feyzal
JF-Expert Member
- Apr 20, 2016
- 6,805
- 12,672
Baada ya kusoma hili andiko mwanasport nikaona huyu Mchezaji ni mwehu na kuna wengi tu wa aina yake mfano Ajibu.
Nimekopi kama ilivyo kwenye gazeti la Mwanasport
MWAKA 2012 wakati wa Cecafa kule Uganda, niliupeleka ujumbe wa klabu ya El Merreikh ya Sudan ukiongozwa na ofisa habari wao, Idrissa Adelbagi Sheikh, kwenye kambi ya Tanzania Bara kufanya mazungumzo na Mrisho Ngassa.
Mazungumzo hayakwenda vizuri. Jamaa wakaondoka kurudi kwao Khartoum.
Baada ya mashindano wakaja Dar es Salaam na dau kubwa zaidi, dola ,000 na mshahara wa dola 5,000 kwa mwezi kwa Ngassa mwenyewe, na dola 100,000 kwa Azam Fc.
Siku hiyo Tanzania walikuwa wakicheza dhidi ya Somalia, Ngassa akafunga mabao 5 peke yake. Mwenyekiti El Merreikh kule Khartoum akapiga simu kusisitiza kwamba Ngassa lazima apatikane kwa vyovyote.
Jioni tukaonana na Ngassa na jamaa walikuwa na dau la dola 100,000 kwa Ngassa mwenyewe pamoja na mshahara wa dola 4,000 kwa mwezi, na dola 75,000 kwa klabu yake ya Azam FC.
Mazungumzo hayakwenda vizuri. Jamaa wakaondoka kurudi kwao Khartoum.
Baada ya mashindano wakaja Dar es Salaam na dau kubwa zaidi, dola 200,000 na mshahara wa dola 5,000 kwa mwezi kwa Ngassa mwenyewe, na dola 100,000 kwa Azam FC.
Azam FC ikakubali, lakini Ngassa mwenyewe hakupatikana. Tukaanza kumtafuta bila mafanikio.
Jamaa wakadhani Azam FC au mchezaji mwenyewe au wote wawili wanawafanyia uhuni...wakaongeza dau la dola 300,000 na mshahara hadi dola 6,000 kwa Ngassa, na dola 200,000 kwa klabu yake ya Azam FC.
Bado Ngassa hakupatikana. Mwenyekiti akapiga simu na kusema jamaa wasirudi bila Ngassa. Adelbagi akabaki hapa Dar es Salaam akihangaika na viongozi wa Azam FC na mimi kumtafuta Ngassa...bila mafanikio.
Baadaye akaondoka na kusema wameachana na mpango wa Ngassa.
Mimi binafsi nilihangaika sana kwa sababu waliniahidi dola 10,000 endapo mpango ungekamilika.
Kwa hiyo kujificha kwa Ngassa kulinivuruga mno kwa sababu kulinikosesha pesa nyingi sana.
El Merreikh walipoondoka, Ngassa akapatikana. Kumbe alikuwa amefichwa na Yanga kwenye hoteli ya Double Tree Hilton, Msasani Dar Es Salaam.
Lakini El Merreikh hawakukata tamaa. Wakanitumia tena mkataba mwingine wenye kipengele cha kumlipa Ngassa mshahara wake wote ambao wamekubaliana, endapo klabu ingeamua kuvunja mkataba katikati.
Nikamtafuta Ngassa na kuanza kuongea naye kumuelewesha maana ya mshahara wa dola 10,000 na dau la dola 400,000 la kusainia mkataba.
Wakati huo, dola moja ilikuwa sawa na Shilingi 1,800, kwa hiyo dola 10,000 ilikuwa sawa na Sh 18 milioni.
Nikam-wambia hiyo ni bei ya kununua kiwanja kilichopimwa, maeneo ya Mivumoni na Mbweni, ambacho wakati ule kilikuwa Sh. 15 milioni.
Kwa mkataba wake wa miaka 4, ilikuwa na maana kwamba angeweza kununua kiwanja kimoja kila mwezi na baada ya miezi 48, angekuwa na viwanja 48 katika maeneo ya kifahari ambayo baadaye
angeweza kuuza kwa bei mbaya sana.
Nikamuelewesha kuhusu kuwekeza kwa kununua dhamana za serikali. Nikamwambia dola 200,000 za kusainia mkataba, ukinunua dhamana za serikali, kila mwaka unapata mgawo wa 10%... sawa na dola 20,000.
Huo ulikuwa sawa na mshahara wake wa mwaka wa wakati huo akiwa Azam FC.
Tena hapo ilikuwa kabla signing fees haijapanda hadi Dola 300,000 na baadaye Dola 400,000.
Kiufupi, Ngassa katika miaka minne ya kucheza El Merreikh angeingiza mfukoni mwake Sh. 1.6 bilioni, hiyo ikiwa ni pesa ya kusaini mkataba na mishahara yake ya miezi 48. Hapo haujajumlisha na posho nyingine ambazo angepata kutokana na mafanikio ya timu.
Akanijibu, ‘tafuta pesa kwa nguvu zako, usitegemee nguvu zangu’.
Alinijibu hivyo baada ya kumueleza kwamba katika dili lile, mimi nilikuwa na dola elfu 10. Kwa hiyo akadhani nahangaikia maslahi yangu pekee bila yeye kufaidika.
Nikatafuta namba ya baba yake, mzee Khalfan Ngassa, na kumuelewesha haya mambo niliyokuwa namuelewesha mwanaye.
Mzee akasema yeye mwenyewe anasikia kwa watu tu...Mrisho hajawahi kumwambia hata mara moja.
Nikawajibu El Merreikh kwamba Ngassa hapatikani. Ndipo wakaangukia kwa Suleiman Ndikumana wa Burundi, ambaye kwenye ile Cecafa aliifungia Burundi bao moja dhidi ya Tanzania Bara, na kuisaidia timu yake kushinda 1-0.
Leo Ngassa analalamika Yanga hawamjali yeye mzawa...anasahau kwamba alipoteza nafasi yeye mwenyewe.
El Merreikh walikuwa tayari kumlipa pesa zote hizo na kumgharamia kila kitu kule Sudan (yaani hata angeshindwa kutamba angelipwa pesa zote).
Leo angekuwa na dola 400,000 kwenye dhamana ya serikali maana yake angekuwa na uhakika wa dola 60,000 kila mwaka (sawa na Sh. 11 milioni kila mwezi).
Asingekuwa mtu wa kuilalamikia Yanga, badala yake angekuwa mtu wa kuisaidia Yanga kama alivyokuwa akifanya Mwinyi Zahera.
Pole sana Ngassa. Ingekuwa busara ungeamua kusema hadharani namna ambavyo uliivuruga kesho yako wewe mwenyewe ili kizazi kinachoibukia kijifunze kutoka kwako.
ANDIKO NIMEKOPI GAZETI LA MWANASPORT
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekopi kama ilivyo kwenye gazeti la Mwanasport
MWAKA 2012 wakati wa Cecafa kule Uganda, niliupeleka ujumbe wa klabu ya El Merreikh ya Sudan ukiongozwa na ofisa habari wao, Idrissa Adelbagi Sheikh, kwenye kambi ya Tanzania Bara kufanya mazungumzo na Mrisho Ngassa.
Mazungumzo hayakwenda vizuri. Jamaa wakaondoka kurudi kwao Khartoum.
Baada ya mashindano wakaja Dar es Salaam na dau kubwa zaidi, dola ,000 na mshahara wa dola 5,000 kwa mwezi kwa Ngassa mwenyewe, na dola 100,000 kwa Azam Fc.
Siku hiyo Tanzania walikuwa wakicheza dhidi ya Somalia, Ngassa akafunga mabao 5 peke yake. Mwenyekiti El Merreikh kule Khartoum akapiga simu kusisitiza kwamba Ngassa lazima apatikane kwa vyovyote.
Jioni tukaonana na Ngassa na jamaa walikuwa na dau la dola 100,000 kwa Ngassa mwenyewe pamoja na mshahara wa dola 4,000 kwa mwezi, na dola 75,000 kwa klabu yake ya Azam FC.
Mazungumzo hayakwenda vizuri. Jamaa wakaondoka kurudi kwao Khartoum.
Baada ya mashindano wakaja Dar es Salaam na dau kubwa zaidi, dola 200,000 na mshahara wa dola 5,000 kwa mwezi kwa Ngassa mwenyewe, na dola 100,000 kwa Azam FC.
Azam FC ikakubali, lakini Ngassa mwenyewe hakupatikana. Tukaanza kumtafuta bila mafanikio.
Jamaa wakadhani Azam FC au mchezaji mwenyewe au wote wawili wanawafanyia uhuni...wakaongeza dau la dola 300,000 na mshahara hadi dola 6,000 kwa Ngassa, na dola 200,000 kwa klabu yake ya Azam FC.
Bado Ngassa hakupatikana. Mwenyekiti akapiga simu na kusema jamaa wasirudi bila Ngassa. Adelbagi akabaki hapa Dar es Salaam akihangaika na viongozi wa Azam FC na mimi kumtafuta Ngassa...bila mafanikio.
Baadaye akaondoka na kusema wameachana na mpango wa Ngassa.
Mimi binafsi nilihangaika sana kwa sababu waliniahidi dola 10,000 endapo mpango ungekamilika.
Kwa hiyo kujificha kwa Ngassa kulinivuruga mno kwa sababu kulinikosesha pesa nyingi sana.
El Merreikh walipoondoka, Ngassa akapatikana. Kumbe alikuwa amefichwa na Yanga kwenye hoteli ya Double Tree Hilton, Msasani Dar Es Salaam.
Lakini El Merreikh hawakukata tamaa. Wakanitumia tena mkataba mwingine wenye kipengele cha kumlipa Ngassa mshahara wake wote ambao wamekubaliana, endapo klabu ingeamua kuvunja mkataba katikati.
Nikamtafuta Ngassa na kuanza kuongea naye kumuelewesha maana ya mshahara wa dola 10,000 na dau la dola 400,000 la kusainia mkataba.
Wakati huo, dola moja ilikuwa sawa na Shilingi 1,800, kwa hiyo dola 10,000 ilikuwa sawa na Sh 18 milioni.
Nikam-wambia hiyo ni bei ya kununua kiwanja kilichopimwa, maeneo ya Mivumoni na Mbweni, ambacho wakati ule kilikuwa Sh. 15 milioni.
Kwa mkataba wake wa miaka 4, ilikuwa na maana kwamba angeweza kununua kiwanja kimoja kila mwezi na baada ya miezi 48, angekuwa na viwanja 48 katika maeneo ya kifahari ambayo baadaye
angeweza kuuza kwa bei mbaya sana.
Nikamuelewesha kuhusu kuwekeza kwa kununua dhamana za serikali. Nikamwambia dola 200,000 za kusainia mkataba, ukinunua dhamana za serikali, kila mwaka unapata mgawo wa 10%... sawa na dola 20,000.
Huo ulikuwa sawa na mshahara wake wa mwaka wa wakati huo akiwa Azam FC.
Tena hapo ilikuwa kabla signing fees haijapanda hadi Dola 300,000 na baadaye Dola 400,000.
Kiufupi, Ngassa katika miaka minne ya kucheza El Merreikh angeingiza mfukoni mwake Sh. 1.6 bilioni, hiyo ikiwa ni pesa ya kusaini mkataba na mishahara yake ya miezi 48. Hapo haujajumlisha na posho nyingine ambazo angepata kutokana na mafanikio ya timu.
Akanijibu, ‘tafuta pesa kwa nguvu zako, usitegemee nguvu zangu’.
Alinijibu hivyo baada ya kumueleza kwamba katika dili lile, mimi nilikuwa na dola elfu 10. Kwa hiyo akadhani nahangaikia maslahi yangu pekee bila yeye kufaidika.
Nikatafuta namba ya baba yake, mzee Khalfan Ngassa, na kumuelewesha haya mambo niliyokuwa namuelewesha mwanaye.
Mzee akasema yeye mwenyewe anasikia kwa watu tu...Mrisho hajawahi kumwambia hata mara moja.
Nikawajibu El Merreikh kwamba Ngassa hapatikani. Ndipo wakaangukia kwa Suleiman Ndikumana wa Burundi, ambaye kwenye ile Cecafa aliifungia Burundi bao moja dhidi ya Tanzania Bara, na kuisaidia timu yake kushinda 1-0.
Leo Ngassa analalamika Yanga hawamjali yeye mzawa...anasahau kwamba alipoteza nafasi yeye mwenyewe.
El Merreikh walikuwa tayari kumlipa pesa zote hizo na kumgharamia kila kitu kule Sudan (yaani hata angeshindwa kutamba angelipwa pesa zote).
Leo angekuwa na dola 400,000 kwenye dhamana ya serikali maana yake angekuwa na uhakika wa dola 60,000 kila mwaka (sawa na Sh. 11 milioni kila mwezi).
Asingekuwa mtu wa kuilalamikia Yanga, badala yake angekuwa mtu wa kuisaidia Yanga kama alivyokuwa akifanya Mwinyi Zahera.
Pole sana Ngassa. Ingekuwa busara ungeamua kusema hadharani namna ambavyo uliivuruga kesho yako wewe mwenyewe ili kizazi kinachoibukia kijifunze kutoka kwako.
ANDIKO NIMEKOPI GAZETI LA MWANASPORT
Sent using Jamii Forums mobile app