Neno Moja kwa Kikundi cha Futuhi Startv

Neno Moja kwa Kikundi cha Futuhi Startv

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,270
Nyie kikundi cha Futuhi cha startv, kwa nini mnafikiri kwamba kushikana mashati, kuzabana vibao na kukimbizana ili kumkata mwingine mtama ni kichekesho?
Mnaniudhi sana kwa jinsi mnavyokwaruzana kwenye kila episode zenu mkidhani kwamba mnachekesha/kuburudisha.
Betri za remote yangu zinaisha haraka sana kwa sababu nabadili channel kila mnapotokeza kwenye screen ya tv yangu.
Jifunzeni maana ya ucheshi na namna ya kuchekesha!
 
bro utakuwa umevurugwa tu.......kwa sasa hakuna best comedias ktk nchi hii km futuhi........

Kama futuhi huwa wanakuchekesha, basi wewe unaweza ukaangalia rangi mbichi iliyopakwa ukutani ikikauka na ukaona inachekesha.
 
mi hawanichekeshi kwakweli but bi mkubwa huwa anawapenda hadi namshangaa
 
wanatumia nguvu nyingi kuliko akili katika uchekeshaji wao. Hata hivyo uchekeshaji wa kupigana mitama na kabali za uongo ulikwisha pitwa na wakati. Hayo wawaachie watoto wa shule ya msingi wanaojifunza maigizo.Unapokuwa prophesional inabidi uende hatua mbali zaidi ya hapo.
 
SHIEKA, umemaliza kila kitu.

Kinachonisikitisha ni kuwa watz wengi eti wanafurahishwa, binafsi watu wanaopenda hizo komedi nawakadiria viwango vya chini sana vya uelewa... kuna wengine wanaitwa mizengwe, mwanangu darasa la nne haangalii hizo komedi...
 
Last edited by a moderator:
Vipi mbona hachambui na OK wa TBC1 au wakina Shabaan?
 
wanatumia nguvu nyingi kuliko akili katika uchekeshaji wao. Hata hivyo uchekeshaji wa kupigana mitama na kabali za uongo ulikwisha pitwa na wakati. Hayo wawaachie watoto wa shule ya msingi wanaojifunza maigizo.Unapokuwa prophesional inabidi uende hatua mbali zaidi ya hapo.

Kuna shughuli moja hivi mwaka juzi, Mpoki alikuwa host, alipiga suti na alipiga stand up comedy ya kwenda shule stejini kama dk 15 hivi, watu walivunjika mbavu!! Wangeanza kujikita huku kwenye stand up comedy, ila sio kama ya vuvuzela! Stand up comedy inachagizwa na matukio ya kila siku ktk jamii kutoka kwa wanasiasa, wasanii, nk!
 
Wajifunze kwa akina joti,masanja na mpoki OK, ni wabunifu sana,show haiwezi kupita bila kipengele kitakacho kugusa ucheke mpaka utoe machozi
 
bro utakuwa umevurugwa tu.......kwa sasa hakuna best comedias ktk nchi hii km futuhi........

Kutokuwepo best comedians katika nchi hakuondoi ukweli kwenye mada ya SHIEKA, vichekesho vya kukimbizana vishapitwa na wakati mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Jambo moja la msingi ni kutamani na kutafuta mafanikio kwa nguvu na akili zote. Sio tu kwenye sanaa, bali maisha kwa ujumla. Wengi tumekwama hapo, hatujui nini haswa tunataka kwenye maisha. Sisi ni vile tunavyofikiri kwa hiyo jinsi tulivyo ndio tulivyofikiri na tumekua hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Kwenye game ya comedy ki EA Kansiime is the best
Ndiyo, huyo dada anajitahidi sana ila wakatki mwingine anapotoka pale anapomshambulia mtu kwa maneno makali na yenye kudhalilisha.
 
Watu wengi wana wanakifurahia so wewe anzisha Chako AU kwani lazma uangalie. Ovyooooooooo.....
 
SHIEKA, umemaliza kila kitu.

Kinachonisikitisha ni kuwa watz wengi eti wanafurahishwa, binafsi watu wanaopenda hizo komedi nawakadiria viwango vya chini sana vya uelewa... kuna wengine wanaitwa mizengwe, mwanangu darasa la nne haangalii hizo komedi...
Umenena Lukansola. Wanaochekeshwa na futuhi pia wanachekeshwa na mtu anayecheua!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom