Kumbe upo mbali sana uelewa. Nikupe shule ndogo:
Kwenye vita, mwenye nguvu anakupiga ili baadaye mkae mezani ukubali matakwa yake ukiwa kwenye hali dhaifu, ukijua kuwa ukikataa unarudia kwenye hali ya hatari.
Hata mataifa yaliyokuwa makoloni, yalipambana kwa vita, lakini mwishoni walikaa na nchi watawala mezani ili kufikia maafikiano ya mwisho. Hata Putin anaipiga Ukraine, huku akiwa ameweka mapendekezo yake kama Ukraine inataka vita iishe. Hata Tanzania ilipoizidi uwezo Uganda, kilichofuatia ilikuwa ni kuwataka waganda waweke utawala mpya ambao si adui kwetu. Israel inaipiga Lebanon, lakini baada ya kuona imekwishaidhoofisha, imeitaka Lebanon waende kwenye mazungumzo, huku Lebanon ikiwa dhaifa, na hivyo Israel italazimisha matakwa yake ya kutaka Hezbollah wanyang'anywe silaha. Hata ukiwa na nguvu, hakuna vita ambayo utapigana na Taifa jingine, ukalishinda, halafu baada ya hapo mkawa katika utulivu bila ya mazungumzo ya mezani yatakayoondoa uhadama. Marekani inaipiga Iran ili idhoofike, halafu ilazimishe matakwa yake. Lakini kama Iran inaona bado ina uwezo wa kupigana, itaendelea, ili wakienda kwenye mazungumzo, isiende ikiwa dhaifu. Kitu ambacho Marekani na Israel hawatataka, hivyo kuna uwezekano wataendelea kuipiga mpaka ifike Iran ione kuendelea na vita ni kuangamia, na hivyo aheri kuridhia matakwa ya Marekani ili kujiokoa.
Kwenye haya mazungumzo ya sasa, Marekani iliamini kuwa tayari Iran ipo dhaifu kiasi cha kukubali chochote ili nchi iwe salama. Lakini Iran inaona bado inaweza kuendelra kupigana.