hello wadau, nilikuwa nasikiliza STARTV kipindi cha Tuongee Siasa na uchumi. mtaalamu toka Policy Forum kabainisha kuwa kumbe tayari rasimu ya Sera ya Madini imeshatayarishwa na itajadiliwa katika kikao cha bunge kitakachoanza karibuni. Cha ajabu ni kuwa Development Partners na mining companies ndo wameshirikishwa zaidi katika utengenezaji wa sera yenyewe na watanzania wenye madini yao kutoshirikishwa vya kutoshwa.
kama kuna mtu ana hiyo sera tafadhali tuwekeeni hapa na sisi tuione na kutoa maoni. Maoni tutakayotoa yanaweza kusaidia wabunge watakaoijadili bungeni.
jingine, je kuna uwezekano wa kutoa pingamizi mahakamani suala hili lisijadiliwe bungeni hadi watanzania washirikishwe kutoa maoni.
kama kuna mtu ana hiyo sera tafadhali tuwekeeni hapa na sisi tuione na kutoa maoni. Maoni tutakayotoa yanaweza kusaidia wabunge watakaoijadili bungeni.
jingine, je kuna uwezekano wa kutoa pingamizi mahakamani suala hili lisijadiliwe bungeni hadi watanzania washirikishwe kutoa maoni.