza it doesn't make sense kumuhusisha mtu kama padre na case husika na matukio ya saga lenyewe.

Siasa zimetumika kupotosha uhalisia wa kesi na hili swala lilikuwa linahusu interest za two parties largely PAP and Standard charter kwanini wanasiasa wapotoshe ukweli na kuchukua upande surely mahakama inaweza zuia swala lisijadiliwe kutokna na upotoshaji wa awali not that i care anyway hila tusubiri kesho tuone huu mziki unaendelea vipi na watu wanavyozidi kujipotezea credibility mbele ya jamii ukweli utakuja kuwa wazi tu mbeleni.

Inawezekanaje PAP kuilipa VIP $75,000,000 + $7,000,0000 za kufuta kesi kwa 30% shares iliyokuwa nazo IPTL, halafu kuilipa PiperLink (kampuni feki)/Mechmar only $3000 kwa 70% shares za hiyohiyo IPTL? Huyo JMali aidha ni James Rugemalira au Jerome Rugemalira
 
Nani kasema Rugemalila kumpa Prof Tibaijuka bilioni 1.6 ni kosa, hakuna. Kinachosemwa hapa ni kwamba pesa aliyopewa Prof Tibaijuka ni ya wizi, ilitoka kwenye akaunti ya Escrow. Unaweza kujiuliza Prof angejuaje: utetezi dhaifu sana. Kupokea mali au pesa ya wizi ni kosa na ndiyo sababu kutokana na kiwango cha fedha hiyo kuwa kikubwa wenye akili tunaamini Prof alijua huu ni mgawo wa shukrani.
Umejipinda sana kutetea wizi huu, mara nyingine ujumbe kama huu waandikie wajinga wenzio.
Haya sasa kumbe waliopokea hela hawana makosa na tatizo imekuwa hela yenyewe ni chafu tu. Ina maana hakuna aliefisadi moja kwa moja au mbona amtueleweshi vizuri sisi raia?

Kwanza madai yenyewe mapya ya kukokotoa upya capacity charge hayakuamuliwa na mahakama zetu na yamekuja baadae sana wakati watu wameshalipwa kama mahakama ya Tanzania ilivyoagiza. Mahakama ya uingereza ndio iliotoa shauri la kukotoa upya capacity charge (huko ni kama kuongeza chumvi kwenye ugomvi wa IPTL na Tanesco) na kumrudisha standard charter kwa nguvu za kikoloni.

Na hao wadai wa standard charter walipoitwa na jaji utumwa kuja kutetea madai yao hawakutokea wakitegemea mahakama ya uingiereza itoe maamuzi ya kuwa favor wao, baada ya kuona Tanzania ina jurisdiction power to decide on the matter ndio wanaomba kesi isimamishwe, isitoshe wao si wabia bali ni wadeni wa mmbia kwanini wanatafuta remedy ya fidia na habari za Tanesco kunufaika na mitambo wakati wabia walikuwa na mzozo na umeme unahitajika. Standard charter walitakiwa wa deal na Rugemalira kwanza kuhusu deni lao aliloacha mechamar lakini tamaa na wao ndio wakaona wanaweza fanya forceful take over; tangia lini benki ikafanya biashara ya umeme.

Ni mwehu tu anaeweza watetea standard charter si ajabu jaji akaona PAP achukue IPTL hawalipe tu hela yao hao standar charter that is what they deserve and nothing more wapuuzi wakubwa wanadhani bado sisi koloni lao.

Isitoshe hawana hata hizo hati za shares wanazodai wamezirithi evidence tu ya kuwa mechamar alikopa na aliacha hisa benki ambazo wanadai wamerithi.

Watanzani tuamke na tuache kutumiwa na mafisadi unaweza ukawa na harisa sana na Ruge kwa matendo yake ya awali kwenye swala la IPTL in the 90's lakini yote ni matokeo ya serikari weak.

Hila hili la sasa la mafisadi kutaka kulipeleka shirika kwa wazungu by force hapana kwakweli, kwanza ni kamati ya PAC kupitia huyuhuyu zito ndio wanaofanya PAP apate shirika kwa sababu ni wao waliotoa mwongozo wa kisheria Tanesco isimiliki mitambo ya IPTL in any circumstances si ndio maana leo kampuni lina amia kwa matapeli. Who knows kwanini zito alishauri hivyo huko nyuma huyu chalii ni mchumia ata mimi naanza kumuona for what he is anatumika tu kama mpira wa kitandani hana tofauti na Andrew Chenge binafsi ni mtu pekee ambae ningependa kuona hili la escrow linamtoa kwenye siasa kabisa i have had enough of this old reprobate kama kweli kapata 1.6 bn; he has played a big role to hinder our economic development kila sehemu aliyoshiriki.
 
Inawezekanaje PAP kuilipa VIP $75,000,000 + $7,000,0000 za kufuta kesi kwa 30% shares iliyokuwa nazo IPTL, halafu kuilipa PiperLink (kampuni feki)/Mechmar only $3000 kwa 70% shares za hiyohiyo IPTL? Huyo JMali aidha ni James Rugemalira au Jerome Rugemalira
Rugemalira alianza kuzi value shares zake na kutaka kuziuza since 2002 at $100 mil. Isipokuwa mgogoro tu wa ubia ukawa tatizo ndio maana akauza kwanza ili PAP amalizane na wabia kumbuka kulikuwa na wind up mahakamani aliyofungua VIP kuna mengi hapa lakini siwezi kuwa upande wa standard charter hata kama Ruge nae ni shetani kwa upande wake, be it within the law akishirikiana na wahuni wengine kufanikisha uhuni wake.
 
Nani kasema Rugemalila kumpa Prof Tibaijuka bilioni 1.6 ni kosa, hakuna. Kinachosemwa hapa ni kwamba pesa aliyopewa Prof Tibaijuka ni ya wizi, ilitoka kwenye akaunti ya Escrow. Unaweza kujiuliza Prof angejuaje: utetezi dhaifu sana. Kupokea mali au pesa ya wizi ni kosa na ndiyo sababu kutokana na kiwango cha fedha hiyo kuwa kikubwa wenye akili tunaamini Prof alijua huu ni mgawo wa shukrani.
Umejipinda sana kutetea wizi huu, mara nyingine ujumbe kama huu waandikie wajinga wenzio.

kwani rugemalira ni mlalahoi mpaka ashukiwe namna hiyo? ungekuwa wewe ndio umetoa msaada wa bilioni tungeshangaa, rugemalira ana hela toka enzi hizo anamiliki tritel, misaada ya mamilioni kwake kawaida tu. Hivi leo ikigundulika Mengi hajalipa kodi utadai na fedha alizotoa kwa tibaijuka mil 250 kwenye shule ile ile nazo ni za wizi?
Pili, Rugemalira ameuza hisa zake kwa sethi, kama sethi aliiba hakuna tatizo, fedha zitarudishwa na rugemalira atarudishiwa hisa zake 30% kama zamani. Kuna tatizo hapo?
 
Inawezekanaje PAP kuilipa VIP $75,000,000 + $7,000,0000 za kufuta kesi kwa 30% shares iliyokuwa nazo IPTL, halafu kuilipa PiperLink (kampuni feki)/Mechmar only $3000 kwa 70% shares za hiyohiyo IPTL? Huyo JMali aidha ni James Rugemalira au Jerome Rugemalira

sasa hilo swali anatakiwa kuulizwa nani rugemalira ambaye kalipwa kiwango stahiki kwa hisa zake na KALIPA KODI, au TRA na Sethi? Kwa nini mnamzonga rugemalira wa 30% halali badala ya aliyeuza na kununua 70% kifisadi? kama mimi ni rugemalira mmojawapo basi naomba kwa heshima na taadhima nikuite Reginald mengi!
 
Kitu nachokiwaza sana ni kwanini ile share ya 70% ya Singasinga haiongelewi kabisa badala yake tuko busy na 30% ya VIP Eng.? Hapa panahitaji umakini angalieni tusiwe tunalishwa matangopori na ku-uacha ukweli wote pembeni.

Hii hela ya Singasinga wamekula akina nani?
 
Kitu nachokiwaza sana ni kwanini ile share ya 70% ya Singasinga haiongelewi kabisa badala yake tuko busy na 30% ya VIP Eng.? Hapa panahitaji umakini angalieni tusiwe tunalishwa matangopori na ku-uacha ukweli wote pembeni.

Hii hela ya Singasinga wamekula akina nani?

Zote ni pesa haramu zilizopatikana kwa njia ya kitapeli na rushwa. Nani kalipwa kiasi gani na nani that's irrelevant.
 
sasa hilo swali anatakiwa kuulizwa nani rugemalira ambaye kalipwa kiwango stahiki kwa hisa zake na KALIPA KODI, au TRA na Sethi? Kwa nini mnamzonga rugemalira wa 30% halali badala ya aliyeuza na kununua 70% kifisadi? kama mimi ni rugemalira mmojawapo basi naomba kwa heshima na taadhima nikuite Reginald mengi!

No simple answers to complex legal issues like this. Halafu kuna tofauti kati ya kudai kuwa na 30% shares kwenye IPTL (issue ambayo ilikuwa mahakamani kwani $13.5 million ambazo VIP inadai ililipa kwa 30% shares hazikuwa registered na Mechmar. Uhalali wa 30% shares za VIP kwenye IPTL was in dispute), na kulipwa pesa haramu zilizotokana na grand corruption na utapeli uliotukuka. Kama Rugemalira kalipia kodi au kagawa zote it still doesn't change the facts kwamba kalipwa pesa haramu, na alifahamu dili nzima.
 
ada inalipiwa kutokana na uwezo wa mzazi kama Harvard, kama wewe kwenye fomu umetaka misifa ya kuonekana unaingiza hela nyingi shauri lako!
jMali jMali sasa unapotoka
au umevuta kwa Ruge?
maana toka majuzi ww ni kutetea huo wizi mpaka tukakushangaa
Pinda ametakiwa ajiuzulu na hapo ndipo Baba yako Rugemalila atakapozirudisha na hela zetu zote alizowagawia


 
Last edited by a moderator:
jMali jMali sasa unapotoka
au umevuta kwa Ruge?
maana toka majuzi ww ni kutetea huo wizi mpaka tukakushangaa
Pinda ametakiwa ajiuzulu na hapo ndipo Baba yako Rugemalila atakapozirudisha na hela zetu zote alizowagawia


sijatetea wizi wa pesa za umma, nimemtetea james rugemalira, kuna tofauti hapo. Elewa kuwa James rugemalira akirudisha pesa na yeye hapo hapo atarudishiwa umiliki wa IPTL kwa asilimia 30! Kuna wizi gani hapo?
 
No simple answers to complex legal issues like this. Halafu kuna tofauti kati ya kudai kuwa na 30% shares kwenye IPTL (issue ambayo ilikuwa mahakamani kwani $13.5 million ambazo VIP inadai ililipa kwa 30% shares hazikuwa registered na Mechmar. Uhalali wa 30% shares za VIP kwenye IPTL was in dispute), na kulipwa pesa haramu zilizotokana na grand corruption na utapeli uliotukuka. Kama Rugemalira kalipia kodi au kagawa zote it still doesn't change the facts kwamba kalipwa pesa haramu, na alifahamu dili nzima.

FACT: hizo 30% ambazo wewe unadai was in dispute, ndizo zilizomuwezesha Ruge kuiweka IPTL mufilisi under RITA kupitia mahakama. Kama ingekuwa hazitambuliki hilo liliwezekanaje?
Pili, kutokana na ripoti ya PAC, ruge alitambulishwa kwa sethi na prof Mhongo, ruge alilipwa "chake" (maneno ya zitto), sasa hapo alifahamu vipi dili?
 
Tanesco imeshtakiwa kwa kuwa ni mdhamini wa IPTL wakati IPTL inakopa ilipeleka barua zinazoonesha kuwa inalipwa pesa na Tanesco. Na tanesco ikaridhia
Na wakati wa mauzo Standard Charterd Bank iliweka zuio likatupwa na mahatma a zetu za kifisadi sasa wafanyaje wakaenda kufungua shauri kwenye mahakama zinazotenda haki na ninawahakikishia wana jamii tanesco itashindwa na italipa tutaona

Kuhusu mama Tiba umemtetea sana inawezekana alikuja hajui, lakini kutokujua sio kinga ya kuhusika, mfano ukikutwa na ngozi ya ngombe aliyeibiwa nawe ni muhusika Hata kama wewe ulipewa ngozi tu

Kimsingi nionavyo tanesco kama tanesco haina shida, tatizo limo kwa wanasiasa wanaoingilia utendaji wa tanesco, kama mawaziri, makatibu wakuu.

Hakuna kitu kibaya kama gari kukosa dereva Tanzania sasa haina kiongozi mkuu, kila mtu anajiamulia atakavyo wakes hakuna hapo juu yuko zuzu hivyo wanafanya watakavyo.

Haingii akilini mambo kama haya yanatendeka Rais yuko lakini yuko kimya hii ni hatari sana
 
Inashangaza sana hawa waliogawiwa kwa malboro pale mkombozi jinsi wanavyotapatapa. Yaani CAG anasema ni fedha ya umma na pia takukuru inasema ni fedha ya umma pia TRA. Bado jinga linakuja kubishana hapa. Unafaa kutemewa mate usoni!! Na kama ni za bank hao maccm na maasikofu waliozila nao ni wamiliki wa hiyo bank unayotaja? Acha ujinga we ni mtu mzima!!
 
sijatetea wizi wa pesa za umma, nimemtetea james rugemalira, kuna tofauti hapo. Elewa kuwa James rugemalira akirudisha pesa na yeye hapo
hapo atarudishiwa umiliki wa IPTL kwa asilimia 30! Kuna wizi gani hapo?

Kamati imeshapendekeza IPTL itaifishwe na kuwa Mali ua Umma na mm nashauri huyu Nshomile afilisiwe na kufungwa na hata hao ndugu waliopewa gawio hata humu JF watafutwe

cc

MANKA MUSA pendolyimo optimus prime Apollo 11 shadow recruit assanal pitapiti

Kwa mujibu wa Taarifa ya CAG na kuthibitishwa na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU fedha hizo pia ziligawiwa kwa watu mbalimbali binafsi. Kamati haina tatizo na watu wawili kuuziana makampuni yao kwa thamani wajuazo wenyewe, au jinsi ya kuzitumia fedha zao, ama kuwachagulia watu wa kuwagawia, lakini Kamati imejidhihirishia kuwa fedha iliyotumika kulipia manunuzi hayo ni fedha ambayo sehemu yake ni ya umma iliyochotwa bila huruma wala aibu, kutoka Benki Kuu. Hivyo, Kamati inazitaka mamlaka za uchunguzi kuhakikisha kuwa fedha hizo zinarudi Benki Kuu hata ikibidi kwa kufilisi mali za watu wote 97 waliofaidika na fedha hizo kwa thamani ya fedha walizopewa na Bwana Rugemalira
Aidha, Kamati imebaini kuwa Waziri wa Nishati na Madini ndiye alikuwa dalali mkuu aliyewakutanisha Bwana Harbinder Singh Sethi na Bwana James Rugemalira, tena katika ofisi ya Umma; na pengine hii ndiyo iliyokuwa sababu ya upotoshaji huu. Waziri wa Nishati na Madini alifanya udalali huo akijua dhahiri kuwa Bwana Sethi hana uhalali wa kisheria kufanya biashara kwa jina la IPTL.
 
Hao Standard Chartered walitakiwa wakaidai Mechmar walioikopesha na si IPTL wala TANESCO. Na kisheria Mechmar imefilisika, STANDARD CHARTERED wanatakiwa wadai Insurance yao lakini badala yake wanakuja kuidai TANESCO kwa kuwa tu TANESCO wamelala doro.

Wamelala doro kwa kuwa wangenunua wao wenyewe kwa mkopo mitambo mizuri zaidi ya hiyo na mpaka sasa deni lingekuwa limekwisha zamani na umeme kushuka bei.

TANESCO walikuwa wanajifikiria matumbo yao tu mpaka Kikwete alipokuja na kubadilisha mambo kwa kuamua kununuwa mitambo yetu wenyewe na si kukodisha tena, Kinyerezi I, II, III na IV.

Kudos Kikwete.
sina tusi la kukutukana matusi yote ya zamani ngoja nitafute jipya ahahahah
 
Back
Top Bottom