Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Ni baada ya gari alilokuwa anasafiria huko Singida kupasuka tairi la mbele na kupinduka mara tatu. Alikuwa katika ziara ya kikazi kukagua barabara akitokea mkoani Manyara. Ndio kwanza alikuwa amewasili mkoani humo. Washuhuda wanasema Chibulunje aliokolewa na airbags ambazo zimemfanya asiumie sana. hata dereva wake na meneja wa Tanroads mkoani humo nao hawakuumia sana lakini inaelezwa Chibulunje alipatwa na mshituko wa moyo baada ya ajali ingawa ametibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani kupumzika
Last edited by a moderator: